PENZI LA MHALIFU 31
Cyborg aliniambia kuwa ata yeye alishangaa kuona boss wake Salome akitengeneza ukaribu na yeye na ilifika kipindi alikuwa akimruhusu kuondoka na gari lake Cyborg aliniambia ndiyo sababu iliyopelekea yeye na Afande Joel wawe kwenye ugomvi.
"Basi kama ni hivyo sitaki kukuona tena ukitengeneza mazoea na huyo boss wako sababu mda wowote ule mnaweza kuzagamuana" nilimwambia kama yeye alivyokuwa akinikataza kuwa karibu na asikari wenzangu wa kiume na mimi sikutaka kumuona akiwa karibu na boss wake lakini Cyborg alinihakikishia hakuna chochote kile kilichokuwa kikiendelea kati yao.
Baada ya kuniambia hivyo nilikumbuka kitu na kuamua kumuuliza.
"Kwanini ile siku hukutaka ata kunishika na wala hukuwa na habari na mimi!?" Nilimuuliza nikimaanisha ile siku tuliyolala bira Cyborg kunishika wala kufanya chochote na mimi.
"Malaika ile siku nilikuwa na mawazo tu na kilichokuwa kinanifanya niwaze ni lini na mimi nitakuwa na gari langu na kununulia wewe sababu nimeshaanza kuuona umhimu wa kumiliki gari" Cyborg aliongea na mimi ilibidi nikubaliane na maneno yake japo sikulidhika nayo.
Baada ya kuona nimemuuliza kuhusu sisi kutokufanya mapenzi Cyborg alianzisha palepale utundu wake kwa kunibeba na kunipeleka chumbani na tulivyofika huko tulianza mizagamuo.
Siku hiyo ilipita na siku iliyofata asubuhi na mapema nilipigiwa simu na mama na aliniambia kuwa mdogo wangu wa kike anayeitwa Anna atakuja kunitembelea hivyo nijiandae kwenda kumpokea.
Sikutaka kukataa sababu ndiye mdogo wangu wa pekee niliyekuwa nae hivyo niliacha maagizo kwa dada wa kazi ya kwenda kumpokea na mimi nilielekea moja kwa moja kazini kwangu.
Anna alikuwa bado akisubiri ajira na kwa wakati huo hakuwa na kazi yoyote ile ya maana na kiukweli mimi pamoja na mdogo wangu tulikuwa tukifanana karibu kila kitu.
Nilifika kazini na kuendelea na kazi zangu kumbe Afande Joel alikuwa bado ana lake kichwani, nilishangaa kumuona akinifata nakuanza kuniongelesha kwa hasira.
"Mme wako anajifanya mjanja na anataka kushindana na mimi sio!? subiri ataona" aliongea bira kujali kama kuna asikari wengine waliokuwa wakitusikia.
"Kwani umechanganyikiwa au!? emu nitolee umalaya wako hapa" ilibidi nimwambie na alikasirika baada ya mimi kumuita malaya.
"Unaniita malaya!?" aliongea na kunyenyua mkono wake ili anipige lakini tayari nilikuwa nimeshamgundua.
Haraka niliuzuia mkono wake na baadae asikari wenzetu walisogea kwa ajili ya kututuliza.
Kiukweli Afande Joel alinifanya nichukue siku hiyo na kuna mda nilikuwa nikikikumbuka kituo changu cha kazi nilichokuwa nikifanyia kazi mwanzo.
"Afande Joel una matatizo gani mbona unamletea vulugu Afande Angel!?" Afande mwenzetu alimuuliza na Afande Joel aliishia kumwambia maneno ambayo hayaeleweki.
Kelele zetu zilimfikia mpaka mkuu wetu na haraka tuliletewa taarifa za kuhitajika na mkuu mwenyewe.
Baada ya kupewa taarifa tuliamua kuongozana na njiani hamna aliyekuwa anamwongelesha mwenzake mpaka tulipofika kwenye ofisi ya mkuu wetu.
Tulifika na mkuu alituuliza shida nini na kwanini tunapiga kelele kwenye kituo cha kazi!?.
Mkuu alionekana kutofurahishwa na kile kilichotokea ila mimi niliamua kumwambia ukweli ili kama yakitokea matatizo mengine niwe na sehemu ya kujitetea.
Nilimwambia yote kuanzia pale Afande Joel alipokuwa akinishawishi tuweze kufanya mapenzi na yote aliyomfanyia Cyborg ya kumloga ili asiweze kusimamisha.
Baada ya kumwambia mkuu alimtazama Afande Joel.
"Afande Joel wewe siumeoa kabisa mbona bado unatamani kumzagamua Angel hujui kama ni asikari mwenzako na unatakiwa kumheshimu!?" alimuuliza ila Afande Joel alikuwa kimya tu.
"Nisamehe mkuu" Afande Joel aliamua kumjibu.
"Sio nikusamehe mwambie hapa hapa kuwa hutomsumbua tena na hutomfatilia mme wake" Mkuu alimwambia na Afande Joel alinigeukia na kuniambia kama alivyoambiwa aongee mbele yangu.
"Hii iwe mara ya mwisho fanya kilichokuleta hapa lasivyo utakuja kunilaumu baadae kwa maamuzi nitakayoyachukua ikiwa utaendelea na tabia hii" baada ya mkuu kuongea alimwambia Afande Joel aondoke na kuniacha mimi mwenyewe ofisini kwa mkuu kwani alidai kuna kitu anachohitaji kuniambia.
Kiukweli nilikuwa kwenye hofu sababu sikujua mkuu anataka kuniambia kitu gani, niliogopa na niliombea asije kunitongoza na kuomba afanye mapenzi na mimi.
Mkuu aliniambia nikae kwa ajili ya kufanya nae maongezi.
"Angel unajua wewe ni mwanamke mzuri na unavutia sana" mkuu aliongea na mimi ndani ya moyo wangu niliona sasa pamekucha kwani niliamini Mkuu nae anaelekea kunitongoza mda sio mrefu.
Niliamua kumjibu baada ya kunisifia kuwa mimi ni mzuri "hapana mkuu mimi ni mwanamke wa kawaida tu"
"Wewe unaweza kujiona ni mwanamke wa kawaida ila sisi wanaume ndiyo tunaujua ukweli ata mimi huwa natamani kukufanya uwe mchepuko wangu lakini nakuheshimu kwakuwa naipenda kazi yangu na kuheshimu wafanyakazi wangu" Mkuu aliongea lakini bado nilikuwa njia panda.
"Mkuu kwanini umeniambia hivyo"
Niliamua kumuuliza sababu niliona ananiambia mambo yasiyo na maana huku nikiomba asije kuniomba kitumbua changu sababu ingekuwa balaa jingine tena......ITAENDELEA..