Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94

MMMMH...SHEMEJI HAPANA!!!?? 04

14th Apr, 2025 Views 40

Story……………….MMMMH...SHEMEJI HAPANA!!!?? 04
Mtunzi…………….SIMULIZI ZA ZOOPER
Whatsap………....0613083801/0748697173
Umri………………..18+

ENDELEA.........
Nilimtimua na shemeji Rashidi aliondoka na mimi nilirudi kitandani na kukaa huku nikiendelea kuwaza kile kilichotokea, baadae nilipata wazo na kuanza kukunja nguo zangu.
"Siwezi kuendelea kukaa hapa tena sitaweza kumuangalia dada Aisha usoni" niliongea mwenyewe huku nikikunja nguo zangu na kuziweka kwenye begi.

Baada ya kumaliza nilienda kuoga na bahati nzuri shemeji Rashidi alitoka na kwenda kazini na kuniacha mimi mwenyewe nyumbani. Baada ya kumaliza kuoga nilivaa nguo na kubeba begi na kuianza safari ya kurudi nyumbani pasipo kumuaga mtu yoyote yule.

Nilifika nyumbani na mama alishangaa kuniona maana sikumjulisha kama nitakuja siku hiyo.
"Fatuma mbona gafra sana!?"
"Mama nahitaji kupumzika kwa sasa, tutaongea baadae" nilimwambia na kuingia kwenye chumba changu kwa ajili ya kupumzika pasipo kumwambia mama sababu iliyonitoa kwa dada haraka kiasi kile.

Masaa kadhaa yalipita nikiwa nyumbani na mda huo nilikuwa tayari nimeshaamka, sikutaka kumwambia mama kile kilichonitokea ila simu yangu iliita na mpigaji alikuwa ni dada Aisha, moyo wangu ulienda mbio baada ya kuona dada akinipigia simu ila nilijikakamua na kuamua kuipokea.
"Fatuma mbona umeondoka pasipo kutupa taarifa!?" Dada aliniuliza.
"Utanisamehe dada yangu nilimkumbuka mama ndiyo maana nikaamua kuja nyumbani mara moja" nilimjibu na baadae dada aliniambia.
"Yote sawa lakini kwanini uondoke pasipo kutuambia na chumba umekiacha hovyo huku ukiwa umemwaga chai chini na kupasua sahani pasipo ata kukifanyia usafi!?" Swali la dada lilinifanya nikumbuke kile kilichotokea asubuhi ila niliamua kumuomba msamaha na kumwambia kuwa nilikuwa na haraka ndiyo maana sikukisafisha chumba nilichokuwa nikilala.

Maongezi yetu mama alikuwa akiyasikia na baadae aliamua kuniuliza.
"Hiyo ndiyo sababu iliyokutoa kwa dada yako!?"
"Ndiyo mama ata hivyo mimi siwezi kurudi huko tena na uzuri shemeji ameahidi mwenyewe atanisaidia kunitafutia kazi" nilimjibu mama na bahati nzuri mama alinielewa na hakuendelea tena kuniuliza maswali.

Siku hiyo ilipita nikiwa nyumbani na siku iliyofata shemeji Rashidi alinipigia simu lakini sikutaka kuipokea na baada ya kuona sipokei simu alinitumia ujumbe wa kunipa taarifa kuwa tayari ameshafanikisha kunitengenezea mpango wa kufanyakazi kwenye hospital aliyokuwa akifanyiakazi yeye. Kiukweli nilijikuta nikifurahi nakusahau kile alichonifanyia shemeji Rashidi maana niliamini ndoto yangu inaenda kutimia.

Haikupita mda shemeji Rashidi alinipigia simu na mimi sikutaka kuacha kuipokea kama nilivyokuwa nikifanya mwanzo, niliipokea na Shemeji Rashidi aliongea.
"Kesho kutwa unatakiwa ufike haraka kazini" aliniambia na kukata simu na hakutaka kunipa nafasi ya mimi kumuuliza.

Niliamua kumtumia ujumbe nikimtaka anipe maelezo vizuri lakini shemeji Rashidi hakunijibu zaidi ya kukaa kimya.
Sikutaka kuendelea kuumiza kichwa kwa kitendo cha shemeji Rashidi kutokujibu ujumbe wangu hivyo nilipanga kuondoka nyumbani siku inayofata kwa ajili ya kwenda kuishi kwa dada kwa mda kwani kulikuwa na ukaribu mkubwa na sehemu niliyotakiwa kufanya kazi.

Siku iliyofata niliondoka nyumbani na kwenda nyumbani kwa dada Aisha na nilimkuta akiwa mwenyewe huku shemeji Rashidi akiwa kazini.
"Hongera mdogo wangu kwa kupata kazi shemeji yako amekupambania sana" dada alinipa pongezi na mimi niliamua kuzipokea pongezi zake.

Baada ya masaa kwenda shemeji Rashidi aliweza kurudi nyumbani na alinikuta nikiwa nimekaa mwenyewe sebleni, alinipita pasipo ata kunisemesha na mimi kidogo nilianza kujiuliza amepatwa na kitu gani shemeji Rashidi mpaka kuamua kuninunia kiasi kile!!.

Siku hiyo ilipita bira shemeji Rashidi kuniongelesha na siku iliyofata nilijiandaa mapema ili niweze kuelekea kazini maana ndiyo ilikuwa siku yangu ya kwanza. Niliongozana na shemeji Rashidi kwenda kupanda kwenye gari yake na mpaka mda huo shemeji Rashidi alikuwa hataki kabisa kuniongelesha, wote tulikuwa kimyaa ndani ya gari huku tukiendelea na safari ya kuelekea hospital.

Baada ya safari ya dekika kadhaa shemeji Rashidi aliipaki gari yake pembeni na kuniongelesha kwa mara ya kwanza.
"Ivi Fatuma unajua nimepambana kiasi gani mpaka kukutafutia nafasi wewe pale kazini!?"
"Sijui shemeji" nilimjibu na shemeji Rashidi aliongea.
"Kwakuwa hujui ngoja nikwambie sasa, nimetoa pesa nyingi sana ili waweze kukuajiri wewe na mimi niliamua kukusaidia wewe sio kwa sababu ni shemeji yangu ila ni kwakuwa nakupenda na nahitaji uwe mtu wangu" shemeji Rashidi aliongea kwa hisia.
"Wewe tayari ni mme wa dada haiwezekani mimi kuwa pamoja na wewe" nilimjibu pasipo kumuangalia usoni.
"Kwani mimi nimekwambia nataka nikuoe Fatuma!? mimi ninachotaka kwako ni mapenzi tu na sio kingine".
"Mmmmh shemeji hiyo haitawezekana siku dada akijua hatonisamehe na italeta picha mbaya kwa upande wangu"
"Oooh basi chagua moja ushuke kwenye gari yangu na hutopata kazi au ukubali kuwa unafanya mapenzi na mimi kisiri ili upate kazi" shemeji Rashidi aliniambia, nilibaki njia panda kutokana na kile alichokiongea......ITAENDELEA..

Za hivi punde ni za 🔥🔥🔥 | Sema Jambo

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest