Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Pyar Ho Jane Dushman

NIMEZAMA 01πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹

27th Jul, 2025 Views 5


Sikitu , sikitu ,sikitu....sauti ya mamdogo iliniamsha asubuhi na mapema ..niliamka nikiwa na usingizi sana nikajikuta kisha nikakaa kitandani.

Sikitu muda umekwenda niandae uwahi stend si unajua tayari umeshakatiwa tiketi gari itakuacha......sawa mamdogo .
Nilijivuta kivivu nikatoka nje nikachukua ndoo nikachota maji katika kisima na kuelekea bafuni kuoga...nilioga chap kisha nikarudi ndani kuvaa.

Mamdogo bado alikuwa amekaa kitandani...fanya haraka ni saa kumina moja kasoro alfajiri una dakika chache tu za kuwahi gari vinginevyo utaachwa.

Nilijiandaaga Fasta nikamaliza kisha mamdogo akanivuta mkuku mkuku kutoka nje ili kuwahi stendi
Alijitwisha begi langu alimaarufu kama shangazi kaja huku mkononi akiwa ameshikilia mkungu mdogo wa ndizi.....mimi pia nilikua nimeshika dumu dogo la maji ya kunywa pamoja na kimfumo kidogo ambacho ndani yake kilikuwa na mihogo pamoja na ndizi zilizochemshwa vizuri na kachumbari kwaajili ya kula njiani.....tulitembelea haraka sana tukafika stendi.

Oooh asante Mungu gari bado ipo mamdogo alishusha pumzi na kutua begi chini....Sikitu mwanangu nenda ukafanye kilichokupeleka huko mjini una miaka 20 tu wewe bado mdogo usijichanganye ukifika huko kumbuka baba na mama yako walishafariki usipojipambania maisha yako hakuna atakaye kupambania...maneno ya mamdogo yaliingia mpaka kwenye ubongo wangu nikasema sawa mama sitakuangusha.

Abiria abiria gari inaondoka ingieni Fasta twendeni... Nilikimbilia kwenye gari huku mamdogo nae akipanda akiwa ananiaga huku akilia machozi...nitakukumbuka sana Sikitu...niliacha pia huku watu wakitushangaa...mama embu shuka tuondoke mnalialia nini bana ...ilikua ni sauti ya konda haraka mamdogo kushuka na kusogea dirishani nje ya gari akiwa ananipungia mkono....hatimaye safari ilianza kuelekea mjini ambako nilikuwa sijawahi kufika kabla......

ilitimia saa nne asubuhi ..... abiria jiandaeni tunaingia hotelini.....ilisikika sauti kubwa ndani ya gari....gari ilielekea hotelini kwaajili ya abiria kushuka na kupata chakula.....walishuka wooote mimi nilibaki ndani ya gari na kufungua mfuko wangu nikatoka ndizi mbili na mihogo miwili nikaanza kula ..... ..nikaangalia pembeni yangu alipokuwa amekaa jirani yangu alikua ameshuka kula na pale kwenye siti yake alikua ameacha camera kubwa pamoja na head phones nilishangaa tu kisha nikaendelea kula .....abiria walirudi na gari ikaondoka......ndani ya gari ilitanda harufu ya Chipsi nyama ambazo watu waliingia nazo baada ya kutoka hotelini.....nilijikaza maana ilitamanisha kiukweli. ......jirani yangu aliporudi alikua na mifuko miwili ya Chipsi alinisalimia ....habari dada ...salama shkamoo kaka......aaah usijali karibu chakula alinipatia mfuko mmoja ....wakati huo nilikua nimepakata ile mihogo yangu na ndizi mapajani... asante kaka nimeshiba .....okay basi chukua utupe nje πŸ™„πŸ™„ nilikodoa macho kwa aibu nilichukua ile mfuko na kuupakata .....Karibu.....yule kaka alinikaribisha......sikumjibu zaidi ya kutingisha kichwa ishara ya kukubali.........nilikula kwa pupa mpaka nikamaliza aisee zilikua tamu mno lkn nikachukua mihogo na ndizi zangu nilizokua nimepakua nikala na kumaliza kisha nikashushia na maji yangu hapo nikasinzia 😴😴 tulitembea mwendo mrefu sana nikiwa nimelala .........abiria jiandaeni tunaingia hotelini kupata lunch....ilikua ni saa nane mchana na gari ilisimama kisha watu wooote wakashuka....kama kawaida nilibaki kwenye gari na kufungua mfuko wangu kisha nikatoa mapande matatu ya mihogo pamoja na mapande matatu ya ndizi ...kabla ya kuanza kula nilinyanyua dumu langu dogo la maji kisha nikanywa na kunawa mikono nikaanza Kula........ Mara abiria wote wakarudi ndani ya gari ....jirani yangu pia akarudi na kuketi

ITAENDELEA

FULL STORY UNAIPATA KWA KULIPIA TSH 1000
NAMBA YANGU YA WHATSAPP NA KULIPIA PIA NI 0715906120 MTANDAO YAS JINA LA USAJILI FLORA.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

NIMEZAMA 01πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹πŸ’‹  >>> https://gonga94.com/semajambo/nimezama-01
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Pyar Ho Jane Dushman
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
offa ya msimu wa nanenane
offa ya msimu wa nanenane

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest