SEHEMU YA 04
Favour de Mr Burudan
Basi bwana mpka unafika muda wa kulala hakuna cha sms wala Simu ya namba ngeni😥nikawa nawaza au kaipoteza namba yangu si bora ningemwambia hata anidipu sasa daah kimyaa na usingizi ulinipitia,,mpaka nikamuota huyo kaka et ananitongoza hee nilipo shtuka tayari asubuhi ,cha kwanza nilishika simu kuangalia kama kuna namba mpya lakini doroo😥 duh ngoma ngumu nilitaka kushangaa angenitafuta ningesema mkosi wangu umetoka lakini haya bwana nikamshukuru mungu tu maana hata kule kunishobokea tu kwangu inatosha sio rahisi mkaka kama yule kuna shaukia mimi mdada wa mabondeni hukooo 😥
Hiyo siku mi ilikuwa naondoka zangu kurudi om kwangu yaan natoka pale kizuiani naenda kwangu sasa nikaendelee na Life yangu , nikachukua zangu boda mpaka Om , nilimkuta shoga angu yule alinikwaa kwa bwana angu huwa tunafanya nae biashara zetu za kuhangaika lakini tunakaa pia nyumba moja akanambia "bora nimekuona shoga anguu" akainuka alikuwa amekaa anatengeneza utumbo wa kuku maana huwa tunauza hivyo vitu vya kurumbua rumbua utumbo ,miguuu ya kuku vichwa NK ndo biashara zetu watoto wa uswahilini na yeye hata baada ya kujua anacheat na bwana angu mi hata sikutaka kumnunia hayo maisha ya kizamani sana kwangu ni ujinga ...
Alivyoniona alikuja mbio ,tayari nilikuwa nishafika mlangoni kwangu nafungua
"Pole kwanza na kuuguza "
"Asante kuna usalama mbona unafuraha hivyo ??"
"Aah furaha wapii shoga anguu , nilikuwa nataka tu nikualike harusi mwenzangu "
"Enhee nani anaolewa"
"Mimi tena shoga angu kitakuwa kishuhuri hapa hapa kesho jioni yaani kama umekuja muda muafaka "
"Hongera mwaya baba harusi ndio nani??"
"Mikaa huyo huyo " yaani baada ya kumtaja mika moyo wangu ulipiga paaa!! Nilihisii donge kubwa la uchungu chozi lilitaka kunitoka lakin niliomba mungu anilinde nisije kuonesha udhaifu mbele ya adui yanguu nikajichekesha chekesha nikampa hongera kama zote , ndo nikaingia ndani ,nafika tu ndani machozi yananitoka jamani moyo uliniuma sana niliamini kweli mimi nina mkosi jamni
Mika alikuwa ni mwanaume wangu hakuwahi hata siku moja kutamani kunioa yaani mimi sijawahi kuahidiwa ndoa kabisaa na mtu yeyote hicho ndio kiliniuma kweli inamaana wanaume wote hakuna hata muongo wa kuniongopea ndoa??
Huyu shost wamekaa na mika hata miezi miwili bado lakini wanafunga ndoa aisee niliumia sana sana nikatamani hata niwafanyie fujo siku ya ndoa yao lakini nilimkabidhi mungu anishikilie maana yeye ndie kaniumba😥😥
Nilijilalia zangu stress kama zotee machozi kila nikiyazuia wapii sa mi namkosi gani jamani aaah 😥
Nililala usingizi wa haja nimekuja kushtuka ilikuwa tayari giza limeingia nikajikokota zangu kwenda barabarani kuchukua chakula, nilipo rudi om ndo nikakumbuka simu yangu sijaishika mda kweli hata mama kachanga sikumwambia kama nimefika salama ndo nikaichukua ilikuwa na msg za mama mtoto ananiuliza kama nimefika salama nikauta na msdcll za namba ngeni zilikuwa msd mbili nikaipiga ile namba kumbe salio langu limeisha nikaandika msg nayo ikafeli aah nikaitupia zangu huko simu nikala zangu nikaenda kuoga nimetoka kuoga nikakuta tena msd call 3 namba ile ile asa nikawa najiuliza huyu sijui nani tunapishana kweli nikawaza nitamtafuta kesho mi naona uvivu kwenda dukani mida hii kuchukua vocha tu kwahiyo nikajilalia zangu mpaka asubuhi nikaamkia kuchukua biashara hapo nawaza niende kwenye hicho kiharusi chao au nikaushe ??
Nilichukua biashara mpaka eneo ambalo ninafanyia kazi nikatengeneza nikaandaa vizuri baada ya hapo ndo nikakaa kusubiri wateja mi huwa nauza kuanzia sa 7 mchana nikimaliza nakuwa zangu tu free, wakati nipo hapo nachezea chezea simu aah ndo nikapata wazo la kuitafuta ile namba nikapiga haikupokelewa nikarudia tena mpaka ikakataka mara 3 nikaachana nayo , hiyo siku niliwahi sana kumaliza maana nilichukua kidogo kwa muhofu nina muda mrefu sijafungua naeza kudoda bure ,asa nilipo maliza nikapanga hapa nisiende nyumbani yaan pamoja kukubali mimi kumuacha mika sio siri swala la wao kufunga ndoa linaniumiza sanaaaa aisee sanaaa siwezi hata kulivumilia nikawaza niende kwa shoga angu mmoja hivi mpaka usiku ndo nirudi zangu kulala mana nilimaliza mapema sana ,
Huyo mpaka kwa shoga angu ni mitaa miwili tu unafika akawa ananitania kuhusu mika et anaona basi nikamjibu kwanza mimi sina hata shida nae ningekuwa nampenda si ningemgombania kipindi najua mahusiano yao ???
Mida ya sa moja hivi simu yangu iliita na mpgaji alikuwa shost kuolewa nikaipokea "shoga angu mbona kimya mpaka sasaa" nikashangaa huyu nae mbona kama mimi ndo mfungishaji ndoa tenaa ?? Nikajiuliza moyoni afu nikaanza kucheka cheka
"Shoga angu bado nipo kibruani ndo mana umeona kimya ila nikimaliza tu nakuja my dear " nilimjibu huku nmechangamka kweli
"Haaa!!udugu wangu vibaya hivyooo,au mume ulikuwa bado unamtakaa" mmh 🤔kwanza nikaguna " haya tena yanatokea wapi shost??"
"Aah nakuona ona tu tangu nikupe taarifa mwenzangu kuhusu harusi naona umebadilika kweli " nikaona huyu anataka kunivuruga mie sasa mfyuu
Nikamwambia " sikia emmy huyo mwanaume mimi ndio nilimuacha kwahiyo simuhitaji sijaja kwa sababu bado nina shughuri zangu sawa..." nilikata na simu bila hata kusubiri jibu lake ndipo alianza kunitumia msg aisee🙄yaa nilibaki nimetoa machooo wee hizo msg anadai et mimi namloga sana na alinialika maksudi nikafanye uchawi wangu baada ya kuona ngoma ngumu et nmekimbia nyumba anajua nimemaliza biashara muda tu nimeikimbia hadi nyumba naogopa kuaibika 😡Huyu mshezi alinitia hasira nikasema wacha niende huko huko yaani mtu bibi harusi afu anachambana duh nikamuaga shoga angu ye ananiambia usiende embu mpuuzie nikasema hata siendi kuongea kitu naingia chumbani kwangu kimyaa ila nikisema nisiende hata mashoga zake wataamini kweli mi nimekimbia kwa sababu amepawangia.
Nikakusanya makolo kolo yangu nikachukua boda yaan hasira nilizo kuwa nazo hata kutembea nilikuwa nashidwa niliona tu nicheck boda ila nyumbani hapana umbali wowote ....
ITAENDELEA...
Sehemu ya tano
Nikachukua zangu boda mpaka om, nilikuta ndo pamenoga hatari shamra za hapa na pale mashost wa mtaani kama wotee, nikashuka zangu kwenye boda nikalipia hapo natetemeka miguu , nikawapita ajabu wamekaa mpaka mlangoni kwangu wakati nakaribia mlangoni nikamuona bibi harusi katoka haraka kasimama mlangoni kwake ananitazama mi hata sikumjali nikafungua nikaingia ile namalizia tu mguu nilisikia cheko hiloo mpaka wamegonganisha mikono mh mi nikatabasam tu lakini nilijiskia aibu sana😥 kama sec kumi tu nikasikia honi na kelele waowaji wamefika mi nasikilizia tu ndani duh moyoni nasema ama kweli emmy anabahati dada mi nazeeka sina ndoa wala mtoto duh 😥😥inakera sanaaaa
Naskia tu vigere geree hatarii nalazimisha usingizi nao hata hauji nikawa natazama tu dali, simu ilinishtua ikawa inaita nilipotazama ilikuwa ile namba inaishia 666 imekuwa ikinipigia tangu jama nikaipokea
"Hallo" ilikuwa sauti ya kiume
"Nani" nikauliza mapema
"Mmmh mamkubwa ndio hata salamu hakunaa!!!" Haa yaan alivyosema mamkubwa furaha iliyolipuka moyoni mwanguuu anajua munguuu jamani 🥰🥰🥰nilisema asante munguu nikanyoosha mikono juu haaa😀😀nilianza kucheka cheka
"Abbass..." niliita ili nipate uhakika ndie yeye ??
"Naam!! Umeniita vizuri haya nambie mana jana nimepiga hata hupokei nikasema isije kuwa upo na shem mi nakazana tu kupiga" uuuphsss kwanza niliikombatia simu kwa sec afu nikaitoa haraka kurudisha sikioni
"Hata hamna nilipitiwa usingizi nikakuta msg call nimejaribu kupiga kumbe sina salio nikaenda kuoga narudi nikakuta tena msd call leo mchana nimepiga hata hujapokea nawewe" nilitoa maelezo sio poa kuhakikisha yamenyooka
"Ooh niliona sema nilikuwa na kazi so nikasema nikitulia nitamucheck mamkubwa" nikacheka tu maana anavyoliita hilo mamkubwa na lafudhi yake haijui vizuri kiswahili basi ndo anaongezeka tu mvuto
"Waitwa nani mamkubwaa!!"
"Mi naitwa Nasraa"
"MASHAALLAH " hiyo mashallah ilivyotajwa nyiee🙌🙌 mpaka Rahaaaa
"Ni muslim???"
Nikasema ndio akasema tena mashallah
" Umehifadhi Juzuu ngap " mmmmh jamani mambo tena ya kuhifadhi juzuu mimi huyuu nikajisikia aibuu 🤦♂️🤦♂️Jamani nyie hii sikieni tu yaan mtoto wa kiislamu uulizwe hili swali alafu uwe holaa yaan wewe ni alifu tena alifu yenyewe ya juu juu daah aibu mnooo nikajikakamua
"Mh mi hata sikujaaliwa kupitia madrasa lakini natamani sana kama walau ningepitaga huko "
"Ooh pole ila bado hujachelewa muhimu unapumua nafasi ya wewe kusoma ipo "
'"Mmh abbass unajua maisha yanavyotuendesha sie watoto wa mtaani mpaka ukimbizane ndio ule , muda umepita labda upate hicho kijinafasi ukimbie hiyo ijumaa "
"Noo!! Nasra Noo!! Mfanye mungu wako kuwa wa kwanza kuliko hayo maisha mungu ndo anapanga maisha yako kwanini usimpe muda mwingi wa kumshukuru walau kwa pumzi na afya unayotamba nayo ?? Nasrs hujachelewa usiseme ukipata muda utakwenda kuswali tena ijumaa No!! Mshukuru mungu kwa kila sec ya pumzi yako inapo toka !! Muombe mungu kwa kila Dakika unayopumua hutakiwi kumfanya mungu yeye ni wa ziada au dharula noo !! Kusoma Quran sio kuingia peponi wala sio kipimo cha mja mwema jitahidi sana kumjua mungu wako kwa mapana zaidi okay ,kama una nafasi hata ya sec moja unatumia kuchezea simu hiyo sec itumie kuongea na mungu"
Duhh nilikaa kimyaaa kuacha dawa iniingie ukweli mimi nilimfanya mungu kuwa wa ziada yaan nikipata nafasi nitaenda ijumaa au nisiendee inategemea na mood yangu niliona aibu maana aliyosema yalinikumbusha uchungu yaan ni kama alinigusa kati kati kwenye kitovu cha moyo nilijikuta kimoyo moyo ninamuomba mungu msamaha na kujiahidi sasa hivii kila ijumaa ni lazima kwenda msikitini sio hiari ,tuliongea mengii yakunichekesha basii ndo nacheka kama sina akili , Ya kuniasa kuhusu maisha tuliongea jamani sijawahi kuongea na simu hivyoo ,
Mwisho nikasikia kimya nikabaki haloo haloo haloo!!! Ikabidi nitoe simu kutazama haa kumbe imezima 😀😀kwahiyo imeishaa 🙌 nikaichomeka haraka haraka bibie nina haraka kama nimetongozwa ilivyowaka nachek saa, sa 7 kasoro ,wee 😳 yaan nimeongea na simu kutoka sa moja ile sijui sa mbili mpaka sa saba usiku Serious????
Wakati bado nashangaa ikaingia sms
(Ulale salama mamkubwa , pole na uchovu wa siku nzima) uwiii nilikabusu hako ka sms alijuaje kama siku ya leo imenichosha kiasi kikubwa 😄 niliikumbatia ile simu nikawaza nimjibu nini ?? Basi kila nikiandika sms nafuta nafuta nikasema ngoja nikakojoe afu ndo nije kuijibu wakati nafungua mlango ndo nikakumbuka kulikuwa na harusi jamani😀😀 palikuwa kimyaa hata sijui walimaliza sangp ilikuwaje yaan hata sielewi nikaenda zangu chooni nikarudi sasa nikabaki nimeshika simu nimjibu nini huyu kaka mana mmmh
Wacha usingizi unipitie 😆 yaan nimekuja kushtuka asubuhi simu ipo pale pembeni sms juu haa nikawaza sema atasema nimemdharau jaman daah nikachukua simu haraka haraka nikaanza kuandika jamani usin...... hata sijamaliza sms ikaingia pale pale inatoka kwake
(helllow Queen Goodmorning )
Haaa🥰🥰🥰nakaribia kuzimia haya si ndio mapenzi ya kizungu jamani mi hata sijawahi kutumiwa ka sms ka maneno ya kingeleza hawa wanaume zangu wenyewe tulifeli wote darasa la nne sangp ataandika Goodmorning nikamjibu kiswahili mi sipendi kujifanya matawi wakati sina kitu mie
(Alhamdulillah nimeamka poa ,Hofu kwako)
(Mashaallah, mi pia nipo poa nilikuwa nakupa tu hi )
(Asante simu yangu jana ilizima chaji )
(Yeah nilipiga ikawa haipatikani )
Basi nikajichekea kumbe alipiga mmh haya bwana mi ndo nishapata mpenzi hivyo atajua yeye hata asipo nitongoza akanambia ndo naelekea kibaruani nilitoka nitakucheck bibie 🥰🥰nikaandika sawa kazi njema akanambia kwako pia , yaan hapo ni kama nimepewa mtaji mana sio kwa afya ile nilitoka nayo ndani tabasam kama lote natoka nakutana na mdada hivi chumba cha jirani akanisalimia vizuri akanambia jana walikuwa wananigongea wanipe sadaka ya chakula , nikawaza hawa watu wanaakili sawa sawa hawa hee afadhali Abbas alipiga simu muda muafaka aisee jana ningejuta kuzaliwa mie basi muda huo ukafunguliwa mlango wa shost bibi harusi sasa kha!! Nikashangaa kwani si inatakiwa bibi harusi anatakiwa aende kwa mwanaume au alienda kuna mtu kalala humo bado sijamaliza maswali yangu namuona mika anatoka kifua wazi chini kajifunga khaga daah kidogo nicheke kwa sauti ila nikajizuia akaenda uwani nami nikamsubir atoke niingia alivyotoka akanisalimia et za asubuhi nikamjibu poa
Nageuka nakutana jicho na mkewe akanisonya khaa !!! Yaan kaamua kuoa yeye sasa heheh😆😆 nilichekea moyoni haya nihusu wee nikaenda kuoga nikajiandaa mishe mishe zangu kutafuta pesa kwanza ....
ITAENDELEA.......
Soma mpaka mwishoo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0781858056.