Neema alipanga siku mpya. Akiwa amevaa kanga yenye maua ya manjano, alitembea hadi jikoni kukagua hali. Hapo alimkuta Baraka akijifanya kuosha sahani huku Aziza akisimama pembeni akipiga miayo kama mtu aliyeamka sasa hivi.
Neema (kwa sauti tulivu yenye sumu ya shaka): “Aziza, unasema umeamka sasa? Basi niambie– nani kade–ki leo?”
Aziza alihema, macho yakikwepa. Kabla hajavujisha siri, Baraka alijibu haraka:
Baraka: “Leo nilitaka nishughulikie mwenyewe mke wangu. Niliona uchovu wako jana, nikaona nionyeshe mfano.”
Neema alimtazama mumewe kutoka kichwani hadi miguuni, akatikisa kichwa taratibu.
Neema: “Sijawahi kukuona ukiosha kikombe hata cha mgeni, leo unaosha vyombo vyote? Sawasawa. Mungu anashuka weeh!”
Kisha akasimama mbele ya Aziza.
Neema: “Leo usiende sokoni. Tukimaliza chakula utanisaidia kupangua stoo. Hapo ndipo pana vumbi kuliko sebule.”
Aziza alimeza mate, akajibu kwa tabasamu la bandia: “Sawa dada.”
Neema akaelekea bafuni. maana musa uikuwa ushaenda ilibidi ajiandae aelekee kazini na alihisi kuchelewa tayari
Dakika ishirini baadaye, Neema alitoka bafuni akiwa na gauni la bluu na harufu ya ‘Spanish Rose.’ Alimkuta Baraka amesimama sebuleni.
Neema (akitabasamu kidogo): “Nielekeze barua za wateja uziweke mezani, nikitoka kazi niangalie.”
Baraka alisogea, akamshika kiuno:
Baraka: “Ubarikiwe mke wangu. Usiwe na mawazo.”
Walikumbatiana. Mwishowe mwanmke aliingia ndani na kujiandaa tayari kwa kutoka
Busu la kwaheri likawa laini, ila jicho la Neema likatafuta ukweli nyuma ya paji la Baraka. Hakuliona. Akatoka; mlango ukafungwa.
Barak naye alipiga mswaki na kunawa uso kisha akaenda zake kazini lakini muda anatoka aliitwa na Aziza .
Aziza alimkimbilia na kumkumbatia kwa nyuma yaani mambo ni moto" naomba leo saa tano urudi nataka nikupe tamu yako baba tafadhari...
" okay usijali mke kwa ajili yako nitarudi"
Akamgeuza na kumpiga mabusu mengi mengi kiasi kwamba ni ngumu kuyahesabu na katoto tayari kamezama penzini mwa mume wa bossi wake ila mapenzi shikamoo na ndoa ni pacha wake marhaba ...
Saa tano na nusu za mchana, jua likiwa linawaka juu ya dari la nyumba, Baraka alisimamisha pikipiki yake mbele ya lango. Alijishika roho kama mwizi mwenye furaha. Alipofungua mlango, Aziza alikuwa amekaa sebuleni akiangalia tamthilia ya Kikorea; mikono yake imekamatia mto, macho yakiota ndoto za mbali.
Baraka hakusema neno. Alienda moja kwa moja, akamvuta kwa mikono miwili, akamuinua taratibu.
Baraka (akishusha pumzi): “Tangu asubuhi nimehesabu dakika kurudi. Moyo umekuwa mwiba.”
Aziza aliinamisha kichwa kifuani kwake. Mikono ya Baraka ikapanda kiunoni, akamkumbatia. Aziza akainua uso, wakatizamana. Hakukuwa na neno, walisemezana kwa pumzi.
Baraka akampa busu lenye ukimya mrefu; busu linaelea, linashuka hadi kwenye mashavu. Aziza akamgusa bega, akamvuta karibu zaidi.
Walisogea taratibu hadi nyuma ya kochi. Nguo hazikuvaa aibu; zikasugua, zikalalamika chini ya miguso. Muda ulisimama.
Lakini barua ya Aziza aliyompa Baraka asubuhi ilikuwa mfukoni mwa shati lake ikaribiana na moyo wake, ikimkumbusha aibu na deni. Alijitoa taratibu kwenye kumbatio.
Baraka: “Aziza, tunacheza na moto. Lakini moyo wangu tayari umeungua.”
Aziza akasema kwa sauti ya unyoofu:
Aziza: “Usiniache katikati ya barabara. Ama ufungue mlango niingie, au nifunge daftari niende.”
Baraka hakuwa na jibu. Alimshika mikono, wakakaa kochini kwa muda, kimya.
Wakati huo huo, Neema akiwa ofisini alijikuta akisoma hati lakini macho yake hayakuona herufi. Kichwani kulilia kengele: “Baraka ameabadilika sana … Aziza naye simuelewi?.”
Akamuita rafiki yake, Aisha, akamweleza wasiwasi. Aisha akatoa hukumu ya haraka: “Huyo dada wa kazi anaonja asali yako.”
Kabla hawajamaliza mazungumzo, simu ya Neema ikaita. Ilikuwa namba isiyoandikwa – mtandao wa kificho: Onesmo, mmbea wa mtaa.
Onesmo (kupitia simu): “Mama mwenye nyumba, habari za mchana? Habari hiyo ina moto, tafadhali beba kilo moja ya nyama njoo Mtaa wa Tatu, nyuma ya duka la Mzee Kipara. Siri ya mumeo iko hapa.”
Neema alishtuka. “Na nyama ya nini?”
Onesmo: “Siri bila nyama ni kama chai bila sukari. Ukichelewa, napakia mdomo kwenye redio za mtaa!”
Neema alikata simu, akajifunga kanga juu ya gauni, akachukua pochi. Akaenda butchery, akanunua kilo moja ya nyama ya mbavu, kisha akapanda bodaboda hadi nyuma ya duka la Mzee Kipara.
Chini ya mti wa mkungu, Onesmo alikuwa amevalia suti ile ile ya kaki iliyokopa hadhi. Alipomuona Neema akishuka, uso wake ulijaa tabasamu lenye meno yasiyo na aibu.
Neema alimkabidhi mfuko wa nylon .ulionukia nyama rost na kapilipili kwa mbali sana
Neema (kwa ukali wa sauti nyororo): “Sasa sema, nimegharimika.”
Onesmo akasafisha koo.
Onesmo: “Siri yenyewe ni hii. Mumeo anatema mate kwenye sahani mbili. Yaani namaanisha wewe na Aziza wote ni sahani za mumewe kifupi asali yako na aziza zinalambwa na mumeo .pole sana
Neema alihisi tumbo lake limejaa mawe.
Neema: “Ulikuwa unataja pesa kila mwezi ili ubaki kaburi. Leo unaongea.”
Onesmo: “Aliniahidi pesa. Hajalipa. Sasa siri itanuka kama nguo ambayo haijafuliwa. Utaamua kufanya nini.”
Neema akavuta pumzi, macho yakabadilika rangi. Bila kusema zaidi, akageuka, akamwacha Onesmo akikwaruza meno yake kwenye mfupa wa mbavu aliyotafuna kabla.
Neema aliamua kuchukua boda na kurudi nyumbani maana anahisi lazima watakuwa wapo wote ...
Njia nzima, Neema moyo wake ulijipa maswali:
“Je, ni kweli? Au Onesmo anauza chumvi ya maneno au anachosema ni kweli ?
Kipindi hicho nyumbani watu wapo faragha nguo zinatupwa nguo zinaangushwa bila huruma watu tayari kwa zoezi
Siku za mwizi ni Arobaini na leo naona kama ndio ya 40 unadhani itakuwaje usikose
.