Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  gonga94 official track

SAMIRA ๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹ ๐Ÿงš๐Ÿปโ€โ™‚๏ธ 06&7 (Nimeshindwa kusamehe)

19th Jul, 2025 Views 32



BY DIANA STORIES

WTSP 0768328909

Kijana yule alinisaidia kuvuta begi langu mpaka sebuleni kwao kiukweli sebule ilikua pambe sana jamani ilipendeza ilionekana kuwa ni familia yenye pesa sana sana.

"Karibu binti karibu sana samira...."

"Asante "
Nilijibu kwa sauti ya chini kabisa na kusimama pembeni

"Salome......"

Aliita kwa sauti yule mama na muda huo huo akaja binti ambaye kwa muonekano tu alionekana kuwa ni mkubwa sana kwangu

"Chukua ili begi na ukaweke chumbani kwako "

"Kwanini chumbani kwa Salome, samira angepewa chumba chake tu "

Alidakia kujana yule ambaye alikuwa akiitwa samiry na yeye ndo alinifuata kule kituoni yaani mpenzi msomaji naogopa sana kuwa peke yangu na ukiangalia ni ugenini nikaamua kudakia tu

"Ni sawa kama nitakuwa pamoja na dada hapa naogopa kulala peke yangu "

Basi mama yule alikubali na mabegi yangu yakapelekwa chumbani kwa Salome ambaye kwa muda huo nilishamuweka kuwa ni dada kutokana na kunipita umri

"Samira kaa tu hapa upumzike mwanangu "

Basi nikaka kwenye kochi nikishangaa uku na uku yaani nilikuwa nashangaa jamani ๐Ÿ˜‚๐Ÿ™Œ kiukweli ushamba ni mzigo.

Majila ya usiku tulikaa kwenye meza ya chakula na kuanza kupata chakula baada ya muda tulimaliza lakini baba qa familia aliomba kuzungumza na sisi

"Aaah Samira niseme tu karibu sana, lakini pia Asante sana kwa kukubali kuja kuishi na sisi"

"Asante "

Nilijibu tu kwa ufupi maana sikuwa na neno la kuongezea

"Aaah Salome, huyu ni samira mtakuwa mkisaidiana kazi za hapa nyumbani yaani ni mfanya kazi mwenzio mimi ningependa muwe na umoja, mpendane na kusaidiana katika kila kitu "

"Usijali baba na mama ila niseme tu asanteni nimepata mtu wa kupiga nae story kwakweli sasa hivi nitachangamka "

Hapo nilifurahi na kuona sasa hapa nimepata dada maana alionekana kuwa mcheshi Sana

Siku iliyofuta nilianza kazi zangu rasmi uku nikipokea maelekezo kutoka kwa dada Salome

"Mpelekee hii juice samiry kule chumbani kwake "

"Kwani ye awezi kuja kuchukua uku chini ??"

"Weeeh unataka mama aje uku atunyooshe au ? Eeeh yaani huyu mama ako na mtoto mmoja tu na hii ratiba ya kupelekewa juice kila asubuhi niliokuta hivyo nafanya kuendeleza tu "

"Makubwa wacha nitimilize wajibu wangu "

Basi sikuwa na budi nikachukia juice na kuipeleka chumbani kwake, niligonga mlango na aliruhusu niiingia, nilifika na kuiweka mezani

"Kwani hujui kusalimia ??"

Aliniuliza maana nilifika tu na kuiweka mezani na kutaka kuondoka

"Ooooh samahani nimepitiwa, umeamkaje kijana "

"Niite samiry au kaka "

Alijibu hivyo

"Sawa...."

Sikutaka kuongeza neno lolote nikatoka nje.

Majukumu yaliendelea na siku ziliendelea kusonga na kujikuta nikiwa nimepazoea sana yaani nilijikuta kumzoea dada Salome mno lakini pia familia nzima isokuwa samiry ambaye mimi tu nilitokea kumchukia bila sababu ya msingi.

"Samira..."

"Beeeh "

"Tupike chap ili marafiki zake wakija wakute tumemaliza kila kitu "

"Sawa"

Yaani siku hiyo marafiki wa samiry walikuwa wanakuja kumtembelea pale nyumbani na tulipewa maagizo na mama mwenye nyumba kuwa tuwaandalie chochote kile kizuri na tuwapatie watakachokiitaji

Majila ya saa 8 mchana marafiki zake walifika walikuwa kama 7 hivi yaani wakaka watanashati lakini pia walikuwa wacheshi mno tuliwatengea chakula mezani kisha mimi na Salome tukarudi chumbani baada ya muda mlango wetu wa chumbani tulisikia ukigongwa, kwakuwa mimi ndo mdogo nikainuka na kwenda kufungua mlango uso kwa uso na samiry

"Oooh kaka samiry "

Nilizungumza hivyo gafla tu ata sijui hiyo nguvu ilitokea wapi

"Waoooh ili tabasamu ningekuwa napata kila siku sijui ningenenepa kiasi gani "

Alidakia kaka samiry

"Nakusikiliza kaka "

"Oooh nilikuwa naomba utuongezee chakula lakini pia na juice "

Tukaongozana nikaingia jikoni na kuwawekea chakula, na kuwapelekea mezani kwao, niliweka na kutaka kuondoka

"Samiry mbona ututambulishi dada yetu jamani, eeeh Salome tunamjua huyu je ??"

"Mnazingua bhana haya bhana, huyu anaitwa samira ni m......."

Kabla ajamaliza kuzungumza mmoja Kati ya rafiki yake akadakia

"Ndo huyu aliye......."

Samiry chap akamziba mdomo rafiki yake na kusema

"Samira unaweza kwenda"

Nilitoka eneo ilo lakini nilisimama kwa kujificha nikitaka kujua kwanini alimziba mdomo mwenzie

"Ulitaka kulipoka nini nawe "

"Daaah kwani bado ujafanya mambo au ??"

"Bado namuogopa hatari lakini pia ni mkali mno muone hivyo hivyo "

"Mnatuweka njia panda mnaongea vitu ambavyo hamjatushirikisha kabisa "

"Jaah wanangu mshikaji ambaye hajawai kuwa na semu tangu aachane na yule chuma ulete wake kaangukia kwa mtoto samira "

Alizungumza rafiki yake yule ambaye moja kwa moja walionekana kuwa ni watu wa karibu sana sana

"Chekeni tu lakini ndo mmjue samira ameteka akili yangu na kila kitu kwangu...."

Alidakia samiry baada ya kuona wenzie wanacheka sana, na mimi katika kushtuka si ndo nikatoa sauti ๐Ÿ˜‚๐Ÿ™Œ.

ITAENDELEA ๐Ÿ‘Œ

SAMIRA ๐Ÿ’‹ ๐Ÿงš๐Ÿปโ€โ™‚๏ธ 07
(Nimeshindwa kusamehe)

Baada ya kusikia na kuona kuwa wamestuka kuwa kuna watu wanawaangalia nilitoka mbio moja mpaka chumbani na kufunga mlango

"Nini nawe mbona tunashtukana "

Alilalama dada Salome baaya ya mimi kuingia chumbani kwa fujo

"Aaah yaani nimeamua kujikimbiza jamani pole kama nimekushtua "

"Mmmmh we nawe, subili niende nje mie "

Alizungumza Salome

"Kufanya nini nawe tukae umu ndani "

Yaani muda huo nilikuwa naona aibu Sana na nilikuwa nikijiuliza maswali wale wakakapale nitawaangaliaje mie jamani lakini pia sikuwa na namna nilipita pale sebuleni kama kishada yaani shaaaah ๐Ÿ˜‚ lakini da Salome hakuwa ata na haraka kama ambazo nilikuwa nazo mimi.

Da Salome akachukua na mpira akatoka nao nje tukaanza kucheza kwa kurushiana wakati huo niliwakumbuka sana wadogo zangu niliowaacha kwenye kituo cha watoto yatima yaani michezo hiyo nilikuwa nikicheza na watoto hao kwa miaka kadhaa tangu nilipopata ufadhili kwa mjomba rafiki.

Tulicheza mpira pale na baada ya muda walikuja wakaka wote pamoja na samiry tukaanza kucheza nao kwa siku hiyo nilifurahi sana sana tangu nimeingia kwenye nyumba hiyo lakini pia nilikuwa naongea na kucheza na samiry bila kisilani changu cha siku zote.

Majila ya jioni kama kawaida tukarudi kwenye jukumu letu la kuandaa chakula na siku hiyo rafiki zake walilala pale nyumbani yaani kulichangamka sana jamani๐Ÿ˜Š nyie mkiwa wengi halafu ucheshi wa kutosha.

Muda wa kulala kila mtu aliingia chumbani lakini wakina samiry waliendelea kucheza tu game ๐ŸŽฎ.

Nikiwa nimelala ujumbe mfupi uliingia kwenye simu yangu ulisomeka hivi

"Umelala kipenzi au ? Kumbe wewe ni mcheshi kiasi iko ? Tabasamu lako sasa mama daah "

Ujumbe huo ulitoka kwa samiry niliuangalia na kujikuta nikitabasamu tu walahi haya mambo ni konyo, lakini pia nilikuwa sina jibu hivyo niliweka simu pembeni na kutafuta usingizi lakini pia ilikuwa sio rahisi kupata usingizi nikijikuta nikiifudia ile sms kila mara mpaka pale nilikopitiwa na usingizi.

Ilipita week moja nikiwa sijatoa jibu lolote kwa samiry lakini pia tulikuwa watu wa karibu sana kupita kawaida alinifundisha hadi kucheza PS nyie ๐Ÿ˜‚๐Ÿ™Œ mtoto wa watu mie yatima mimi lisije likanikuta jambo bure maana haya ninayoyaona mmmh.

"Samiry anakuita chumbani kwake "

Alizungumza dada Salome wakati huo tulikuwa tumekaa chumbani tukipiga story za hapa na pale

"Anataka nini naye yaani msumbufu huyo "

"Ujamzoea tu nawe, yaani anaweza akakuita ukaensa halafu akakutuma maji ya kunywa "

"Nitamnyoosha ananijua nananisikia atafuata mwenyewe "

Basi niliinuka na kuelekea chumbani kwa samiry

"Sms zangu uzioni au ??"

"Unachosha nawe aaah "

"Mimi ndo nakuchosha au, samira nikuulize kitu ??"

"Niulize "

"Ila ni kuhusiana na maisha yako "

"Hakuna shida "

"Imekuwaje mpaka wewe umelelewa na kituo cha watoto yatima ??"

"Na kweli umezamilia kujua unakumbuka ili swali umewai kuniuliza nikiwa kule kwenyw kituo ??"

"Yaah natamani sana kujua "

"Sawa, mimi nimebahatika kulelewa na baba tu........."

Nilitumia muda mrefu sana kumsimulia samiry maisha yangu mpaka hapa nilipofikia kiukweli ninapoongelea maisha yangu uwa nashindwa kujizuia najikuta tu nikilia Sana

"Ila uwa namshukuru sana Mungu mpaka hapa nilikofikia "

Nilimaliza kwa kusema maneno hayo na muda huo huo alinisogelea na kunikumbatia jamani niliachia kilio iko daaah

"Usilie jamani "

Alizungumza samiry, niliinuka na kuondoka moja kwa moja mpaka chumbani kwetu.....
KARIBU IPO FULL NJOO WHATSAPP NAMBA 0768328909 JINA NO ZA MALIPO I

0768328909 JINA DIANA JOHN NI VODA KARIBU.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

SAMIRA ๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹๐Ÿ’‹ ๐Ÿงš๐Ÿปโ€โ™‚๏ธ 06&7 (Nimeshindwa kusamehe)  >>> https://gonga94.com/semajambo/samira-06-7-nimeshindwa-kusamehe
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
karibu msagala furniture
karibu msagala furniture

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MKEKA 03

majario rewards 100 Comments 0
 

.BABAMKWE epsd 19.

majario rewards 100 Comments 0
 

ALINIINGIA BILA IDHINI

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE..17..18

msagala rewards 100 Comments 0
 

bei sawa na bule

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 16

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 14...15

majario rewards 100 Comments 0
 

MDOLI MPENDA UTAMU...1

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest