Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Pyar Ho Jane Dushman

ALIFIRISIKA BAADA YA KUACHANA NA MKE ALIYECHUMA NAYE MALI | EP 15

27th Jul, 2025 Views 3



Baada ya kuondoka kwa kina Rasma pale nyumbani, nyumba ilitulia kidogo, vurugu zilipotea kabisa. Walibaki watu wawili tuโ€”Mama na mtoto wakeโ€”wakiwa sebuleni, kila mmoja akimtazama mwenzake ๐Ÿ‘€.

Garma hakuwahi kufikiria kwamba kumpoteza Mayner kungekuwa na athari kubwa kiasi hicho, lakini alihisi ametimiza wajibu wake.
Kwake, hakupenda kudharauliwa. Kitendo cha Mayner kwenda kwa mganga, ilhali tayari alikuwa amemkataza, kilimvunja moyo na kumvunjia heshima ๐Ÿ˜ค. Kama mwanaume, alihisi inampasa kuonyesha kuwa yeye ni nani.

Mama yake alimtazama kwa sekunde kadhaa, kisha akasogea hadi alipokuwa na kusema:
"Usijali, kila kitu kitaenda sawa. Yule hakuwa mwanamke wa maana wa kusema unataka kumuo..."
Kabla hajamalizia, aliona kitu kama chupa chini ya meza ๐Ÿ˜ณ.

Akasita kuzungumza, kisha akainama na kuichukua ile chupa.
"Si umeona? Umeona huu ni uchawi wake. Wale wanga haki tena!" alisema huku akimkabidhi chupa hiyo kwa mtoto wake.

Chupa hii ilikuwa ile ile aliyopewa Rasma na mganga, sehemu ya dawa. Kwa bahati mbaya, wakati wa ugomvi wa Mayner na kaka yake, Rasma aliidondosha bila kujua ๐Ÿ˜“.

Mama alidhani ni dawa ya Mayner.
"Nimepata nywele yake na hii dawa... mbona namkaanga mchana kweupe! Huyu lazima awe chizi! Haiwezekani aniabishe kiasi hiki," alijisemea moyoni.

"Kwahiyo ni nini sasa?" Garma akauliza.
"Ukisikia libwata ndio hili! Huu ni uchawi mbaya sana. Hapa kama ungerogwa, kila kitu ungemuandikisha yule mpuuzi!" ๐Ÿคฌ

"Mh! Bora Mama umeniokoa aisee. Ubarikiwe sana, Mama. Ndiyo maana nakupenda. Ngoja niivunje kabisa!" Garma alisema huku akinyanyua chupa hiyo.

Mama yake akamzuia haraka.
"Hapana! Naomba usivunje. Itakuwa kama ushahidi. Nikae nayo mimi hapa."
"Sawa," alisema Garma na kukabidhi chupa hiyo. Kisha alianza kuondoka kuelekea chumbani. Lakini alipopiga hatua nne, alikumbuka jambo ๐Ÿค”.

"Mama, yule mwanamke ameolewa?"
"Yupi?"
"Yule uliyemleta, Ninnah."
"Aolewe wapi? Bado anakusubiri tu."
"Basi kesho tutaongea vizuri, na kama ikiwezekana tutaenda kwake."
"Sawa, hakuna shida," Mama Garma alitikia, akimtazama mwanawe akiondoka kwa bashasha ๐Ÿ˜Œ.

Ndani ya moyo wake, kulikuwa na furaha isiyoelezeka ๐Ÿ’ƒ. Alifurahia kwamba amefanikisha kumtoa Mayner pale nyumbani na kupata nywele pamoja na dawa aliyokuwa amepewa Rasma na mganga.

Furaha iliongezeka alipoona mtoto wake ameanza kumuulizia Ninnah ๐Ÿ˜.
"Hapa sasa mambo yamekaa sawa! Ndoa muda si mrefu, ebu ngoja..." alisema kwa sauti ya chini na kuelekea chumbani kwake.

Alipofika chumbani, hakupoteza muda. Alipiga simu kwa Ninnah kumpa taarifa.
"Mama kuna nini?" aliuliza Ninnah kwa sauti ya kushtuka.
"Umejiunga na kifurushi cha ndoa yako!" Mama Garma alisema kwa tabasamu pana ๐Ÿ˜‚.

"Mama jamani! Hapo unazungumza kama huduma kwa wateja! Hebu niambie, kuna nini kinaendelea?"
"Kapigwa! Katiwa mateke na kafukuzwa kama mbwa!" ๐Ÿ˜†
"Weeee! Usiniambie!"
"Kakwenda na aibu! Mabegi juu juu. Sijui kaenda wapi ila kesho tutakuja kwenu."
"Kunini tena?"
"Wewe naye! Kuna kingine zaidi ya ndoa?" ๐Ÿ˜

Ninnah akashikwa na butwaa.
"Mama, nina furaha sana! โค๏ธ Moyo wangu una amani! Nakupenda sana! Mwaaah! Mwaaah! Mwaaah!" ๐Ÿ˜˜
"Hahaha! Sawa mwaya, ngoja nimkaange mtu hapa. Nitakutafuta kesho nikiamka," Mama Garma alimalizia na kukata simu.

Akapiga magoti uvunguni mwa kitanda, akatoa ukaango mdogo uliokuwa na maji meusi sana. Aliweka kidole, maji yakapotea kama kwa uchawi ๐Ÿ˜ฎ. Akaweka nywele aliyoitoa katika khanga, akaichanganya na dawa, kisha akajisaidia mkojo humo ๐Ÿ˜ณ.
"Kesho nitadili naye," alijisemea huku akijifuta mikono.

---

Asubuhi ilipofika, pirika pirika zilianza. Kwa upande wa Garma, aliamua kuvunja ratiba zote ili kwenda kwa kina Ninnah kufanya mazungumzo.

Akiwa kitandani, alijiangalia:
"Mwanamke angeniua huyu! Kumbe ni mchawi hivi?" alijisemea na kwenda kuchagua nguo ya kuvaa ๐Ÿ‘”.

Baada ya masaa mawili, wote walikuwa tayari na waliondoka nyumbani. Dakika 45 baadaye, walifika kwa kina Ninnah. Ninnah aliwapokea kwa upendo wa dhati na tabasamu la furaha ๐Ÿ˜Š.

"Sidhani kama Mama hajakuambia kila kitu?" Garma akauliza.
"Mama ataongea na Mama, lakini mimi bado. Kuna nini?" aliuliza Ninnah.

Mama Garma akaamua kueleza kila kituโ€”kuanzia sababu ya ugomvi, mpango wao juu ya ndoa, hadi mipango ya maisha ya baadae.
Wakaafikiana kwamba ndoa itafanyika mwezi ujao ๐Ÿ’, hivyo maandalizi yaanze mapema.

Kila mmoja alijawa na furaha ๐Ÿ˜Š. Garma aliamini Ninnah ni chaguo sahihi kwani alichaguliwa na Mama yake.

---

Wakati huohuo, upande wa pili...
Wakiwa kwenye meza ndogo ya chakula iliyojaa maboga na mamungโ€™unga ๐Ÿฅฌ, mazungumzo yalikuwa kati ya Mayner na Rasma.

"Hapa ndipo mimi na wewe tutaishi. Si sehemu nzuri, lakini tutaishi kwa amani," alisema Rasma, huku akinywa chai โ˜•.

"Asante. Hakuna ubaya katika dhiki. Kikubwa ni kupambana tu. Najua tutafanikiwa... ingawa moyo wangu bado unamkumbuka Garma," alisema Mayner, huku akifuta chozi ๐Ÿ˜ข.

Rasma alimtazama kwa maumivu, akasema:
"Najua unaumia. Lakini tunapaswa kukubaliโ€”kuna watu sio sahihi maishani. Ukiwapoteza mwanzoni itauma, lakini baadaye utapata amani."

"Sijui nitayaweza maisha ya upweke. Na siku Garma atakapoamua kuoa, nitaweka wapi sura yangu?"
"Wanasema wakati mgumu ndio wakati wa kujifunza..."
Kabla hajamaliza, ghafla akatetemeka! ๐Ÿ˜ณ

"Dawa yangu iko wapi?"
"Uliweka wapi?"
"Ngoja kwanza..." alisema huku akitikisa kichwa chake. Baada ya muda alitulia.

"Nina wasiwasi nimeidondosha sehemu..."
"Wapi?"
"Kwa kaka!"

"Kwahiyo?" Mayner akauliza kwa hofu ๐Ÿ˜ฐ.

Rasma akasita kidogo, halafu akasema kwa uthabiti:
"Naenda kuichukua!"
"Nikusindikize?"
"Hapana! Wataweza kugundua mambo ya kwako. Acha niende mwenyewe..."

Wakaendelea kula, lakini Rasma alikuwa na hofu kubwa.
Je, ataikuta dawa? Au imechukuliwa tayari...?

Ukiwa mjanja utajua namna gani nakupa uhuru wa kununua kutokana na kipato chako. Tazama, simulizi nzuri kama hii unanunua kutokana na vile unajisikia. Njoo WhatsApp namba ni 0717255498 Niambie una Tsh ngapi, nikupe simulizi usome..
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

ALIFIRISIKA BAADA YA KUACHANA NA MKE ALIYECHUMA NAYE MALI | EP 15   >>> https://gonga94.com/semajambo/alifirisika-baada-ya-kuachana-na-mke-aliyechuma-naye-mali-ep-15
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Pyar Ho Jane Dushman
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest