"Sihitaji kuelewa lolote lile naomba ufate ninachosema,na wala sitaki maelezo yoyote mimi nimeshakuozesha ,na nilishakuambia mara nyingi siku yoyote nikikukuta umesimama na mwanaume kihasara hasara sitotaka mambo mengi,ndo nitawafungisha mimi mwenyewe....hivyo huyu ni mumeo atapoenda basi utaenda nae, nyumbani utakuja kutembea,nimemaliza"
Niliyakumbuka maneno ya baba yangu aliyoyasema siku nne zilizopita,maneno ambayo yaliumiza moyo wangu,nikajiona sina thamani kwa wazazi wangu,au wamenichukuliaje mimi mpaka kufikia kuniozesha ndoa ya mkeka...!?🤦🏼♀️ Kwamba sijatulia sana au? Mbona najiheshimu mimi,sina kesi za ajabu ajabu....sijihusishi na mapenzi.....yaani licha ya kutojihusisha na habari za ajabu ajabu leo hii ndio wa kuniozesha ndoa ya mkeka😭😭😭na mwanaume ambaye sina mahusiano nae wala ukaribu nae,zaidi tu namuona mara chache sana akija kijinini kwetu kusalimia ndugu zake ambao walikuwa majirani zetu...ambao mzee wa huo mji yeye alikuwa alikuwa anamuita mjomba ...kwahiyo kitendo cha mimi kusimama nae kumsikiliza anataka niambia nini ndio kwamba najihusisha nae kwenye mahusiano...!? Babangu mbona anatanguliza ukali na ubepari kwenye kitu hamna.....!!!!🤦🏼♀️niliumia sana yaani ndo ndoa gani haina tarumbeta🎺🎷mdundiko 🥁wala muziki🎤🎼hata sare hamna.....yaani ndoa chukuchuku haijadamshi kabisaa 😁😁😁
Nikiwa naendelea kuwazua nilishtuliwa na sauti ya mwanaume aliyekuwa pembeni yangu ambaye ndio mume wangu eti anaitwa Hakim🤦🏼♀️🤦🏼♀️🤦🏼♀️ akiniambia kuwa tumefika mwisho wa safari yetu....Safari ambayo ilikomea stendi kuu ya mabasi ubungo jijini dar es salaam kutokea Tanga, ilinibidi niwe makini nisije potezana nae🙌japokuwa mimi ni mjeuri na kiburi sana😁😁😁......afu nina nyodo plus naringa lakini kwenye miji ya watu sitaki kuleta mbwembwe 🙆🏻♀️🙆🏻♀️🙆🏻♀️nikipotea jee...!🤦🏼♀️hivyo nilikuwa mtii sana kwake tunashuka na kupanda kwenye tax aliyokodi kutufikisha nyumbani,wakati huo mimi niko zangu kimya wala sina stori nae😒😏hapo nasema nitakunyoosha wewe mpaka ujute kukubali kunioa😒😒😒 huwezi kunioa kizembe halafu nikuchekee🌝👌mbona na nyiee mtashuhudia tu😁😁😁
Halafu kumbe sijajitambulisha mnataka mnijue?🙄na hamsemi...!!!🙄buana mimi kwa jina natambulika kama Kulthum mzaliwa wa Tanga.....nina miaka kumi na tisa,elimu yangu nimeishia kidato cha nne🤪nilipata zangu pass sijui ya mkaa sijui ya umeme ile...yaani nilifeli msijifanye hamjaelewi🙄🤣nyiee kusoma tuwaachie wenye vichwa vyao vya kusoma jamani😅mimi nilifanya kuwasindikiza tu kusema ukweli,vingi sana nilikuwa sielewi 😁😁mfano wa karibu ni hili somo la namba🤣 nilikuwa naambulia maksi 15% yaani hapo ndo nimejitahidi mno 🤣🤣🤣yaani kifupi mimi na somo hili la namba tulipeana mkono wa kwaheri pale herufi nazo zilivyoamua kujiingiza mara sijui tafuta thamani ya x mara sijui xy zimefanyaje😒😒😒 kwanza somo linabadilika badilika majina wewe huogopi....!? Mara hesabu...mara hisabati mara mathematics 🙌🙌🙌 ila nilikuwa bingwa sana wa kuimbisha "dereva tumwage"🤣🤣👐 tukiwa tunaenda safari ya kimasomo🙆🏻♀️🙆🏻♀️tuishie hapo jamani kuhusu CV yangu hiyo😁 nisije toa siri zangu zingine bure miyeee👐
Mimi kwetu tumezaliwa wanne namimi ndio msichana pekee kwetu tena last born🤭wenzangu wote watatu ni wa kiume,Salum,Halid na Mustafa 🥱🥱 baba yangu ni mkali mno inahitaji moyo kumzoea🤦🏼♀️ila ndio nilishamzoea kwakweli ana sheria kali mno, licha ya ukali wake ambao hauzoeleki hii ya kuniozesha ndio alinivunja vunja moyo😢😢🥲 yaani jamani hata hajali mwanae nitaenda ishi maisha yapi huko na huyo Hakim dah.....!🤦🏼♀️🤦🏼♀️🤦🏼♀️
Ila sina jinsi ndo nishaolewa hivyo,na hata nyumbani nishatoka sasa niko dar es salaam kutumikia ndoa wajamen🙌🙌🙌Basi bhana usafiri ule wa tax ulitufikisha kwenye nyumba moja ya kifahari, nikabaki kushangaa shangaa🙄🙄🙄
"Tumeshafika,shuka sasa tuingie ndani"Hakim aliniambia
"Sawa" nilishuka,nae akashuka na kulipia hela ya usafiri akabonyeza switch pale nje ya geti ikapiga kengele humo ndani ikiashiria kuwa kuna mtu anapiga hodi
Akatoka mkaka mmoja na kutukaribisha,akapokea mizigo....mimi sikuwa na mzigo mkubwa ni kibegi kidogo tu sasa nibebelee minguo,miviatu au mibegi kwa raha gani....!?😒😒😒kwanza Hakim Alisema ataenda ninunulia👌👌 tukaingia hadi ndani,tukafikia sebuleni mimi nilikaa sofa moja,Hakim akakaa lingine....yule kaka alotupokea alipeleka mizigo yetu sijui ndo chumbani
"Kulthum,karibu hapa ndio nyumbani kwangu" Hakim alianza niongelesha
"Asante" nilimjibu kifupi tu🌝sipendi kuwa pale,ila baba yangu🥲amejua kunikomesha,mara kidogo yule kaka akarudi pale sebuleni na kutuambia
"Jamani,nishaandaa chakula kwa ajili yenu ,hivyo karibuni mezani"
"Ok,asante tunashukuru" Hakim alijibu
"Sawa,mimi niko nje"
"Poa poa....but huyu anaitwa Kulthum ni mwanafamilia wetu mpya"
"Karibu sana Kulthum,mimi naitwa Joel"
"Ahsante''
"Sawa,mimi niko nje"
"Okay" Joel akaondoka
"Kulthum najua umechoka sana,hivyo twende ukapate chakula kisha upumzike"
"Mimi nimeshiba"
"Umeshiba ni wapi umekula mama?"🙄
"Sijisikii kula,nataka kuoga"
"Sawa, twende nikuonyeshe bathroom,kisha tutakula"
Alinyanyuka nami nikamfuata nyuma🚶🏻🚶🏼♀️mpaka chumbani
"Hiki chumba cha nani...!?"nilimuuliza
"Cha kwangu"
"Sasa kwanini yule kaka ameingia?"
"Huwa anaingia,ameshazoea..... ni mfanyakazi wangu lakini tunaishi kama ndugu hivyo kazoe,pia kuna mlinzi huwa anakuja jioni asubuhi anaondoka "
"Ndio aingie chumbani kwako?" Nyieee,mgeni ndio nimefika leo halafu nataka nipangie watu maisha 🤣🤣🤣
"Sorry,kwa wakati huo tukiwa tunaishi wenyewe kwa sasa hatoingia"
"Sawa,nataka kuoga sasa"
Alinionyesha bafu na yeye kutoka,nikasema hivi huyu si simpendi na sijamridhia inabidi nisilale naye chumba kimoja🖖sitaki aniguse kabisa 👐👐👐anipe chumba kingine tu hapa nioge halafu nimwambie maana nyumba ni kubwa tu nipewe chumba changu🤣🤣🤣👌
ITAENDELEA
Chuma ndio kimeanza🔥🔥🔥tukutane sehemu ya pili🔥🔥🔥🔥🔥
FULL STORY UNAIPATA KWA KULIPIA TSH 1000
NAMBA YANGU YA WHATSAPP NA KULIPIA PIA NI 0715906120 MTANDAO YAS JINA LA USAJILI FLORA.