Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

ALIFIRISIKA BAADA YA KUMUACHA MKE ALIYECHUMA NAYE MALI | EP 07

27th Jul, 2025 Views 11



Kulia kwake aliamini kwamba ndiyo sehemu sahihi ambayo ingemfanya kupoza machungu kwa kile ambacho alikuwa anapitia πŸ’”. Wakati akiendelea kulia, aliona taxi nje ikisimama πŸš•.

Akili yake ilimwambia kwamba kulikuwa na mtu ambaye alishuka katika taxi ile. Alipiga hatua hadi kwenye geti na kufungua.
"Kaka, mbona kama ulikuwa unalia?" 😟
Sauti hilo halikuwa la mwingine bali ni Rasma, ambaye alikuwa mahala pale akitokea Dar es Salaam πŸ™οΈ.

Garma hakuwa na jinsi zaidi ya kumweleza ukweli dada yake kwa kile kilichotokea 😞. Ilikuwa ni sehemu ya masimulizi ambayo yalimuumiza Rasma. Alijikuta anapatwa na hasira 😑, akatupa mizigo chini na kutaka kuingia ndani, lakini kaka yake alimzuia.
"Muache, hata usimpige wala kumgomea," alisema Garma huku akiwa amemshikiria ndugu yake 🀲.

"Kaka, huyu mama unavyomchekea ndivyo anavyozidi kukuzoea! Anazidi kukuzoea na si kwamba hana akili? Sawa, mtu hampendi, ndiyo amuumize hata siku ya msiba jamani?" 😠
"Mama naamini ni mtu mzima, tena mtu mzima hasa, na anafahamu anachokifanya," 🧘
"Ujinga! Hebu ngoja bwana!" Rasma aling'aka na kujitoa mikononi mwa kaka yake kwa nguvu 😀.

Alipofanikiwa kuporonyoka, aliingia ndani na kumkuta mama yake akiwa amesimama karibu na mlango huku akimtazama πŸ‘€. Hasira zake zilimfanya amrushie maneno makali bila hata salamu 😠.

"Kwa hiyo hapo ndipo umefurahia? Una furaha sasa hivi si ndiyo? Hivi mama, hii roho utaiacha lini? Mbona unaniogopesha hadi kuzaa?" 😰
Rasma alikuwa akitetemeka mwili, mapigo ya moyo wake yalikuwa yakienda kasi, huku kijasho kikimtoka πŸ’¦.

Alimwangalia mama yake ambaye alikuwa amenywea. Ule upole na ubaridi ulikuwa kwa mwanamke yule ambaye alimweka tumboni kwa miezi tisa 🀰.
Wanasema kila shetani na mbuyu wake, mtu na mtuwe. Wembe ni mdogo lakini unakata nywele, lakini ukubwa wa shoka umeshindwa kukata nywele πŸͺ“βœ‚οΈ.

Mama Garma mbele ya Rasma hakuwa mzungumzaji. Pindi mwanawe huyu wa kike alipotoa neno, basi alikaa kimya 😢. Hakuwa mkali kama ilivyokuwa kwa Garma.
Hii ilitokana na sababu moja yenye kujigawa mara mbili:

Sababu yenyewe ni kwamba kujifungua kwa Rasma kulikuwa kwa njia ya upasuaji πŸ₯, hivyo alimchukulia mwanae kama yai πŸ₯š. Alimpenda mno kuanzia utotoni hadi anakuwa πŸ’–.
Kisiele kingine ni kuwa Rasma alikuwa wa mwisho, licha ya kuwa wa mwisho pia alikuwa ni mwanamke, hivyo mapenzi yalizidi mno kwa mtoto huyu πŸ‘§.

Kuzidisha kwa mapenzi yake kwa Rasma kulimsababisha ajikute anamsikiliza sana, anamwelewa, na muda mwingine hakutaka kumbishia wala kumjibu pindi aongeapo 🫒.
Hii ilifanya hata leo, anapogomewa kama mtoto, ashindwe kujibu lolote.

"Narudia tena, hii tabia unayoifanya hapa iwe mwanzo na mwisho. Mtoto amefariki kikawaida, lakini wewe unataka kuonyesha kama amekufa kwa kurogwa πŸ§™β€β™€οΈ. Nimechoshwa na tabia zako. Kama mtu humpendi, huna sababu ya kumfanyia vituko wala madhira ya kukera kama haya 😀. Muache aendelee kuishi. Chuki yako haitamfanya achukiwe na dunia nzima."
Alisema kisha aliingia zake chumbani ambako alimpoza Mayner πŸ›Œ.

Kauli za Rasma zilipoza kelele zote za Mama Garma. Zilifanya nyumba ile itambulike kuwa kulikuwa na msiba na si muziki tena 🎼🚫.
Watu mbalimbali walikusanyika na taratibu za kufanya mazishi zilianza πŸ•―οΈ.

Hawakutaka kuchelewesha sana kutokana na maiti kuwa ya mtoto mchanga πŸ‘Ά, hivyo walihisi ingeharibika kwa haraka zaidi. Walipofanikiwa kuzika, maisha ya kawaida yalirudi.
Lakini kwa upande wa Mayner, alikuwa kama amechanganyikiwa πŸ˜΅β€πŸ’«.

Wiki mbili sasa, bado akili ya Mayner haikuwa sawa πŸ§ πŸ’”. Alikuwa mwanamke ambaye amechanganyikiwa. Amani katika maisha yake ilipotea kabisa πŸ•ŠοΈπŸš«.
Hakuna alichokuwa anazungumza zaidi ya kulia 😒.

Muda mwingi alikuwa akijifungia chumbani na kuangua kilio 😭. Alilia kuhusu mtoto wake, akizungumza neno moja tu:
"Mwanangu hajafa." πŸ’”

Watu mbalimbali walikuwa wakifika pale kumpa pole, lakini hakuacha kuwahadithia jinsi alivyokuwa amejifungua. Hakuwacha kuwalalamikia na kuwaambia jinsi gani Mungu alivyokuwa katili kwa kuchukua kiumbe chake πŸ˜žπŸ™.

Mayner aliichukia dunia 🌍🚫. Alitamani angalau impe muda wa kwenda kaburini kuzungumza na mtoto wake.
Muda wa kulala ulikuwa akiweka mdoli pembeni, basi ikifika usiku sana anajaribu kumnyonyesha maziwa ambayo yalikuwa yakitoka 🧸πŸ₯Ί.

Hii ilimuumiza sana Garma πŸ˜”. Kama mwanaume mwenye mapenzi ya dhati kwa mke wake πŸ’‘, alikuwa na wakati mgumu.
Kile ambacho alikuwa akipitia mke wake kilimfanya ajihisi kama mmoja wa watu wasiokuwa na thamani 😞.

Kwake, alimchukulia Mayner kama sehemu ya mwili wake πŸ«‚. Alimheshimu na kumpenda ❀️. Akampa moyo wake wote, akampa akili na afya pia.
Hivyo, kitendo cha kumuona akiwa hana furaha kilimnyima amani zaidi.

Alikuwa mtu ambaye akifika nyumbani, basi ataenda kuzungumza na mke wake huku machozi yakimtoka 😒. Baada ya hapo angerudi tena kufanya mazungumzo na dada yake.

Mazungumzo yao yalihusu namna ya kumweka sawa mpendwa wao πŸ—£οΈ.

"Nataka nifanye utaratibu wa kumweka sawa Mayner. Anateseka, halafu mimi sipendi awe katika hali hii 😞. Moyo wangu unaumia," alizungumza Garma huku akiwa amekaa katika gari kwenye eneo la maegesho 🚘, pembeni yake kulikuwa na ndugu yake.

Walikuwa katika kikao kidogo ambacho kwake alikiona ni cha muhimu. Kilikuwa cha muhimu kwa sababu alihitaji namna nzuri ya kumtibia mpenzi wake πŸ’•.

"Hapo naona suluhisho ni kumtafuta mtu wa saikolojia tu," Rasma alisema 🧠.
"Kwahiyo namtoa wapi? Najua anateseka, na vinginevyo anaweza kuwa chizi huyu. Mama naye amekuwa si mtu wa kujali," Garma alijibu kwa huzuni 😟.
"Mama unataka ajali vipi? Kama damu yake anakutukana kisa Mayner, atashindwa kumuacha Mayner mwenyewe. Mimi nitafanya utaratibu wa kumtafuta daktari," alisema Rasma.
"Bora iwe hivyo, nawe kama inawezekana hamia hapa kwangu basi," Garma alisisitiza.
"Sio jambo baya, nitafanya hivyo. Hakuna hata shida," Rasma alikubali 😊.

Wiki moja mbele, walifanikiwa kumpata daktari ambaye alikuwa ni mwanasaikolojia πŸ‘©β€βš•οΈ. Daktari huyu alifanya juu chini ili kumweka Mayner sawa.

Kwa uhodari wa hali ya juu, alitumia wiki moja kumjenga na kumuimarisha Mayner kiakili πŸ§˜β€β™€οΈ. Alimfanya awe mtu ambaye ameanza kurudisha matumaini, hata tabasamu kwake lilianza kurejea πŸ˜„.

Furaha katika nyumba ilirudi, tabasamu kwa kila mmoja lilirudi 😊. Lakini kwa upande wa mama yao bado alikuwa na kinyongo, huku akipanga mikakati zaidi ya kuhakikisha kwamba anafanikiwa kumuondoa Mayner katika nyumba ile πŸ˜’.

Pindi alipoweza kuzungumza na Ninah pamoja na mama yake, hakuacha kumwelezea hali ilivyo.

"Haha! Amekuwa kama chizi hivi. Akili yake imeruka. Sasa hivi kaweuka na bado hajaanza kunuka, ila siku si nyingi!" πŸ€ͺ
"Shoga haya mambo sijui hata umejifunzia wapi?" πŸ€·πŸ½β€β™€οΈ
"Wee! Nakosaje kuyajua mie? Nina udigo ndani yangu hata kama unaona nakandamiza maneno πŸ™„. Sipendagi mwanangu awe na wanawake wa ajabu ajabu. Mwanamke ukimtazama unatamani kutapika 🀒. Ninah ndiye anaendana na mtoto wangu, siyo yule!" aliendelea kujimwambafai 😀.

Hizi ndizo zilikuwa hoja na maongezi yao. Kila walipokutana, basi habari kuu ilikuwa ni kuhama kwa Mayner kwa kumtengenezea ugonjwa, huku wakiamini kuwa siku si nyingi zoezi hilo lingekamilika 🀐.

Nisingependa nikupangie bei katika kununua simulizi hii. Natamani kuona unanunua kwa bei yako mwenyewe. Pesa yako unaijua, matumizi yake siwezi kukupangia. Je, unataka kununua kwa Tsh ngapi? Njoo Whatsapp namba ni 0717255498..
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

ALIFIRISIKA BAADA YA KUMUACHA MKE ALIYECHUMA NAYE MALI | EP 07  >>> https://gonga94.com/semajambo/alifirisika-baada-ya-kumuacha-mke-aliyechuma-naye-mali-ep-07
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
offa ya msimu wa nanenane
offa ya msimu wa nanenane

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest