Shirikisho la mpira wa miguu barani ulaya UEFA,limepanga kuiondoa klabu ya Crystal Palace Football Club kwenye orodha ya timu zitakazoshiriki kwenye mashindano ya UEFA Europa League Msimu ujao 2025/26, kwasababu ya muingiliano wa umiliki.
Wamiliki wa klabu ya Crystal Palace FC 🦅 wanaimiliki pia Klabu ya Olympique Lyonnaise kwa asilimia 43%.
Kwa mujibu wa kanuni za UEFA timu ambazo zipo chini ya umiliki wa mtu, kampuni au ushirika mmoja na kama zitatokea zote zimefuzu kucheza shindano husika ambalo lipo chini ya UEFA,ni klabu Moja ndio itaruhusiwa kushiriki mashindano hayo.
Olympique Lyonnaise wamefuzu kucheza mashindano ya UEFA Europa League na Crystal Palace FC pi wamefuzu kucheza mashindano hayo hayo na wote wapo chini ya umiliki wa mtu mmoja, Crystal Palace FC wana asilimia kubwa za kuondolewa kwenye mashindano kuliko Lyonnaise.
FOLLOW US..