Aryan aliumia sana na kujikuta anaongea kwa uchungu Mussa nimewakosea nini hadi mfikie hatua ya kutaka kunipa ukilema? Yule jamaa alinyanyua ile sindano ile anataka tu kumchoma sindano machoni alijikuta akiidondosha mwenyewe kisha alishuka chini taratibu na kusema jamani tumbo linaniuma , hakika yule njemba alijaribu kujikaza lakini hakuweza hadi akalala chini huku akihisi mwili wake kukosa nguvu,
Wenzake walivyoona mwenzao kapatwa na homa ya tumbo ghafla ndipo njemba ya tatu alitoa upanga ili amkate Aryan mikono na miguu lakini hata yeye hakufanikiwa alikamatwa na tumbo ,anajikuta anaachia upanga huku akilia kwa maumivu tumboo jamani tumbooo,
Sasa njemba ya tatu ambae alikuwa amemkaba Aryan kwa nyuma nae tumbo likamkamata vile vile wakajikuta wanamwachia Aryan
Walianza kutembea kwa kutambaa na kujiburuza maana waliumwa tumbo kwenye kitovu na walihisi limekaza ,walijiburuza huku Aryan akiwashangaa na kujiuliza hawa watu nini kimewakuta ,"ooh asante Mungu"Aryan alijisemea moyoni.
Aryan hakutaka lile suala alipeleke polisi,wale njemba walijiburuza weee hadi walivyotoka nje walishangaa wanakuwa poa hata matumbo yao hayaumi tena ,
Oya mwamba tumbo langu haliumi tena kwani ilikuwa ni nini? Njemba moja aliuliza huku wakipanda kwenye bajaji ,mmoja aliguna na kusema mmmh kwa leo tuache kumfanyia ubaya yule jamaa maana nilihisi kufa kufa ,waliondoka zao.
Basi siku hiyo Aryan alikaa na bibi wakapakua chakula chao wakaanza kula ,Aryan alimsaidia bibi kumega matonge anampa kwenye mkono halafu anaupeleka mkono wa bibi hadi kwenye chombo cha mboga hakika bibi alijihisi faraja baada ya kufadhiliwa na Aryan walivyomaliza kula bibi alimwita Aryan.
Aryan nae alienda na kukaa karibu yake ,bibi alishika mkono wa Aryan kisha akaanza kuonge"Aryan mjukuu wangu nimekaa hapa japo kwa muda mfupi ila nimegundua kuwa watu wengi wanao kuzunguka hawakupendi wengi wao ,hasa hawa majirani ,jana wakati naenda msalani ,majirani walikuja na kuniambia niondoke huu mtaa ",Aryan alimwangalia bibi ambae goti lake bado halijapona vizuri ,Aryan alisema " bibi nimesema hakuna kuondoka hapa mimi nitahakikisha nakulinda nakuhudumia kwa kila kitu ,
Kisha bibi akaendelea na maongezi ,"usiku nimeota ndoto mbaya mama mmoja kafukuzwa kazi ambayo alikuwa akifanya ,huyo mama alivyofukuzwa wakati ana mawazo ya kufukuzwa kazi alipita kandokando ya barabara aligongwa na gari ila hakuumia sana ,ila kapelekwa hospitali,
.Aryan alitabasamu na kumwambia bibi ndio maana napenda kukaa na wewe story zako bana huwa zinanifurahisha ,sasa hio si ndoto ya kawaida bibi?
Bibi alitabasamu na kumwambia ndio ya kawaida ila nimejisikia kukuambia tu ,yalikuwa maongezi huku Aryan akimsugua bibi miguu na maji ya uvuguvugu,bibi alianza kupendeza na kuonekana safi.
Tukirudi maeno ya mwenge mama yake na Aryan baada ya kufukuzwa kule kwa akina Jesca aliondoka zake akiwa anavuka bara bara hakuangalia gari pande mbili za barabara,
Mama akajikuta anagogwa na gari na kudondoka ,kelele zilisikika watu wakisema ajali ajali ,watu walikimbia hadi kwa yule mama ,bahati nzuri aliyemgonga alikuwa ni mama ,
Yule mama alikuwa na moyo wa kipekee alishuka upesi kwenye gari na kuomba watu wamsaidie kumpakia huyo mama kwenye gari yake ,hakupenda kuchelewesha alimuwahisha hospitali.
Mama alioneka kuchubuka maeneo ya mkono wa kulia na damu nyingi kumtoka sana puani ,
Yule mama baada ya kumpakia yule mama aliyemgonga ,kila akiangalia ile damu inayotoka kwa yule mama anaitamani akitaka kupeleka kidole walau achovye alambe kidogo anasita, mara simu yake ikaita aliipokea na kusema
Haloo ,upande wa pili sauti ilisikika ikisema mama leo sijisikii vizuri nimeenda kwa rafiki yangu Jesca ,nilichokiona kule hata sijapenda Jesca kamfanyia roho mbaya mfanya kazi wao wa ndani
"Samairah mwanangu haya nenda nyumbani nikirudi tutaongea vizuri" kisha mama akakata simu ,kumbe aliyemgonga ni mama yake na Samaira ,ambae samairah alitokea kumpenda huyo mama.
Na tukirudi nyuma ile ndoto ya bibi aliyemsimulia Aryan kuwa ameota mama mmoja kapata ajali ilikuwa ndoto ya ukweli ni mama yake na Aryan kapata ajali.
Tukirudi maeneo ya muhimbili mama aliwahishwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi alipokelewa kisha akaanza kufanyiwa matihabu, lakini mama yake Samairah ambae ndiye alimgonga alirudi kwenye gari na kuanza kulamba ile damu ya mama ambae ilidondoka kwenye siti ya gari.
Mama alilamba ile damu yote ,kisha akasema natamani nirudi katika hali yangu ila binti yangu nitamuachaje? Mama alitikisa kichwa kisha akawasha gari nakuondoka zake
Mama Samairah ni mtu wa aina gani hadi analamba damu za watu na anasema anataka kurudi katika hali yake.
Tukirudi maeneo ya mikocheni zile njemba baada ya kushidwa kumtoboa macho Aryan walirudi kwa akina Kudra na kuwaeleza kila kitu kwamba wameshidwa ile kazi ,Kudra alichukia sana na kuwaambia wakamtafute tena na kuhakikisha wanamtoboa macho Aryan,
SAMAIRAH ๐โค๏ธ๐
*____Mr Burudan______*
SEHEMU YA 02
Hatimae siku ijayofuata wakiwa darasani Mussa alisimama na kusema jamani nyie wasichana kama mnajipenda nione mtu anamfuata Aryan nitakachomfanyia kitu atajuta ,wasichana wote walitokea kumchukia sana Mussa ,Jesca alisimama na kusema mimi kwa Aryan hunitoi ntamfuata,,, tena pale pale Jesca alichukua kiti na kwenda kukaa karibu yake.
Jesca alimsogelea Aryan na kumnong'oneza "Aryan nakupenda kwanini hutaki kunisikiliza moyo wangu umekuchagua wewe ni samehe hata kwa mabaya yote niliyokufanyia niko tayari kufanya chochote kwa ajili yako",,hayo ni maneno yake Jesca alitokea kumpenda sana Aryan ,ila tatizo Aryan huwa hawapendi wanawake.
Yale maneno ya Jesca yalimfanya Aryan asimame na kumwambia haya nimekusikia nitakujibu baadae kisha Aryan na akaondoka zake ,siku hio Jesca alijisikia amani baada ya Aryan kumwambia atamjibu baadae.
Tukirudi kwa Samairah alikuwa kajiinamia kwa mara ya kwanza alijikuta anaanza kumuwaza Aryan ,"ivi kwa mfano Aryan akiwa mpenzi wangu si itapendeza ee nikiwa njiani twashikana kikono nikienda kwao kujisomea twacheza" Samairah akajikuta anatabasamu.
Aryan baada ya kurudi tena darasani mwalimu aliingia na kuanza kufundisha basi Samairah aliingiza mkono kwenye dawati na kutoa daftari lake lakini kwenye begi aliweka ile bangili aliyopewa na mama yake Aryan
Ile bangili ilidondoka chini kengereee ,ile sauti ya mshido wa bangili baada ya kudondoka kila mwanafunzi akajikuta anageuza macho aliko Samairah
Hata Aryan aliangalia lakini Aryan alipoiona ile bangili alisimama na kuitazama vizuri,Aryan alijisemea ile bangili ya Samairah mbona inafanana na bangili yangu ninayoipendaga ,daa mama angekuwepo ningeenda kuiangalia sasa hata sijui mama alikoiweka ila inafanana sana.
Aryan alipotezea na kuendelea na masomo huku Samairah aliiokota ile bangili na kuiweka kwenye begi kisha masomo yakaendelea,hatimae walimaliza kipindi na muda wa mapumziko uliwadia
Jesca alikutana na Samairah kisha
Jesca alimuuliza hivi Samairah ,"ushaniambiaga kuwa Aryan hana mama?" Samairah aliitikia ndio mama yake hajui aliko Jesca alitulia kidogo kisha akasema "ningejua mama yake aliko ningemfuata nimweleze kuwa nampenda mwanae halafu ningempenda mama yake na Aryan ningemnunulia mazawadi naimani Aryan nae angenipenda,,unaonaje wikiendi hii tuende kwa Aryan kujisomea maana wewe si uliniambia unapajua ,
Samaira alitulia kidogo na kumwambia sawa tutaenda halafu si unajua jumatatu tunaanza mitihani ee ,ila kuhusu mama yake na Aryan hata sijui nikushauri vipi maana we mwenyewe hupendi watu wa hali ya chini maana hata majuzi ulinishangaza ulivyomfanyia yule mama aliyekuwa anafanya kazi za ndani kwenu.
Jesca aliongea ,"aah lile limama silipendi tu halafu nishawahi kuliwekea hadi sumu nusu afe sema baba aliwahi kumpeleka hospitali ki ukweli yule mama mmmm silipendi sijui kwa nini sema baba alikuwa anampenda sababu anajua kupika ,nilikuwa nampiga hata makofi ,basi tu nilitokea kumchukia".
Yule ndo mama yake halisi na Aryan na anasema halipendi lile limama halafu anamuulizia mama yake na Aryan ili awe anampelekea zawadi mi sijui akija kugundua kuwa yule ni mama yake na Aryan atafanyaje.
Siku hiyo Aryan alivyoona ile bangili alijikuta anakosa raha na kusema mama yangu angekuwepo ningefurahi mno halafu ile bangili yangu nishawahi kumwambia nitamvisha mwanamke ninayempenda,Aryan wakati anawaza alishangaa warembo wawili wanamgusa kichwa.
We Aryan mbona una mawazo ya nini bana jumamosi tunakuja kwako kujisomea alikuwa ni bibie Samairah wakiwa na Jesca ,Aryan alisema poa karibuni.
Hatimae wanafunzi waliruhusiwa na ilikuwa ni ijumaa walitangaziwa kuwa jumatatu wanaanza mitihani ya kufunga mhula wa pili ,wanafunzi walitawanyika lakini Samairah alimkimbilia Aryan na kumpa kibahasha flani ,Aryan alikipokea na kuuliza kina nini?
Samairah alimkabidhi na kusema utaona huko huko nyumbani ,Aryan alifika nyumbani aliangalia alikuta kuna noti mbili za elfu kumi Aryan alifurahi kama kawaida aliwasha jiko akapika kisha akamwamusha bibi wakala.
Usiku uliingia Aryan siku hiyo hakusoma alilala.
Aryan alianza kuota ndoto yupo ufukweni na bibie Samairah na wanafurahi kwa pamoja lakini wakiwa katika pozi la kukumbatiana , Aryan aligeuza macho nyuma aliweza kuona kundi la akina Kudra wamesimama nyuma yao halafu Kudra ameshika bastola na kumnyoshea,,Kudra alicheka kwa nguvu na kusema huyo Samairah ni mpenzi wangu nampenda kwakuwa wewe hunisikii wasalimie kuzimu Kudra aliinyoosha bastola kwa Aryan.
Aryan akajikuta anapiga kelele ,usiku kisha akainuka "aaah kumbe naota" duu ile anainua kichwa baada ya kutoka kwenye ndoto ukweli Aryan alishangaa kuwaona wanaume watatu wamesimama chumbani mwake ,.Aryan kucheki mlangoni
Mlango umevunjwa mara akamulikwa tochi kisha akaoneshwa shoka.
Muendelezo ni sh 1000
Njoo WhatsApp 0781858056.