ENDELEA.......
"Una mpazia sauti CEO wa Kampuni ya DreamCloud au unanipazia Mimi!" Victor aliuliza.
"CEO ndio ana kibali cha kuchafua mazingira kwenye hii dunia!.... fanyeni kunipisha tu" Anjeli aliongea.
"Tuondoke!" Osman aliondoka, si mtu wa kupenda kelele.
Victor alianza kulalamika lakini jicho moja la Osman lilimtuliza.
Asha aliondoa gari, ndipo anashtuka kama viatu vyake vinatope.
Aliamua kukausha, kwa sababu kama angekiri kuwa yeye ndio kachafua nyumba basi Victor angezungumza mpaka kesho asubuhi.
Siku zote huwa wanashindana kuonekana bora kwa Osman.
Upande wa Sabrina anatoka chumbani kwake akiwa na nguvu mpya, hakuwa akikumbuka kuhusu tukio la jana.
"Nitafurahi kama Wageni wa hii nyumba watashindwa kutofautisha kati ya Mfanyakazi na Boss, naomba baada ya kumaliza kazi zako uende saluni....kadiri utakavyo onekana kuwa na muonekano mbaya kwangu ndivyo nitazidi kupunguza mshahara wako" Sabrina aliongea.
"Sawa... nitajitahidi kupendeza" Anjeli aliongea kisha akatoka nje kumwagilia maua.
"Baada ya kumaliza kumwagilia maua naomba unisaidie kufua hizi nguo, tafadhali sana naomba nguo zangu zisifuliwe na mashine" Hilda aliongea kisha akaweka kapu la nguo chini.
Anjeli alimwagilia maua chapu chapu, baada ya kumaliza alichukua nguo afue.
"Nguo zote za hii nyumba hufuliwa kwenye mashine, ni marufuku Mfanyakazi wa ndani kutumia mikono yake kufua pengine kama ni adhabu, peleka hizo nguo kwenye mashine" Sabrina aliongea baada ya kumfuma Anjeli akifua.
"Lakini Hilda kasema nguo zake huwa hazifuliwi kwenye mashine...." Anjeli aliongea.
"Ziache hapo atafua mwenyewe....jiandae tunaenda saluni" Sabrina aliongea kisha akarudi ndani.
Baada ya Anjeli kumaliza kazi yake aliondoka na Sabrina.
Hilda anashangaa kuona nguo zake zipo chini.
Aliachia tabasamu baada ya kuelewa kwanini ziko hapa. Aliziweka kwenye mashine akaanza kufua.
Upande wa Anjeli akiwa saluni alipendeza sana, Sabrina aliachia tabasamu baada ya kuona Mfanyakazi wake kawa katika muonekano mzuri.
"Twende ofisini kwa Osman nahitaji upafahamu, kuna muda huwa napenda Kijana wangu ale chakula changu ni jukumu la Mfanyakazi kumpelekea chakula" Sabrina aliongea.
Anjeli alitaka kusema analifahamu Kampuni la Osman lilipo lakini alijizuia.
Wafanyakazi wote walikuwa wanamtazama Anjeli kwa namna alivyopendeza, Sabrina alizidi kutabasamu.
Osman akiwa ofisini na Asha alishangazwa na ujio wa Mama yake, hakuwa akimtambua Anjeli kutokana na alivyopendeza.
"Nimemleta Anjeli hapa alifahamu eneo lako la kazi....Asha naomba umtembeze kila sehemu" Sabrina aliongea.
Asha aliongoza njia akiwa haelewi maana ya yote haya.
Machoni kwa watu Anjeli alionekana kama boss na Asha kama Kijakazi.
Alimpeleka mputa mputa kiasi kwamba Anjeli alitoka jasho.
"Hili ndio eneo lote la Kampuni ya DreamCloud....naikumbuka vizuri sana sura yako, naomba kujua kwanini ile siku ulikuwa unapiga mnada nguo za Osman" Asha aliuliza.
"Ni vyema kama utamuuliza Boss wako kwanini nguo zake zilikuwa zinauzwa..." Anjeli aliongea.
Asha aliachia tabasamu kimtindo baada ya kugundua binti huyu ni jeuri.
Alimtazama vizuri macho yake aliweza kuziona chembe chembe za udada poa, alivuka mpaka kwa kumvutia tisheti yako.
Tattoo ya nyota ndogo ilionekana kifuani kwake.
"Bila shaka ulikuwa ni Dada poa wa usiku mmoja kwa Osman.." Asha aliongea kisha akamtengenezea tisheti yake.
Anjeli si mtu wa kupenda vurugu, mara nyingi hujitahidi kuwa mlokole hasa majira ya mchana.
Alimshukuru Asha kwa kumuonesha mazingira kisha akaondoka.
"Kwanini Sabrina karuhusu msichana mzuri kama huyu kuwa Mfanyakazi katika nyumba yake!" Asha alijiuliza asipate majibu.
Anjeli anaingia ofisini kwa Osman kwa mara nyingine tena.
"Nadhani umeoneshwa kila mahali tunaweza kuondoka sasa...." Sabrina aliongea.
Anjeli alitikisa kichwa kuashiria ndiyo, macho yake na ya Osman yaligongana kuna namna walikosa hewa.
Sabrina hakuelewa kwanini wawili hawa wana babaika.....alimtaka Anjeli waondoke.
"Muache kuna mzigo upo supermarket nitaenda kuuchukua kisha atakuletea" Osman alijikuta akiongea.
"Sure!.." Sabrina aliongea kisha akaondoka.
Osman alijikuta akisimama baada ya kuhakiki mlango umefungwa, tamaa ya kumbusu Anjeli hata kidogo tu ilikuwa juu sana..............STORY TAMU SANA HII๐ UNAKOSAJE KWA MFANO........FULL STORY 1000 TU.
NAMBA YA MALIPO 0743770612 JINA JOFREY.
UKISHALIPIA NICHEKI WHATSAPP KWA NAMBA HII 0683009150..