Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

KAFARA YA CORODANI ZANGU Episode: 04

27th Jul, 2025 Views 34


Mtunzi: @★abuu_lion
№0685086201

Baada ya kusikiliza kisa cha yule dada chote kifupi, nafsi iliniuma sana. Nilimpatia shilingi 30,000 ambayo nilikuwa nimeifanyia kibarua cha kuvuna alizeti kwa siku 4. Hivyo niliona nimpatie yule dada, kisha nikaondoka naye mpaka nyumbani kwetu. Nilimsihi asiwe na wasiwasi kwani siwezi kusema kuwa alitaka kumtupa mtoto—hiyo itakuwa siri kati ya mimi na yeye.

Nyumbani naishi na bibi na babu kizaa mama, hivyo ni ukoo mkubwa na tuko wengi kidogo.

Baada ya kufika nyumbani, tuliingia ndani na yule dada. Nilmkaribisha kwa tabasamu, kisha mama mzazi akanitoa nje faragha kwa ajili ya kujadili.

"Hashim mwanangu, huyu binti ni nani na anatokea wapi? Na kwanini upo naye?" Aliniuliza mama mzazi.

Nilicheka na kusema, "Mama umeuliza maswali mengi sana. Iko hivi, huyu binti ni rafiki yangu sana, nimesoma naye, ila alikuwa amesafiri. Hivyo kipindi anarudi, ndiyo akaona apitie kwa rafiki yake. Kwani kuna tatizo mama?"

Mama akaweka alama ya tabasamu usoni kwake na kusema, "Ok sawa, mimi nilitaka kujua tu yeye ni nani, maana watoto wa siku hizi hamkawii kuzalisha nje bila sisi wazazi kujua."

Mimi: "Sasa mama nizalishe nje na nisikupe taarifa, wakati wewe ndiye msaada wangu? Siwezi bana, haha!"

Mama: "Haya sawa mwanangu, lakini marafiki zako wote huwa unanitambulisha, mbona huyu hujanitambulisha?"

Mmh... niliona kama mama anataka kustukia mchongo, nikageuza maneno na kusema, "Aaah mama, sio wote naweza kukutambulisha mamy."

Mama: "Ok, lakini kuna taarifa hapa imekuja mwanangu—yale maombi yako sasa yametimia."

Nilikaza macho na kumtazama mama huku nikiweka alama ya mshangao. "Taarifa gani hiyo kwanza?"

Mama akaendelea kwa kusema, "Dada yako MERIDA amefanikiwa kufungua duka la nguo za kike, na hana mtu wa kumuuzia. Hivyo amekuteua wewe Hashim. Unatakiwa uende mjini. Hivyo mwanangu nakusihi sana, maana ulikuwa ukililia kazi sasa umepata. Hakikisha unakuwa makini kazini, achana na (uhuni) wa mjini, makundi ya walevi na wavuta bangi. Sihitaji hivyo mimi kama mama yako. Nakuonya."

Hapo tupo nyuma ya nyumba yetu kubwa, mama akiwa anazidi kunipa kama maagizo ya jinsi ya kwenda kuishi huko mjini. Ghafla tunasikia kelele huko ndani tulikomwacha yule dada mgeni niliekuja nae aliyetaka kumtupa mtoto wake. Mmmh... ni kama mtu alikuwa anapiga kelele ghafla, naona watu wanakimbia kutoka nje.

Nilirudi mbio ndani kujua nini kimejiri. Heee! Nilipofika ndani aisee sikuamini nilichokiona! Yule dada niliekujanae nyumbani alikuwa ametapakaa damu mwili mzima, tena akiwa amejing'ata mkono wake mwenyewe, huku akiwa amejichana mkono wake wa kulia kwa meno na akiwa anakunywa damu zake mwenyewe. Kheee aisee! Muda huo mtoto yupo chini analia, huku amekandamizwa na miguu....................

Itaendelea...

Usisahau kulike na kutoa maoni, asanteni..
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

KAFARA YA CORODANI ZANGU Episode: 04  >>> https://gonga94.com/semajambo/kafara-ya-corodani-zangu-episode-04
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

SEHEMU YA 32💘💘

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

majario rewards 100 Comments 0
 

SEHEMU YA 30💘💘

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest