Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

DOCTOR NITIBU NA HUKU KUNAWASHA🌹🌹❤️❤️❤️🌹 ❤👌👌06... 7

1st Jul, 2025 Views 29



Nilikuwa zangu kwenye biashara akaja shoga angu yule jana nilienda kwakee
"Weee yaan jana sijalala kila nikipiga simu yako inatumika utafikiri ulikuwa unaongea na kijiji" kabla hata hajakaa alianza kunipashaa
"Heheh mwenzangu ilinibidi jana niongee na kijiji we kuwezaa"
"Basss ,,waenda harusini jana walipo rudi mwenzangu namuuliza mele huko kwemaaa nikajua umepigana labda na bi harusii akanambia bora hata wangepiganaaa kuliko hilii bibi harusi kaowa😆😆mana watu wanajiandaa kusindikiza harusi kumbe baba harusi ndo kafikaa nikasema ngoja nikupigie simu mie nichekee we nae unatumika tuu ... nawe ulikuwa unamlea mikaa???'"
Ilibidi kwanzza nitabasam kwa uchungu
"Kwahiyo happy unataka kuniambia mika pale ndio kafika"
"Eeeh navyosikia huyo mika hana hata makazi anaishigi kwa washkaji zake tu,,kwahiyo we hujui "
"Khaaa!!! Alhamdulillah..."
Nilinyoosha mikono juu kumshkuru mungu
"Yaan happy mimi mika hata simjui vizuri jamani , tulikutana kwenye mishe mishe mtaani tukaanza mahusiano hata miezi miwili bado nikagundua anatembea na emmy kuwafatilia ndo ile siku nikawakuta chumbani kwa emmy tena wanasuguana heee mbona makubwaaa!!!"
"Ndo hayo dada waswahili wanasema likuepukalo lina heli nawe" mmmh niliguna Tu tukaendelea pale kupiga umbea mana ndo chakula cha uswahilini tena
(Umekula..??) Hee kikaingia ki msg kutoka wa Abbas jamani kamoyo kakafanya Puh🙌🥰
( ndo nataka nifanye mpango)
(Fanya ule muda wa lunch huu)
(We tayari)
(Ndo nakula hapa nikasema mamkubwa kala kweliii??)
Nikaweka emmoj za kucheka tuu sikuandika chochote akanijibu unanichekaa?? Hee nikaweka tena za kucheka safari hii zile za machozi kabisa Hapana bwana nimefurahi tuu
(Mmh haya bwana Mchana mwema)
Jamani mimi nilikuwa na hamu ya kuchati hivyooo et mchana mwema nikamjibu Tu nawe pia...

Nilimaliza biashara zangu siku hiyo karibu giza linaingia taratibu nikajisukuma kurudi nyumbani nikawa nakumbuka mahusiano yangu na mika yaludumu kwa muda mchache sana ila hajawahi kunionesha anapoishi mara zote alikuwa anakuja yeye kwangu na nikimwambia nahitaji kupajua kwako ananiambia muda bado nisiwe na haraka kwahiyo hivyo pia vilifanya mimi nijione nina mkosi mana mwanaume hataki kushea na mimi chochote hata kazi yake tu hataki kunambia mladi namuona ona tu aise sasa nikawa nakumbuka na Tambo za emmy mmh nikaguna tu nikafik zangu home emmy alikuwa anapika pale nje ya mlango wake mume wake amekaa pembeni ya mlango nikasalimia zangu waliitikia majirani wengine na mume wa emmy aliitika lakini bibie walaa nami hata sikujali nikaingia ndani nikatoka na ghanga yangu moja tu nikaenda jimwaia maji nikavaa nikajipikia wakati nakula simu ikaita alikuwa Abbas .
Nikawa naongea nae huku nakula ana story huyo kaka jamani duh ila ukinuona hivi kawaida uso wake utasema huyu kaka haongei mpoleee eeh anaongea jaman hakaukiwi story yaan mimi ni kucheka tu nacheka tuu wee tuliongea mpaka nikaanza kusinzia hapo nishamaliza kula kitamboo akanambia basi lala bibie nisikuchoshe aaah nikavunga mi hata sina usingizi mbona🤗🤗Akanambia kuna kazi nataka kufanya nitakucheck kesho asubuhi sawa nikasema poa , alipo kata simu na usinginzi ulipo potelea hata sijui.

Nikawa nawaza sa mbona hata hanitongizi huyu kaka jamani au hajui kutongoza au ananichukulia tu kama rafiki yake mmh mi hata sielewi ,ka sms kaka ingia( mamkubwa usiku mwemaaa)
Waoooh🥰🥰🤗 jomoniii nisipo nawili huu mwaka ndo basi tenaaa nikawa nawaza sijui nijibu aje nikiandika nawe pia naona imekaa vibaya nafuta Shukrani kwako pia mmh nafuta 🤦‍♂️sa niandike Ka neno gani kazuriiii??
Mwisho niliamua tu kuikumbatia simu usingizi nao ukanisalimu kimojaaa ...

Asubuhi kama kawaida niliamshwa na simu kuangalia Babyyyy🥰🥰 Abbas huyoo nikapokea haraka haraka jamani hapo mi hata sijatongozwa wala sijui kwanini huyu kaka ananitafuta tafuta sana lakini mi ndo nampendaaa natamani hata mimi ndio nimtongoze Jamaniiii 🙌🙌
"Hellow kumekucha mamkubwa "
"Nakwambia ndo unaniamsha hapa ubarikiwe ilibaki kidogo nipitilize" nilijibu huku najichekesha😀 tukapiga piga story akanambia ye ndo anaenda kibaruani kwake kwahiyo badae nikasema poa nami nikainuka kuoga nina bahati mbaya kweli si nikakutana tena na mika kajifunga kagha😄😄😄 ila wanaume wengine bwana mi sipendi basi vile vimakalio vinakaa khaa🙌🙌😄 ujinga Tu
Nikachekea moyoni tukapishana akamsalimia sikuwa hata na shida nikaitika ...

Huyo nikaingia mishe mishe zangu , sa wakati nipo pale nikasikia happy yule shoga angu akasema "weee mbona bi harusi anaanza kazi siku ya pili hakai hata saba" sindo nikageuka eh namkuta Emmy anasafisha kibanda chake mana sie ni majirani Haa!! Mwenyewe nikamshangaa yaan bibi harusi siku ya pili anaaza kazi makubwa hayo nikameza mate nikaendelea na kazi zangu ....

Nilikuwa wa kwanza kumaliza kabla ya emmy nikarudi om, ule muda napika ye ndo akawa anarudi anajipigisha vimafumbo et uchawi umekomaa mpaka kwenye biashara basi anacheka na shoga ake alikuwa wa chumba cha mwisho nikaona wote wajinga hapo Abbas akanipigia simu basi naongea zangu ananichekesha we nachekaaa nacheka mpaka basiii tulipiga story nikamwaliza kupiga nikawa nakula tunongea tu yaan mpaka muda wa kulala basi mi naona Rahaaaa🥰🥰 kazi yangu ni kuhamisha tu sikio hili mara lile kubadili pozi za kulala yaan mpaka basi....

Siku moja nilikuwa naongea na abbas kama kawaida usiku akanambia anaomba hata anione maana imekuwa siku nyingi kweli tangu tuonane tunaongea tu kwa simu , mwenyewe hiyo ndo nafasi nilikuwa naitaka mana mnh sio poa basi akaniuliza lini upo free wacha niseme mi siku yeyote tu nipo free akanambia sio kweli we ni mtu wa kazi bwana,🤦‍♂️ nikaona mpaka aibu maana mi kila siku mtaani sina jpl wa ijumaa nikamwambi w/end huwa napumzika nikamuongopea mi staki hii nafasi niikose mjue🤗🤗 akasema basi mi nitakuchek jpili ndio siku siendi kazini okay nikasema poa poa ......

W/end basi inachelewa🥰🥰 naona kama ni mwakani kulee kila siku nilikuwa napanga vile viwalo nilikuwaga naanunua vya kishua navijaribu wapii mmh naona kama vya kihuni afu hawa wasudani hawa si wanajifunikaga funikaga sana wacha nikavunje kibubu changu huyoo mpaka dukani nikaenda kutafuta nguo ya heshima nikanunua zangu gauni Refuu sema ndo limenishika hatari yaan ule mshepu wa kitusi mule mulee🥰🥰🥰

ITAENDELEA....

DOCTOR NITIBU NA HUKU KUNAWASHA🌹🌹❤️❤️❤️🌹
❤👌👌07

Nikachukua gauni langu hilo la heshima lisilo kuwa na adabu na kimtandio kidogo dogo tuu nisije onekana mzee buree👌

Siku hatimae ikafika mwenyewe niliamka asubuhi nasubiri tu simu yaan hapo nishajipanga kila kitu kipo kitandani, mida ya sa 5 hivi akanipigia simu akanambia mamkubwa jiandae nitakwambia uje sehemu nikasema sawa ,fastaa nikaenda kuoga zangu nikajiweka sawa mtoto wa kikee nikavaa gauni langu la utu lisilo na utulivu nikajitupia kimtandio changu viatu vyangu vya bei bei hivyo nilinunuaga kariakoo nikavitunza mana hata mitoko mi sina 🤦‍♂️
Nikapaka ki wanja wa chini ya macho na ka rangi ka mdomo poda angu kwa mbaliii na hili joto la Dar utafikiri nitafika nayo hata mbali😀😀 ,namaliza tu kujiweka sawa na simu inaita akanambia njoo hapa Pweza beach nikasema sawa akaniuliza nauli unayo ,huyu kaka vipi wakati wenzie wanatumaga tu nauli bila hata maswali aah nikamjibu ninayo 🤔sitaki mambo mengi mana hata hakuna mwanaume wangu hata mmoja aliwahi kunipa mtoko sana tunakutana vichochoron wananishika shika weeee afu naenda hom hakuna hata la maana humo Beach tubebane na mashoga zangu tu ....

Wakati natoka sasa si nikakutana na mika anatoka chooni sijui hata kama anatokaga huyu kaka jamani puuuh🙌🙌🙌
Nikashangaa ananiita pale palikuwa kimyaa kweli nilkuwa nje mimi na yeye nikageka kumtazama et akanambia umependeza nikamwambia asante akanambia Samahani Naah naweza kupata muda nahitaji kuongea nawewe "
Haa hivi huyu kaka anaakili sawa sawa nilimtazama kwa zaidi ya sec kumi kwanza afu nikamwambia mi sina muda kaka angu nisepa huku namtikisia takoo👌👌 nikamuacha kakodoa macho kama mjusi aliebanwa na mlango.
Nikakumbuka kuna siku niliamka usiku kukojoa nikasikia wanazozana mwanamke alikuwa anamwambia mika
"Nimechoka we kila siku uongo ndo uongo ulisema ndugu zako waliokuja harusini wanaondoka tunaamia kwako lakini kila siku huishiwi mapya mi mika nimechoka haya hela huna kila siku kila siku aah nimechoka bwanaa najua nimeolewa ili nipumzike kumbe mateso ndo yanazidii:"
."lakini emmy si nimekwambia kuhusu matatizo yangu kazini kuna ubadhilifu wa fedha ulitokea bado kuna uchunguzi unafanyika nitarudishwa kazini naapa nitakununulia kiwanja chako kule siwezi kumfukuza baba emmy embu nielewe " haloo nilisikiliza kidogo nikaenda zangu uwani mambo yawapenzi haoo..
Leo linataka kuongea nini na mimi?? Wakati analelewa😀😀 Anikomeee!!!!

Nikachukua boda mpaka zakhem mwenzangu nikapanda gari za kigamboni ,
Baada ya lisaa kama na nusu hivi nipo nje ya geti pale nikampigia simu akanambia ingia nitakuona , nilipo ingia akasema "MASHAALLAH kidogo nikusahau kama nisingeona huo mwanya" 😀😀😀 nikacheka yaan hapo ndo nikakumbuka kumbe mimi huwa nina mwanya
Tukaenda kwenye meza flani akanambia unakula nini nikasema chochote, naona aibu achaa sijawahi mimi mitoko kama hii jaman mjueee, akamuita muhudumu akaja akamuuliza et hapa mnachakula kinaitwa chochote yaan mpaka nikacheka kwa sauti muhudumu nae ilibidi tu acheke akatupa menu tuchague nikamuomba anichagulie mana niliona soda tu 2000 jaman
Nisije kuchagua vyakula bei ikawa kubwa mfuko mdogo basi akanichagulia pale nikasema ewaa yaan alipita mule mule😋😋

Nikala zangu tunapiga tu stoy za hapa na pale baada ya kula akanambia twende tukaguse hata maji basi si wanasema maji ya bahari yanatoa mikosi ,mmh nikamjibu mi mwenyewe nasikiaga sema sina hata nguo za kubadili..
Akachukua begi alikuwa nalo la mgongoni dogo dogo akanipa
" nenda kuna nguo humo kabadilishe " nikaenda mpaka maliwatoni nikakuta ki kaptura kizurii cha jinzii afu Highest na crop top jaman niliona aibuuu yaan hizi kabeba kwa ajili yanguuu au ???
Nikavaa afu nguo zangu nitajia kwenye begi natoka hata kutembea hatua zinakanyagana nilikuwa namuonea aibuu na vile manyonyo yangu yalivyodede afu yamejaa basi nikitembea hivii yanaruka aah🤦‍♂️🤦‍♂️🙌 huo mshepu nilijaariwa Tumbo mie sina japo umri umeenda 😀😀Na vile sijajaaliwa mtoto tumbo bado safiii ka kitovu kazurii nyiee🙌🙌 basi nikamkuta amekaa pale pale nae kashabadili nguo wakati nasogea alipo alisimama aiyaa weee🥰🥰🥰🥰Mungu fundi bwanaaa🙏 mkaka amevaa pensi bwana pensi kalii achana na bukta za wacheza mpiraa kwanza afu juu kifua wazi anatumbo kama la wazungu limeingua ndaniii 😀 Afuu pensi kama inataka kutoka hivi kiunoni lakini bado ipo basi nyonga kwa mbali zinaonekana akaja akanishika mkono hao mpaka kwenye maji ilikuwa ndio mara ya kwanza yeye kunishika mkono mkono wake ulikuwa rainii mi nae sijui ndo kupenda yaan mi naona hata akilia nitaona analia vizuri tena anavutia mnoo😀😀
"Unajua kuogelea??" Aliniuliza wakati maji yametufikia magotini
"Mimi najua tu kuchezea maji " nikajibu huku nacheka
"Hayaa twende nitakuogesha " mwili wote ukanisisimkaaaa kuogeshwa tenaa👌👌
Akanipeleka mpaka maji yakafika shingoni hapo naogopa jamani wee " mi sijawahi kufika huku naogoaa"
"Usiogope njoo hapa" akachukua migu yangu akawa amenipakata yaan nimeipitisha kwenye kiuno chake , tupo bahari lakini anaharufu bado nzurii we nasra wee acha ujinga😀 nikajishtua mana niliona kila dalili za shetani kunipitia akawa anapeleka kwenye maji marefuu nilienjoy hatariiii hapo ananibadilisha tu mara nisimame anishike niwe natembea mwenyewe kwenye maji kuna muda akaishika miguu yangu akawa anaivuta mi najidai kupiga mbizii 🥰🥰Raha kwelii kwenda beach na mtu anajua kuchezea maji.

Mwisho akanipakata tenaa ila pensi yake ilikuwa imerowaa😜😜 akaniuliza umechokaa ,?
Nikamwambia "hata sijachoka labda kama wewe umechokaa tutokee "
"Nasraa" aliniita huku ananitazama usonii nyieee nilipo mwangalia maana alikuwa kama amenipakata kiunoni nyuso zetu zinatizamana macho yake yalikuwa mekunduuu ndo akazidi kuwa muhandome🥰🥰
"Abee" nami si nikamkazia macho bwana tukawa tunatizamana mwe🙌
"Una boyfriend " mpaka nilipaliwa na mate kwanzaaa , moyoni nikasema tunda limeivaa hiliii muda ndo huu

ITAENDELEA....
Soma mpaka mwishoooo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0781858056.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

DOCTOR NITIBU NA HUKU KUNAWASHA🌹🌹❤️❤️❤️🌹 ❤👌👌06... 7  >>> https://gonga94.com/semajambo/doctor-nitibu-na-huku-kunawasha-06-7
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

GIGY MONEY DAH😭

majario rewards 100 Comments 0
 

YOUNG AFRICANS,

majario rewards 100 Comments 0
 

BAKORA VILLAGE

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 7...8

majario rewards 100 Comments 0
 

HUYU KAKA EPISODE 2

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE...5...6

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 3...4

majario rewards 100 Comments 0
 

HUYU KAKA 1

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈21

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈20

majario rewards 100 Comments 0
 

DADA WA KAZI EPISODE 8

majario rewards 100 Comments 0
 

DADA WA KAZI EPISODE 7

majario rewards 100 Comments 0
 

Life in a Year (2020)

majario rewards 100 Comments 0
 

Kenya, Tanzania, Congo

majario rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY 40

majario rewards 100 Comments 0
 

POSHY QUEEN:

majario rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY 39

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈19

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈18

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈17

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈16

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈15

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 05 ❤❤.

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 04 ❤❤.

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 03 ❤❤.

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 02 ❤❤.

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 01 ❤❤.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY 34

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈14

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈13

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈10

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

TUWASHUKURU KINA BABA

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest