Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94

MMMMH...SHEMEJI HAPANA!!!?? 10

14th Apr, 2025 Views 5

Story……………….MMMMH...SHEMEJI HAPANA!!!?? 10
Mtunzi…………….SIMULIZI ZA ZOOPER
Whatsap………....0613083801/0748697173
Umri………………..18+

ENDELEA.........
Baadae alitupita nakuendelea na safari.
"Fatuma leo usiku nakuja kulala kwako kipenzi" Nasir alizungumza.
"Nilishakwambia mpaka ndoa ndiyo utapata utamu Nasir kuwa mwelewa tafadhali!!"
"Kwani bado bikra mpaka uniambie mpaka ndoa!!?"
"Sio bikra ila tu nimeshafanya maamuzi Nasir kama unanipenda utafata maamuzi yangu"
"Sasa kama sio bikra kwanini ukatae kulala na mimi au hunipendi!?" Nasir aliongea kwa kulalamika akitaka nikubali kumpa tunda la kati.
"Kwani kuna shida gani tukioane alafu unile mpaka unikinai mwenyewe!?"
"Hakuna ubaya wowote ila sio haki hii Fatuma kabisa!! kama mwanaume aliyekutoa bikra ulikubali kumpa kwanini isiwe mimi! nitaanzaje kukuamini kama kweli unanipenda!?" nyie hiyo siku Nasir alilalamika akinitaka nikubali kufanya nae mapenzi ila niliendelea kumuwekea ugumu huku nikiwa na lengo langu.

Bahati nzuri kuna mfanyakazi mwenzetu alifika na kumwambia Nasir kuwa kuna mgonjwa anayetakiwa kwenda kumhudumia, Nasir aliondoka na mimi niliendelea na kazi zangu.

Mda wa kwenda nyumbani ulipofika niliondoka na kwenda nyumbani kwangu na hazikupita dekika 5 dada Aisha alinipigia simu na kuniambia.
"Fatuma njoo nyumbani mara moja"
"Nije nyumbani kwani kuna kitu gani dada!?" nilimuuliza huku nikiwa na wasiwasi mkubwa na hofu yangu ilikuwa ni siri iliyokuwepo kati yangu na shemeji Rashidi hivyo niliamua kumuuliza dada lakini hakutaka kuniambia sababu ya kunitaka niende nyumbani kwake.

Nilitamani kumtafuta shemeji Rashidi ili nimuulize kuna shida gani!? ila nafsi nyingine ilinisuta hivyo nilijiandaa na kwenda nyumbani kwa dada.

Haikuchukua mda niliweza kufika nyumbani kwa dada huku nikiwa na wasiwasi, nilifungua mlango na mtu wa kwanza kumuona alikuwa ni shemeji Rashidi aliyekuwa amekaa kwenye kochi.
"Shemeji za mida!!" nilitoa salamu kwa shemeji Rashidi lakini hakunijibu na mda huo huo dada alifika na kunikuta nikiwa nimesimama.
"Fatuma bora ata umekuja shemeji yako kaninunia toka atoke kazini na hataki kunisemesha kabisa labda uongee nae wewe huenda atakuelewa" Dada Aisha aliongea na mimi ndani ya moyo wangu nilisijemea kama ningejua kitu alichoniitia dada basi nisingekubali kuja.
"Aya dada ngoja nijaribu kuongea na shemeji" nilimjibu ili kumlizisha, baadae dada aliondoka na kutuacha sisi wawili hapo ndipo kimbembe kingine kilipoanzia maana nilishindwa nianze wapi kumuongelesha shemeji.
"Usije ukajaribu kunisogelea Fatuma nitakupiga hicho kibao ambacho hujawahi kupigwa" shemeji Rashidi aliniambia kwa sauti ya chini iliyojaa msisitizo.

Niliamua kunyenyuka na kumfata dada, nilimkuta akiwa jikoni akipika.
"Umeshaongea nae tayari!?" Dada Aisha aliniuliza, haraka niliwaza ni kitu gani nachotakiwa kuongea mbele ya dada hivyo niliamua kutunga uongo mbele yake.
"Eeeh dada nimeshaongea"
"Kakwambia shida nini inayomfanya awe kimya kiasi kile!?"
"Chakula dada, tatizo ni chakula unachompikia leo, amesema hajisikii kabisa kula chakula unachompikia" nilitunga uongo wangu mbele ya dada.
"Mbona ndiyo chakula anachopenda na ata hivyo kaninunia kabra ata sijaanza kupika chakula"
"Mmmh ila mimi ndiyo kaniambia hivyo sasa" nilimjibu na baadae ilibidi nimuage maana sikutaka kuendelea kukaa nyumbani kwa dada licha ya kuwa ilikuwa ni usiku.

Niliondoka na kwenda nyumbani kwangu na kabra ata sijafungua mlango Dr Nasir alinipigia simu hivyo niliamua kuipokea simu.
"Fatuma nipo mtaa wenu na ninazawadi zako hapa kipenzi changu, nielekeze vizuri ili niweze kufika kwako maana nimeshapasahau" Nasir aliongea na mimi nilijua ni mtego ili aweze kufanya sex na mimi ila sikutaka kuziacha zawadi alizokuja nazo.
"Basi nisubiri nakuja kukufata hapo ulipo" Nasir alikata simu na mimi niliondoka na kumfata mahali alipokuwa. Nilifika na kumkuta akiwa kwenye gari yake.
"Ingia ndani ya gari unielekeze njia vizuri kipenzi" Nasir alizungumza na mimi nilikiri kuwa hiyo siku ni ngumu kuchomoka kwenye mtego wa Nasir aliyeonesha uhitaji mkubwa wa kutaka kufanya mapenzi na mimi.

Niliingia ndani ya gari nakuanza kumwelekeza na baada ya mda tulifika mahali nilipokuwa nikiishi. Nasir alikuwa wa kwanza kuteremka na kwenda kufungua buti ya gari na kuanza kutoa vitu alivyokuwa amekuja navyo huku kukiwa na mchele, mafuta na vitu vingine vingi.

Nilienda kufungua mlango huku nikisaidizana na Nasir kuingiza vitu alivyokuwa ameniletea kama zawadi.

Baada ya kufungua mlango mimi na Nasir tulisaidizana kuingiza vitu na baadae Nasir alinisogelea na kunikumbatia.
"Leo nataka nilale hapa kipenzi changu" aliongea huku akiyashika makalio yangu.
"Lakini sin...
"Sitaki uendelee kuongea Fatuma maana najua hutaki kuona nikilala hapa" aliniambia na baadae alinisogezea mdomo wake akihitaji tukisiane.

Ningeanzaje kukataa sasa na ukizingatia kaniletea zawadi za kutosha. nilikubali kumkiss kitu kilichokuwa na lilikuwa kosa nililolifanya kwani Nasir alipandwa na hisia na kushikwa na upwiru wa hatari. Nikiwa Sina hili wa lile alinisukumia kwenye kochi nakuanza kufungua mkanda wa suruali, nilibaki nikimwangalia mpaka pale alipomaliza kufungua mkanda wa suruali yake na kuivua kabisa.

Baadae alinisogelea na kunitaka nimpe ushirikiano. Kiukweli kuna mda moyo wangu ulikuwa mzito kukubali lakini mwenzangu damu yake tayari ilikuwa imeshaanza kuchemka hivyo ilikuwa ngumu kwangu kumkwepa.

Nasir alivyoona najishauri alinivulisha nguo mwenyewe na kuzitoa zote kwenye mwili wangu. Siku hiyo kwa mara ya kwanza mimi na yeye tulifanya mapenzi japo shemeji Rashidi alikuwa anaufundi wa uangalau kwenye kufanya mapenzi kuliko Nasir.

Nasir alishinda nyumbani kwangu usiku huo na siku iliyofata asubuhi na mapema dada alinipigia simu. Niliipokea simu yake na dada Aisha aliniambia kuwa shemeji Rashidi aliondoka usiku uliopita nyumbani na hakurudi tena.
"Yani hapa nimechanganyikiwa Fatuma nahisi kabisa shemeji yako ameshapata mwanamke huko nje na nikimjua huyo mwanamke lazima anitambue vizuri ata kwa waganga nitaenda Fatuma"
"Mmmmh dada pole kwa hilo ila jaribu kufatilia vizuri" nilimjibu na nikiwa bado naendelea kuongea nae mikono ya Nasir ilianza kuyashika makalio yangu kwa kuyapapa.....ITAENDELEA.

Full Tsh1000 namba za malipo ????????????

0613083801 HALOPESA JINA JOHN BUGUMBA

0755271203 M-PESA JINA JOHN BUGUMBA.

Za hivi punde ni za 🔥🔥🔥 | Sema Jambo

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest