MTUNZI; LIZY MICA
Endelea ๐ป
Sultana aliachia tabasamu baada ya kumuona Liam....hakutaka kukivungia chakula, alikula chote kwa dakika chache
"Sijui vyakula vyao wanapika kwa kutumia nini....ni kingi kwa macho lakini ni kidogo sana pale unapoanza kukitia mdomoni" Sultana aliongea baada ya kusogea kwenye meza ya Liam
"Mhudumu leta sahani nyingine...." Liam alimuagizia chakula kwa mara ya pili
Safari hii Sultana hakula badala yake alianza kukikagua
"Sasa nimeelewa kwanini tumbo langu linahitaji kula bado.... vipande vya nyama vimekatwa vidogo sana kama punje ya mchele...mboga mboga wamezifanya nyepesi sana kama karatasi, wali wao wameusambaza ili uonekane mwingi, kama ningeujua huu mchezo mapema nisinge kula" Sultana aliongea na kumfanya Liam atabasamu
"Anyway, hapa ni mjini vitu vingi vipo juu sana....kama akikata vipande vya nyama ukubwa wa ngumi yangu atapata hasara badala ya faida" Liam alikumbusha
"Na hii ndio sababu narudi Kijijini maisha ya kule ni rahisi sana tofauti na huku" Sultana aliongea
"Muonekano wako hauruhusu kuishi Kijijini unatakiwa kuwa pambo kwenye Jiji kama hili.." Liam alishauri
"Ni ngumu kuishi Jiji kama hili bila kazi.... usiniambie unataka kuwa sponsor wangu, nipo tayari kwa hilo kikubwa nisilale njaa wala kusumbuliwa na mwenye nyumba" Sultana aliongea huku akitabasamu
Liam alijikuta akimtazama na hata akasahau kama ni zamu yake kutoa jibu.
"Tutaonana kwa wakati mwingine..... nahitaji kuwahi gari" Sultana aliongea baada ya kuona mtu anayeongea naye katekewa
"Ni kitu gani kimekuleta mjini, au wewe ni mfanya biashara wa mazao napenda sana kilimo lakini sijui nianzie wapi" Liam aliongea
"Nikikueleza kazi nayofanya utapatwa na mshtuko wa moyo....uwe na siku njema" Sultana aliongea kisha akasimama asepe
Liam hakuwa tayari kumuacha binti huyu aondoke bado alikuwa na hamu ya kuongea naye
"Usihofu kuhusu usafiri nitakurejesha mwenyewe siku ya kesho na gari langu....sijui umeniroga lakini nimejikuta ni kitamani kuongea na wewe" Liam aliongea, simu yake iliita.... mpigaji alikuwa ni Sona aliirudisha mfukoni badala ya kupokea
"Kuliko tukae hapa kuwa mwenyeji wangu....natamani kuiona fahari ya Jiji la Odes nikijua siku ya kesho utanipeleka Kijijini kwetu" Sultana aliongea
Liam hakuwa na ubishi.....kwa pamoja waliingia ndani ya gari wakaanza kuzunguka huku na kule
๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป๐ป
Sona hakukata tamaa, aliendelea kupiga simu mpaka mida ya usiku lakini Liam hakupatikana.
Ukweli ni kwamba Liam na Sultana walikuwa kwenye Club moja kubwa kuliko yote Jijini Odes wakishangaa namna watu wanavyocheza mziki
"Watu wanajirusha kama kesho hawataliona jua.... hakika wanajua kuitendea haki leo" Sultana aliongea
Liam hakuwa na maneno ya kuongea zaidi ya kumkodolea macho.
"Kwanini unanitazama hivyo, usiniambie unafikiria ni namna gani utapata figo zangu ukauze....au unataka kuchuna ngozi yangu " Sultana aliuliza
"Una uzuri wa pekee, ni kawaida kwa Mwanaume yoyote kukuangalia bila kukoma...." Liam aliongea
"Jiji la Odes ni la kawaida sana.... itapendeza ni kipumzika" Sultana aliongea, macho yake yalionekana kuwa na usingizi kupita kiasi
Liam alikuwa mwema, alimpeleka kwenye hotel aliyoamini inatoa huduma nzuri kuliko zote ....bahati mbaya kulikuwa kumesalia chumba kimoja.
"Naomba unisamehe tutalala hapa wote...." Liam aliongea
Sultana hakuwa na muda wa kuzungumza alijitupa kitandani, dakika tano zilikuwa ni nyingi kwake kusinzia
Liam alikuwa na wakati mgumu alijikuta akimsogelea Sultana aliyekuwa hajitambui.
Kitendo cha kushika tu mgongo wake bila ruhusa alikula kofi la uso
"Huna haja ya kunivizia.....tamka kiasi cha pesa ulichonacho nitakuhudumia kulingana na kodi yako..." Sultana hakuona aibu kuzungumza kuhusu kazi yake
Liam hakutaka kujua kuhusu biashara yake, alimpatia pesa alizonazo huku akiahidi kumuongezea zingine siku ya kesho akipita ATM
Walijikuta wakifanya mapenzi baada ya kuafikiana.
Kwa mara ya kwanza Sultana alifurahia kwa namna Mwanaume huyu alivyokuwa ana mtendea kama mkewe na si Kahaba
Kulivyo pambazuka asubuhi..... walielekea ATM kutoa pesa, zilikuwa ni pesa nyingi kiasi kwamba Sultana aliogopa kuzichukua
Liam alimkabidhi zote, kwa kuwa wote walikuwa na njaa walikuwa na njaa iliwalazimu kupita hotelini kunywa chai
Ilikuwa ni hoteli ya kifahari, walisubiria dakika chache lifti ifunguke ili waingie.
Macho ya Sultana yalipatwa na mshangao baada ya lifti kufunguka.....begi lake la pesa lilidondoka chini
Itaendelea ๐ฅ.