ANIPHA 😂😂.
Sehemu ya 12.
Niliingia chumbani kwangu nikachukua funguo za duka na kutoka nje maan Mainda hakuwepo ndani, alikuwa kashaenda kazini kwake na mimi nikatoka hadi nje nikaita boda na kuondoka kwenda dukani
Baada ya kufika dukani nikaanza kufanya usafi huku nasikilza zangu mziki Baada ya usafi nikakaa sasa kusubri wateja, muda kidogo akaingia Allen na Tanasha na mimi nikawa busy kama siwaoni vile, Tanasha akaanza kunisalimia hapo.
"karibuni sana jamani, mmekuja hadi huku"
"Ndio wifi, ngoja tuchague chague nguo kwanza si Ndio babe"
"yeah, anza kichagua mimi nakuja sawa"
Tanasha alienda kichagua nguo na Allen akabaki pale na mimi, na mimi nikachukua simu yangu na kuanza kumfuata Tanasha, Allen aliniita nikasimama.
"Ndio boss kuna shida yoyote"
"anipha embu acha hizo story, mimi nataka tuongee tu japo kidogo"
"tuongee kuhusu nini labda Allen, aah si wewe uliesema kila mtu awe na Maisha yake eeeh au sio wewe"
"Ndio lakini nahitaji kuongea na wewe tafadhali anipha"
"me sina shida na wewe tena sawa, niache kabisa yani kaa mbali na mimi sawa"
"Anipha... Anipha nisikilize basi mama"
Niliondoka na kumuacha Allen amesimama na mimi nikaenda mahali aliko Tanasha, tukaanza kuchagua nguo huku tunapiga story huku tunacheka hapo mimi najikaza tu maan kila nikifikiria kuwa Tanasha ndiye mke mtarajiwa wa Allen naumia sana jamani 🥹🥹🥹.
Tulimaliza kuchagua nguo Allen akalipia kisha wakaondoka, nikabaki peke yangu huku roho inaniuma sana lakini sikuwa na namna Ndio hivyo.
Mida ya jioni nilirudi nyumbani nikiwa nimechoka sana kwani kuna nguo mpya zililetwa dukani hivyo nikawa nazipanga mule dukani, Nilifika nyumbani nikaingia chumbani kwangu kuoga Baada ya hapo nikaenda seblen kula.
"shoga angu ulikuwa wapi jana mmh"
"aah nilikuwa kwa brown Ndio maan sikurudi nyumbani jana usiku"
"Mmmh wewe na Brown mnaanza kunipa wasi wasi kabisa 😂😂"
"umeanza lione kwanza, hamna hata kitu ni vile tu nilikuwa sijiskii vizuri Ndio maan sikurudi nyumbani"
Baada ya chakula cha usiku kila mtu aliingia chumbani kwake kulala, mimi hapo roho inaniuma kweli kweli kujua kuwa Allen wangu mimi analala chumba kimoja na Tanasha 😡😡. Usiku sana nilihisi kama kina mtu kitandani kwangu nikaanza kupapasa kitanda changu nikahisi kama nimeshika kitu kama mwili wa mtu hivi nyie niliogopa sana ikabidi niwashe taa, sikuamini macho yangu kwani aliyekuwa kitandani kwangu ni Allen tena amelala bila hata wasi wasi.
"Huyu anafanya nini hapa jamani kama sio kutafutiana tu matatizo jamani khaaa, we Allen wewe embu amka huku shenzi wewe"
Itaendelea.......
Full 1000
0784468229.