Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

MJEDA TARATIBU BASI* *SSEHEMUYA 7 mpk 10

27th Jul, 2025 Views 53



Tulivyoshuka tu mbele yetu, tukamkuta, baba Sophia na Saphina, alikuja kunipa barua ya kazi niliomba kazi ya ualimu shule binafsi, kupitia baba Sophia mkoa wa Kilimanjaro, tulipata kazi Mimi na Sophia, Saphina yeye alisomea unesi, sisi ualimu wa shule ya msingi, na Mungu kawa upande wetu, tumepata kazi shule Moja...

Sikuwa na simu ya kueleweka kile kisimu changu kilizima toka juzi, nimepigiwa simu, hawakunipata, hii kwetu ilikuwa habari njema, japo huzuni kukaa mbali na familia sijazoea, hili swala mwanzo mjomba alikuwa ameshalipinga lakini kutokana na matatizo yaliyotokea aliona bora niende mbali watakuwa wanakuja kuniona...

Ilibidi shangazi apewe mkanda mzima, muda huo nilikuwa chumbani, sikuwa tena mtu wakucheka kama mwanzo, alivyosimuliwa tu, ata hakuweza kuvumilia hajazima hapo hapo, tukiwa tunatoka kumrudisha hosptal...

Mjeda akafika mbele yetu, aisee binamu zangu walishindwa kuvumilia, wakataka kumvaa mjomba akawazuia na kusema, " kijana naomba utoke nyumbani kwangu mara moja uliyoyatenda yanatosha...

Mzee naelewa, sijaja kwa ugomvi, nimekuja kuwaomba radhi, ukweli sikukusudia ni hasira tu, nimekaa nimetafakari nikaona nimefanya kosa kubwa sana, Mimi hata sikutaka kusikia chochote nilimwambia Isa, anisaidie tumuwahushe mama, wanao sikiliza huyo shetani, wabaki Ili afanye mauaji kabisa, niliongea huku nasaidiana na Isa...

Binamu zangu wakubwa, walikuwa wakimtizama Kwa chuki mbaya mno, wakati tunahangaika ety akaja kunizuia, aisee nilimuweka ngumi ya tumbo, lakini kwake ata haikuwa na nguvu aliushika tu mkono wangu, huku ananitizama...

Toka nijitambue sijawai kuomba msamaa kwa yeyote, ila Kwa sababu yako, LLleo niko hapa kuomba msamaa usinipuuze, Isa hasira ilimpanda, akaokota jiwe akamtwanga nalo, aligeuka tu akamtizama, hakumrudishia kama anavyofanya siku zote...

Aligeukia familia nzima nakusema, kama kunipiga kutawapa furaha nipigeni, sitorudisha ata ngumu moja kwenu, Kila mtu alimpita tukapanda usafiri nakumuacha, kwangu ilikuwa maumivu makali,nilijikuta nakumbuka maumivu, na bado sijapona vizuli natembea kama ninavidonda katikati, najikaza tu kwa sababu ya shangazi...

Lakini kabla hata hatujaondoka, shangazi alipata fahamu alivyoniona tu, akanikumbatia huku analia, tulishuka kwenye usafili turudi tu ndani, bado mjeda alikuwa kasimama pale pale, na leo alikuwa na kofia kabisa ya kijeda, mama alijua moja kwa moja ndo muhusika, alimsogelea binamu Juma, akavuta kisu kutoka kwenye kiuo, Juma huwa anatembea na kisu muda wote na ndo kijana mkubwa...

Wakati mjomba ameshasoma akili ya mke wake, anakimbia kumuwahi, tayari shangazi alimkita kisu Cha mbavu mjeda,na alitaka hata kumuongeza kingine, ilibidi wamtoe shangazi kwanza na mjeda aliondoka uku anachechemea...

Tulikaa ndani Kwa hofu siku hio mimi na mama na Sophia tulikatiwa ticket tuondoke na binam Juma mpaka Moshi kituo changu Cha kazi, hatukuwa tumejiandaa ila Kwa hili tibwili lililotokea, pesa zilichangwa chap chap tukaondoka...

Wanaume wabaki Sasa kuendelea na msala uliotokea, tulisafiri kimya kimya mpaka moshi mjini, tulianzia Kwa shangazi yake Sophia, tulikaa Kwa siku tatu huku tukitafuta chumba cha kupanga tukashauliana tushee chumba Ili tuchangie kodi, kupunguza gharama...

Juma aliondoka kurudi nyumbani, tukabaki watatu Mimi mama na Sophia tuliamua kuchukua chumba na sebule self,tulianza maisha, Kila tukipiga nyumbani wanasema kuko shwari zilipita wiki mbili, tunatakiwa kulipot kazini...

Tayali nilikuwa nimeshapona ila moyoni bado nilikuwa naugulia,sikuwa tena natabasamu, ni mpaka nijilazimishe, shangazi alijitahidi kuniweka sawa..

Niligiza Niko sawa mbele yake Ili kumpa amani, mwanzo nilitamani kujiua, ila nilivyoona Hali ya shang'azi nikaogopa anaweza kufa, alionesha upendo wake kwangu Kwa ukubwa sana, kuliko hata mjomba wangu alieshare ziwa na mama...

Niliona naweza kusababisha binamu zangu wakawa yatima kama Mimi, tena ila Mimi nimepata upendo mkubwa utazani Niko na wazazi wangu, vipi kuhusu wao, watapata wapi mlezi bola, niliamua kujikaza nisogeze tu siku...

Upande wa nyumbani, mjomba alisubili timbwili wapi, wakahisi huu ni mtego, tukisahau waje kulipiza, Kila mtu aliwaza lake kichwani mwake, upande wa mjeda alikuwa anauguza jeraha lake, halikuwa kubwa sana kisu hakikupenya sana, alikuwa kashaanza mpaka mazoezi...

Aliwaza arudi tena, nafsi yake ilikuwa iki muuma mno, na kile alichokifanya kilikuwa kikimrudia Kila siku, na kutengeneza hisia zaidi...

Hakumshilikisha hata rafiki yake wa karibu,alipambana na janga lake mwenyewe, alifunga safari mpaka nyumbani, watu walikuwa waamesambaa hata Juma na Hussein, binamu zangu wakubwa walikuwa wameshaondoka kurudi makazini kwao...

Alifika nyumbani akakuta watu wote wako ndani, akagonga mlango....

Itaendelea...��

*SEHEMU YA NANE*

Ibu wetu akatoka kukaribisha mgeni, alivyofungua tu, akakuta ni mjeda, hakusubili kuambuwa funga, akaamua kufunga ila mjeda akamuwahi, na kuzuia mlango, dogo najua unahasira sana na Mimi, ila naomba uniache niingie tuweke sawa hili, sisi wote ni binadamu...

Lakini Ibu hakutaka kumuelewa, pamoja na mdomo wake lakini alijizuia Ili asilete balaa tena, mjeda akamchana ivi unatambua kama wewe ndio hasira yangu, kupanda zaidi, ulikuwa ukiwasimulia nini watu pale pembeni ya uwanja...

Hapo hata Ibu, aliishiwa nguvu, nakujihisi hatia sana, usijilaumu ni kosa kwangu zaidi kutumia hasira Kwa mtu ambae hahusiki na kusambaza maneno, nilishindwa kujizuia mimi ndie mwenye makosa zaidi...

Nahitaji muelewe, tuweze kuyamaliza haya, aliongea huku akiingia ndani, alivyoingia tu watu wote sebureni wakasimama, " umefuata nini wewe Ibilisi , sikia bro nahitaji tumalize tofauti zetu sote sisi tunamakosa, japokuwa yakwangu yamevuka mipaka, lakini hatuwezi kubadilisha chochote...

Kuliko tuendeleze uadui ni bora tumalize hili bifu, " kijana sisi hatuna shida na wewe, unaweza ukaenda familia yangu haitakusumbua, unaweza ukaenda sasa...

Samahani mzee najua umeongea, Ili tu niondoke hutamani kuniona mbele yako, naomba kuweka wazi jambo moja mzee, tayari sisi wote ni familia, sio vyema kuwekeana vinyongo, naomba uniruhusu nimuoe binti yako...

Hapo kila mtu alipandwa na hasira, japokuwa walizuiwa kuongea chochote lakini walishindwa, ivi we jamaa unajielewa kweli, baada ya kumdhalilisha dada yetu, unakuja kumsanifu, umuoe ili umgeuza ngoma...

Tena mwanangu, hujui tu dua ninayokuombea, itapendeza kama utakaa mbali na sisi, hasa dada yetu, unajua anapitia wakati gani mpaka dk hii? " Nimeshatambua kosa langu ndio maana niko hapa, simuoi kwa sababu yakusahihisha makosa yangu, naumia kwa sababu nampenda...

Ndio maana alipokosea kuingia eneo la jeshi, nilimuachia bila adhabu, kwa sababu tayari nilimuelewa, lengo la siku Ile ilikuwa tu kuwapa onyo lakini sio kwa njia ile, nilitaka tu kumvua nguo na kumwacha, Ili isijekujirudia kunichafua mtaani,....

Lakini kwa sababu tayari, nilikuwa na hisia nae, nilishindwa kujizuia, naomba mniruhusu niongee nae yeye mwenyewe kwa kina, kama kuna mtu anahitaji kunipiga hasila zimuishe, niko tayari, mjomba alimjibu tu kifupi...

Itaendelea...��

*SEHEMU YA TISA*

Kijana sisi hatuna tena shida na wewe, kwa amani tu naomba uondoke, binti yangu hahitaji kukuona wala kukusikia, Ibu akadakia, alisema ata harufu yake tu na manukato yake hataki kuyasikia, amepasua manukato ya kama Juma kisa tu yamefanana harufu na yake...

Mzee naelewa, ndio maana nimemuomba tu uniruhusu niongee nae, wakati unamvua nguo tena ndani kwangu uliniomba ruhusa, kijana najua unanguvu, lakini hapa ni kwangu, usinilazimishe kufanya ukatili, mpaka dunia ika simama kwa muda...

Alicheki chumba changu, tayari alikuwa anakijua, aliwapita kama mshale ata hawakujua imekuwaje, alifika nakufungua, aliingia alitegemea nipo lakini alikuta hewa, ata mabegi tu hakuna...

Alipata hofu, akarudi sebleni kwa mjomba huku amechanganyikiwa, anaongea kwa kupanic, " tafadhali sana mzee, nakuomba kwa heshima zote, na goti akapiga, naomba uniambie binti yako umempeleka wapi...

Nimekosea lakini hii sio adhabu sahihi kwangu, mzee nisaidie tafadhali, sitanii nampenda sana binti yako, nielewe tafadhali, mabinam walimchangia kumpiga, lakini hakuwarudishia alikuwa akiwaacha tu uku anaomba kuelekezwa wapi nilipo...

Upande wangu, nilipata shule nzuri watoto walinipenda sana ila kuna hicho kitoto cha darasa la kwanza, kilinipenda kupita kiasi, leo kilichelewa kuijiwa na hakukuwa na wakubaki na mtoto...

Ilibidi nipigie dereva wa familia yao, aje amchukulie kwangu, sio mbali na shule, mtoto kubaki peke yake na mlinzi sio sawa...

Tulielewana nikaenda na mtoto mpaka nyumbani, tulimkuta shangazi kashaandaa msosi, alifurahi mno kuona katoto tena kakike, basi walicheza , walilishana mtoto alionekana kufurahi mno...

Dereva alifika ila mtoto hataki kwenda kwao, kukakucha, na sisi humo tunagodoro moja tu, na tuko mtu tatu, afu kulala na mtoto haiwezekani, huenda wazazi wake wasituelewe...

Nilijaribu kuongea na mtoto, Amina mtoto mzuri, naomba unisikilize, leo nenda nyumbani kesho tena utakuja na Mimi hivi wazazi wako watachukia, watakuhamisha shule au kukuzuia kabisa kufika kwangu, madam hata usijali wazazi wangu mimi hawana shida, mama angu alishanikataa, Mimi ni nuksi kwake baba angu nae hajaoa tena, hajui ata kutongoza baba angu...

"Baba angu hayupo kasafili, niko na babu tu na anty Shadia, babu kila siku yuko bize hana muda na mimi, na ata anty Shadia, yuko bize na kazi za mule ndani, hawajali kuhusu mimi mpaka wanione, ndio wananiulizia, kufatilia niko sawa ama lah...

Nikifika nitaambiwa tu kulala basi, nilikaonea huruma kanavyolalamika, adi machozi, nilikambembeleza mpaka kakakubali, kalivyoondoka, nikaoga nikaingia kulala...

Upande wa nyumbani, waligoma kabisa kumpa mjeda maelekezo, ya wapi nilipo, aliondoka kwanza kapigika anangeo Kila mahali, rafiki yake, alishangaa na kumuuliza, ivi Mudy siku izi unashida Gani?..

Mbona hueleweki kila ukitoka unarudi na ngeo, kuwa muwazi tatizo nini?

Rama, kausha Kwa sasa, bado nashughulikia nikiwa tayari nitakujulisha ama nikihitaji msaada, Kwa Sasa naomba tu unipe muda, nina likizo ya mwezi mmoja , nahitaji kuweka sawa hili jambo kabla likizo yangu haijaisha...

Itaendelea...��

*SEHEMU YA KUMI*

Duh fresh mwanangu, lakini uwe makini sana, unaonekana kabisa hauko sawa, “usijali bro, kila siku mjeda alikuwa anaenda nyumbani kusumbua, ajue wapi nilipo lakini hakubahatika kupata chochote, upande wangu Mimi niliendelea na mawazo yangu nikiwa mwenyewe nalia kweli, nikiwa nawatu najikaza kuchangamka…

Shangazi, aliamini sasa niko sawa, akafunga safari kurudi kwake, tukabaki mimi na Sophia, Amina alinipenda kupita kiasi ilifika hatua, nikawa naongea na babu yake anamruhusu kulala kwangu..

Alinichukulia kama mama ake mzazi, alinipenda sana, tulipiga picha za pamoja mama na mwana, ata DARASANI nilimfanya apende kusoma na kujitahidi, alianza kufanya vizuli sana, mpaka wengine wakahisi nimempendelea…

Alipewa mtihani tena binafsi, na alifanya vizuli zaidi hata ya mwanzo, na walikuwa wamemsimamia kabisa, mtihani mzima, aliwashangaza sana, akuwahi Kuwa kwenye ten bora Toka aanze shule hapo, sasa kawa wa tatu, hii ilifanya babu na baba wa binti wanitafute kunishukuru…

Huku wakiniahidi zawadi, na kwenye simu, miamala iliingia, tena iliyoshiba, nilifurahi mno babu alitumia laki 8, nilifurahi mno, siku hio hio na baba ake Amina akanitumia million 1, nyie nyie Yaani apa ni mishahara yangu ya miezi kadhaa, ety nimepata kwa siku moja…

Furaha niliyokuwa nayo haikuelezeka, niliamua kutoa kwanza sadaka kwa mayatima wenzangu, kisha nikaomba dua, Kwa ajili ya familia yangu na Mimi mwenyewe…

Nilivyomaliza nikamjaza Anty pesa ya matumizi afu mjomba nikampa pia, ila nyingi nilimpa shangazi, alifurahi uyo niliombea dua kibao…

Likizo hii niliwamiss sana ndugu zangu, lakini Sasa nikikumbuka Kuna shetani anaishi huko, ata nguvu za kwenda mkoani kwangu zinaisha, niliona kuliko kwenda kwenye matatizo ni heli nibaki zangu tu Moshi, Sophia , alisema yeye hawezi kubaki hajapazoea, ikabidi nibaki peke yangu…

Amina alihamia kwangu, uyu mtoto jamani alijua kunipenda, nilijikuta muda wa kuhuzunika nakuwa bize na Amina, tulielewana mno, mtoto alikuwa na akili kama mtu mzima, alinipa mpaka ushauli wa biashara na niliufanyia kazi, nikafungua frame ya ice cream na bites…

Na nilikuwa jirani kabisa na shuleni japokuwa ilikuwa likizo lakini bado niliuza,siku nne zilipita baba ake Amina alisema yuko Moshi anahitaji kumuona mwanae, uyu baba Amina hakuwa muongeaji kabisa…

Ni amenyoka kama rula, hana mazoea akipiga simu ni mtoto wake tu hana muda na story na mimi kabisa, zaidi ya vitendo vya miamala na shukrani za sms tu…

Tulimpa location make mtoto aligoma kwenda kabisa, muda huo ilikuwa saa 9 jioni, tukiwa pale ikaja gari moja kari, Mercedes Benz nyeusi, mimi nilikuwa kwa ndani naiona tu, nikajisemea moyoni duh hii gali gharama yake tu hata nikiuza figo zangu zote nautumbo wangu wote siwezi inunua, watu wanaishi dah…

Mtoto akatoka Kwa furaha anaijua ndiga ya baba ake, Mimi sikutaka ata kujitokeza, nishamsoma ni mtu hapendi mazoea, lakini Amina alimleta kunisalimia na alitaka tutoke wote, muda huo mimi nilikuwa nimeinama sina hili wala lile naweka vitu vyangu sana,kuja kugeuza hivi nilishtuka…
JE NINI KITAENDELEAAA!! "
OFAAAA KUPATA YOTE NI 1000 TU UNAPATA mpk mwisho kabisa

NAMBA YA MALIPO 0755090082 mpesa jina la usajili zainabu sungita mpesa

UKISHALIPIA NJO INBOX
WHATSAP 0755090082
WHATSAP 0766030082.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

MJEDA TARATIBU BASI* *SSEHEMUYA 7 mpk 10  >>> https://gonga94.com/semajambo/mjeda-taratibu-basi-ssehemuya-7-mpk-10
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
offa ya msimu wa nanenane
offa ya msimu wa nanenane

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

SEHEMU YA 32💘💘

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

majario rewards 100 Comments 0
 

SEHEMU YA 30💘💘

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest