Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

ANIPHA ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚. Sehemu ya 13.

7th Jun, 2025 Views

ANIPHA ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚.

Sehemu ya 13.

"we Allen wewe, naomba uamke unafanya nini kitandani kwangu wewe"

"Mmmh jamani nini lakini anipha, mbona wewe ni mgomvi hivyo"

"oooh me Ndio mgomvi si Ndio, aya toka sasa hivi nje ya chumba Changu tena haraka sana"

"sasa Mi nikalale na nani jamani, jana umeniacha nikalala mwenyewe na leo pia unanifukiza kweli jamani"

"nini wewe, unamaanisha jana ulilala chumbani kwangu???"

"Ndio jana nimelala humu, nimekisubiri mpka usingizi ukanipitia bila ya kukuona kweli anipha"

"sitaki kisikia hizo ngojera zako sawa, toka chumbani kwangu mpuuzi wewe yani umelala uko na huyu mwanamke wako alafu unakuja hapa kuniambia sijui nyoko nyoko, toka bwana wee allh"

"Anipha,najua nilikukosea sana lakini nisamehe mama angu eeh, Tanasha sio mpenzi wangu ni rafiki yangu tu nielewe basi jamani"

"๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚Ngoja nicheke kama mazuri, yani mnaitana sijui babe sjui mme Mara mke alafu sasa hivi unaniambia eti ni rafiki yako tu, unaniona mimi mjinga sana si ndio Allen aya toka"

"kweli kabisa anipha, kama huamini twende hata sasa hivi sebleni nikamuite Tanasha kweli tena na hata kuja hapa nilijua kuwa uko hapa na ndio maan nimekuja kwa ajili yako nielewe basi mama eeeh"

"eeeh we kima wewe, embu toka chumbani kwangu hizo story zako kamsimulie Tanasha sawa"

"we nitukane tu vyovyote hata ukitaka kunipiga ni sawa tu ila mimi humu sitoki kabisa yani mpka tuelewane"

"oooh sawa, basi mimi nalala na sitaki usumbufu kabisa na usiniguse kabisa"

Nilirudi kulala, nikajifunika shuka hadi kichwani nikamuacha Allen anaongea mwenyewe mimi nikajifanya kama simsikii kabisa mpaka kunakucha

Asubuhi, kulivyokucha sikumkuta Allen kitandani kwangu nikahisi labda nilikuwa naota mbona Allen hayupo jamani, nikaamka na kwenda bafuni kuoga kisha nikaelekea jikoni kuandaa chai sasa.

"Anipha, njoo tu huku mezani chai ipo tayari mamy"

"afadhali Ndio maan nakupendaga shoga yangu aya ngoja nije"

"Sasa leo shoga yangu hakuna kwenda dukani mpka tumalize mazungumzo kwanza"

"Mmmh kuna nini tena jamani mbona mnanitisha mimi!!!"

"hamna hata kitu tunywe kwanza chai alafu Ndio tutaongea vizuri sasa"

Mimi hapo moyo uko juu juu nikihisi labda ni kwa sababu Allen alilala chumbani kwangu, huenda Mainda alimuona akitoka au Tanasha, jamani me si ndio nitafukuzwa kazi jamani nilimuangalia Allen kwa hasira sana ๐Ÿ˜ก๐Ÿ˜กlakini yeye wala hata hajali chochote, basi Baada ya chai nikatoa vyombo nikapeleka jikoni hapo nawaza sjui hata Mainda anataka kuongea nini ๐Ÿ˜”

Baada ya kuweka vyombo jikoni nikarudi sebleni sasa kumsikiliza Mainda.

"Sasa anipha, mimi nimewaita hapa wote nyie Lengo ni wewe kuyamaliza na mwenzio sioni haja ya ninyi kugombana kwa sababu ya mtu mwingine au wewe Allen unasemaje???"

"Ni kweli kabisa sissy Mainda"

"Jamani ngojeni kwanza, mbona mimi sielewi chochote hapa"

"Anipha, iko hivi Allen amekuja hapa lengo lake ni wewe uweze kumsamehe kwa sababu ameshajua makosa yake na Ndio maan yuko hapa"

"Mimi bado siwaelewi kabisa, Allen ni mume mtarajiwa wa Tanasha alafu mmnasema eti anataka mimi nimsamehe kivipi yani"

" Anipha mimi na Tanasha ni marafiki tu hamna kitu kati yetu, na nimekuja kugundua kuwa huna kosa lolote Baada ya kuambiwa na Briana mdogo wangu"

"oooh kumbe, sasa kwa nini hukunitafuta sasa eeeh"

"nimekutafuta sana Anipha bila ya mafanikio yoyote na hata namba ya simu umebadilisha"

"kwa hiyo hapa umenipataje sasa"

"Ni Baada ya sissy Mainda kuniambia kuwa anaishi na mdada anaitwa Anipha, ndio nikamuuliza yukoje Ndio akaanza kunielezea kuhusu wewe hapo"

"aaah kumbe we Mainda ndio umenichoma kwa huyu mbuzi ๐Ÿ˜ก๐Ÿ˜ก"

"ukweli mimi ndio nilimwambia na Baada ya wewe kunisimulia kuhusu kuachana kwenu, nikajua kuwa ni Allen mdogo wangu maana hizo Ndio tabia za mama yetu"

"Ndio Anipha, wanayoongea Mainda na Allen ni kweli kabisa, mimi na Allen ni marafiki wa muda mrefu sana na nimekuja nae ili kuhakikisha kuwa mnarudiana basi"

"Ndio, Anipha hata mimi mama alimkataa mpenzi wangu kwa sababu ni maskini na Ndio sababu ya mimi kuondoka nyumbani na kuhamia huku Arusha, msikilize basi mwenzio"

"sissy Mainda Sisi tuondoke hapa tuwaache wenyewe waonge si eti"

Mainda na Tanasha waliondoka sebleni na kuniacha mimi na allen sebleni ili toungee sasa muda huo mimi nimenuna hatari nataka kubembelezwa ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚.

Itaendelea.......

Full 1000
Whatsp 0784468229.
   

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MSHANGAZI EPISODE 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 13

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 10

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

YAMENIKUTA

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 9

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINSI YA KUTUNZA UKE

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

PART 5 MY HEART

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MY HEART 03--04

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

*MY HEART* *1---2 *

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 7

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

ANIPHA 6--7.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 05

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

side chick episode 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

SIDE CHICK EPisode 2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 18

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 17

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 16

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 8

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA Sehemu ya 32

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

BOYCHILD PART 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 4.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 3

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest