Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

NILIZANI MWIZI KUMBE MMMM💘💐💘 SEHEMU YA (09__10)

4th Jul, 2025 Views 59



Tulipo kutanisha macho Alex akatabasam afu akaniuliza "Umechoka eeh??"

"Kwanini"

"Aah nakuona tu!!"

"Mi nipo sawa mbona"

"Pole nimekusumbua usiku "

Nikatabasam tu bila kujibu kitu ,muda huo alikuwa amekuja yule mdada wa chakula

"Embu tunaomba na nyama choma eeh"
Akamuagiza tena yule dada ,alikubali kuleta akaondoka"

"Haya kula mama,nimeamua kuchukua chakula chepesi kwa sababu ni usiku naimani utapenda" alinisogezea huku anajitetea nikasema sawa"

Basi my wenu nikawa nakula kwa aibu yaan nahesabu dakika za kuchukua nyama😁 ,ye alimaliza muda kweli mpaka nikajiona mjinga mana alex alikuwa hata havungi anapakia haraka haraka😆 ,

akanisubiri nikamaliza kula ,nimejaza tumbo hatari ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kabisa kuja sehemu Maalumu kama hizi .

Usiku ulikuwa umeenda sana ndio tulitoka pale mpaka nyumbani kwangu , siku hiyo Alex alilala hapo mpaka asubuhi🥰alilala kwenye kochi bwana hahahahaa,

alinambia atakuwa bize siku mbili tatu ila akimaliza tu atakuja kuniona ,nilimwambia Alex Asante nilipata ule mzigo nikimaanisha zile pesa akasema usijali hakukua na haja ya kusema Asante mi ndo natakiwa kusema hivyo huku nikiweka na Samahani,

naomba usimsogelee tena Juddy wala Yule mzee na akikufata hata kwa bahati mbaya tenaaa naomba unipigie simu hata nikiwa kati kati ya kazi ama usiku wa maneno nitakuja hapa na safar hii sintawachekea tena ila nitawafunza kuheshimu kila mtu .

Alex aliongea kikomando kweli ,nikahisi sifaaa kutetewa ha ha ha nilipenda hiyooo ,nikasema sawa akaondoka zake , majirani machooo yote kwenye mlango wangu na hivi asubuhi alienda kuoga wee niliuza hatari😁...

Basi asubuhi hiyo Ile alex ametoka tu juddy huyu hapa kafika,nilikuwa nipo nje napika zangu chai akanifuata akaniambia "Naomba tuongee!!" tena kwa amri ,nilimtazamaaaaa zaidi ya sec kumi afu nikainuka mana mi nilikuwa nimekaa ye kasimama pembeni yangu..

"Kuhusu nini???" Nilimuuliza kwa nyodoo mana kama bwana ake hamtakii mi tena inanihusu ninii?? Na alex amenipa li kichwa ole wakeee anigusee hee atafurahii"

"Salmaaa"

"Kumbe na jina langu unajua kulitamka tena vyema tu ?? Haya ondoka sitaki balaa na huyo mzee wako!!"

Mi tenaaa nilipo maliza kumnyambua nikarudi kukaa

"Ha hahahah hivii unajiona umepata bwana eeh??? Kwa taarifa yako kumleta alex aje kulala chumbani kwako sio kama anakupenda Anakutumia kuniumiza mie..

pole sanaa unatumiwa kama chombo cha kisasi tu amalize hasira zake ila hapa hakuna mbwa aliewahi kuchomoka bila idhini yangu"
Nilimtazama vile anajinadii afu nikacheka rohoni

"Sasa kama hakuna mbwa anaechomoka kwako , kwanini unakuja kuhangaika na mimi ndama nisie hata na chembe ya maziwa ??

Kwanini usichukue mbwa zako ukafungia huko ziache kuhangaika hovyoo??alinikata jicho mihasira kama yote mie huyooo

Nikaingia zangu ndani akabaki anatoa tu machoo hapo mana alikuwa anaongea sauti ndogo tulikuwa mimi na yeye , mi ndo nikapaisha maksudi ili na walio ndani wasikie , nikaingia chumbani kwangu nikafunga na mlango , sijui hata aliondoka muda gani ...

Basi baada ya muda alikuja zakia best yangu akaniambia"shogaaa em nipe ubuyu wewe mwenyeweeee mana naona habari zanichanganya tu miee"

"Ubuyu upiii"

"Sielewi wajuaaa, naskia mara jana umepigwa na mzee amos, et unamkuwadia juddy kwa wanaume ,hilo halijashuka naskia unachangia bwana na Juddy na mnaugomvi

saa sielewi nikasema huyu udugu wangu miee namjua nimemzaa mwenyewe wacha niendee ,ndo nishakuja hapaaa afu nimemuona Juddy anatoka hapa kwako em niambie kulikoni🤗"

Nilijichekesha chekesha tu mana hata sijui nimwambie nini aisee

"Sijawahi mkuwadia yule dada bwana ,wala mi sichangii nae bwana"

"Sasa shida nini?? Kwanini mzee amos akufate jana ??"

"Aah atajua yeye bwana ,wote wapuuzi tu"

"Yaaan watu walivyomchoka huyo mzee basi tu kila mtu kashamdharau sio kama zamani alivyokuwa anapewa heshima "

"Wanahama lini kwanza mi nilivyo wachoka"

"Wee mpya hizi tena nasikia shoga anahamia hapo kwa mzee amos wala haendi mbali"

Nilichoka nikasema huyu baba sijui amepewa nini jamani na Juddy mambo anayo fanya ni aibu afu yeye hata hajali et yupo kawaida , kwa sasa hivi mtaa wote unawatizama wao Aibu naona mie .

Simu yangu iliita namba haikuwa nime save lakini niliitambua hii namba ni inno alitumia alex ile siku nikaipokea hapo nipo na Zakia bado..

"Salmaaa!!!" Kabla hata sijasema haloo ,akaniita jina kwa kuchangamka kweli ,nikacheka nikamwambia mamboo!"

"Fresh kabisa vipi we uko poaa??"

"Alhamdulillah kiasi changu niko poa kabisa"

"Haya mi nipo hapa nje kwako nakuomba mrembo " hee nikashangaa huyu tena kwangu sa hiii???

Niliinuka fasta kutoka nje hata siamini ,nikahisi labda ananitania tu afu mi huyu kaka sijamzoea hata na wala sikuwahi kufikiria et anaweza kunitafuta kama hivii

Kweli bwana nilimkuta Gari imepak pale nje afu yeye amesimama ameegemea mgongo kwenye gari, walikuwa wawili na mkaka tu hivi nae alikuwa classic hatari

"Pole kwa kukuvamia " inno akanambia huku anajitoa pale alipo kuwa ameegemea

"Aah hata usijali"

"Mzima lakini??"

"Mi niko poa karibuni ndani!!"

"Aah sie hata hatukai,nilikuwa mahemezi hapo bro akanambia nikupitishie vitu baadhi nikamwambia ndugu yangu hapa tupite mara moja , Felix huyu anaitwa salma ni sister etu mpendwa kabisaaa"

"Ooh nafurahi kukufahamu mi naitwa Felix " alinisogelea akanipa mkono nami sikuwa na hiyana nikampa ili tusalimiane vizuri..

sasa wakati amenishika akawa ananigusa na kidole kimoja kati kati ya kiganja changu ,hii tabia siipendi miee nikamtazama akanibinyia Jicho khe huyu anaonekana mly huyu😁.....

Basi nikavunga afu nikavuta mkono wangu nyuma

"Vipi ndo shemu ninii??" Akamuuliza inno huku anacheka cheka ,yaan huyu kaka kwa hiyo tabia nilijikuta ninamchukia sana

"Hapana ni dada etu huyu mpnz kabisa kabisa, salma eh mi hata sio mkaaji " inno akazunguka akaenda kufungua mlango wa nyuma ya gari yake akatoa vyakula,

nilibaki nimeduwaaa jamani , alikuwa amebeba mazaga zaga kibaoo dah🥹.

Nilibaki nimeganda naona aibu hata kupiga hatua aisee,baada ya kuvitoa vyote kwenye gari yake akaanza kubeba anasogeza mlangoni mimi bado siamini kabisaa

"Yaan inno vyote hivi ni vyangu au sijaelewa??" Ilibidi niulize najionea makubwa tu mie

"Aaah na vingine vipo njiani vinakuja" hee nikasema sa niwashukuru vipiii?? Inno akanambia wakushukuru ni sisi hapa ,yaan salma kama shukrani tunatakiwa kuzitoa ni sie wala sio wewe haya njoo tuingize ndani basiiii"

Ilibdi nianze kubeba nahisi machozi kabisa yanataka kunitoka mbona kama nauaga hivi umaskini mie au ndo naukaribisha mana kama kazi nishaacha , lakini angalia napata chakula cha kula Karibu mwaka mzimaaaa .

Ukisikia nililala maskini nikaamka tajiri njoo uniulize mimi hapa nitakuthibitishia hakiamungu , moyo ulikuwa umekauka kuna kitu nahisi kimenikaba nilikuwa natamani sana kulia lakini nina jikaza hatari .

Zakia nae akaja kunisaidia kuingiza vitu ndani ,mpaka tukamaliza inno akatoa pesa akanambia nimeambiwa nikupe hizi akanipa elfu 50 nikamwmbia Asanteni sana

inno mungu awalipe kheri akasema Amina na mie zangu hizi naomba upokee ,niliona aibu nae alitoa laki moja nikasema hapana bwana vitu mlivyonipa vinatosha inatosha jamani mmenisaidia sanaaa
Hapo tulikuwa mimi nayeye tu tumesimama pembeni kabisa ,

akanambia salma kwenye haya maisha Alex ndo kitu changu cha thamani sana , hakuna yeye bila mimi ,mimi sio kitu bila yeye nilipo pata taarifa za kupotea kwake ukweli nilichanganyikiwa nilihisi kama nakufa asante kwa kumsaidia ndugu yangu..

Msaada wako salma ni kama umeokoa maisha ya watu wengi sana ,hata kama nitoe milioni nikupe hayo sio malipo ya ulicho kifanya naomba upokee kidogo chochote tutakacho leta kipenzi chetu please salmaaa "

nilichukua zile hela ,sio kwamba nilikuwa nakataa et kwa kupenda wapii?? Aibu tu mwenzangu ,nilipo chukua akaniaga nikamwambia jamani usubiri hata kulaa akasema ,siku ingine atakuja kushinda hapa kwangu na watakula kabisa haya sikuwa na lingine wakaondoka zao .

"Ndo huyo bwana wa Juddy??"

Baada tu ya wale kuondoka zakia akaanza uchunguzi wake

"We nae hata sio"

"Ndo shemu?? Umemtoa wapiii?? Ndo mana sikuhizi na kazi umeacha kumbe una uhakika wa kulaaa heheheh umejua kutunyoosha shoga"

Nilimuona zakia anatapa tapa tu kutafuta habari zangu akazagaze kijiweni kwao nami sikumpa nafasi nilimchotea Mchele na mafuta nikampa na ndizi alinishukuru akasahau na kunipeleleza😁huyo akashukuru na kuondoka..

nilichukua begi langu nikatoa zole hela alinipa alex nikazihesabu tena mimi ilikuwa kazi yangu kuhesabu pesa kila siku , nikachukua laki moja kwenye ile pesa amenipa inno nikaongezea pale ikawa laki sabaa ,nilifurahi nikamshukuru mungu sanaa..

Basi bwana maisha yalisonga siku moja usiku mida ya saa tatu nimemaliza zangu kupika najiandaa kwenda kuoga ghafla kwenye simu yangu kuliingia msg ndefu kweli nikaiangalia ile msg namba ni ngeni mmmhhh

Nikaweka simu pembeni nikaenda kwanza kuoga kisha nirudi kuifuatilia ile namba sasa wakati natoka bafuni ghafla aisee nyieee hamuwezi amini nilichokiona mbele ya macho yangu🥺😳🥵

Itaendeleaaaaaa

KWETU morogoro.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

NILIZANI MWIZI KUMBE MMMM💘💐💘 SEHEMU YA (09__10)  >>> https://gonga94.com/semajambo/nilizani-mwizi-kumbe-mmmm-sehemu-ya-09__10
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 11.

majario rewards 100 Comments 0
 

GIGY MONEY DAH😭

majario rewards 100 Comments 0
 

YOUNG AFRICANS,

majario rewards 100 Comments 0
 

BAKORA VILLAGE

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 7...8

majario rewards 100 Comments 0
 

HUYU KAKA EPISODE 2

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE...5...6

majario rewards 100 Comments 0
 

BABAMKWE epsd 3...4

majario rewards 100 Comments 0
 

HUYU KAKA 1

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈21

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈20

majario rewards 100 Comments 0
 

DADA WA KAZI EPISODE 8

majario rewards 100 Comments 0
 

DADA WA KAZI EPISODE 7

majario rewards 100 Comments 0
 

Life in a Year (2020)

majario rewards 100 Comments 0
 

Kenya, Tanzania, Congo

majario rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY 40

majario rewards 100 Comments 0
 

POSHY QUEEN:

majario rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY 39

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈19

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈18

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈17

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH 💋🙈16

majario rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈15

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 05 ❤❤.

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 04 ❤❤.

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 03 ❤❤.

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 02 ❤❤.

majario rewards 100 Comments 0
 

HAIZIMI 01 ❤❤.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

NIPE YOTE DADY 34

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈14

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈13

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DAAAAAAAH💋🙈10

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

TUWASHUKURU KINA BABA

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest