Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Pyar Ho Jane Dushman

*UNKNOWN BABY MAMA* *Muhudumu wa hoteli alielala na bwana harusi kwenye chumba cha honeymoon.* *6-10*

27th Jul, 2025 Views 27


*_________________________________*

*SEHEMU YA SITA*

Basi tukaanza kupeana mabusu mwana pale na kila mmoja alikuwa anaonekana kama yuko hoi, nadhani mimi ndio nilikuwa hoin zaidi, aisee paul hakutaka hata kunilazia damu, akanibeba juu juu mpaka chumbani kwake, kuanzia naanza kukaa pale sijawah kuingia chumban kwake hata mara moja, kilikuwa ni chumba kikubwa, na ukikiangalia kwa makini unaweza kuhisi kama nyumba ya mtu flani mkubwa serekali, ila sikuwa na muda wa kuangalia hayo muda huo, kwa sababu sijui hata nilikuwa najisikiaje, nimekuja kuona hayo baadae sana…

Basi tukaanza kufanya yetu, mwanzo ilikuwa tabu kidogo maana kama mnavyonijua mimi sijakutana na mwanaume kwa muda mrefu, hivyo kuna namna njia ilikuwa kama imeziba flani hivi, kule kubana ndio kukawa kunazidi kumpa ukichaa paul, akawa anakazana kutema maneno yote ambayo alikuwa anayajua, aliongea mpaka akaniahidi kunipa nyumba anayoishi, sijui yeye alitegemea ataishi wapi…

Tumemaliza hapo, akaanza kuniangalia kisha akasema “ una uhakika kuwa hatujawah kukutana sehemu?...
“ hapana nikajibu maana sikutaka kuongelea jambo lolote lile kuhusu yaliopita, nay eye hakuelewa aksema tu “ ni kweli hatujawah kukutana ila sijui hata nawaza nini na wakati tumekutana juzi tu, ila chichi nakuahidi nitakutunza mamaa…

“ hapana paul, tumemkosea sana mke wako, hukupaswa kunileta nyumban kwako na haukupaswa kuja kunilaza kitandani kwa, kabla hata sijamaliza kuongea nikashangaa natulizwa na busu, ila huyu bwana anajua kunituliza, nikajikuta nimetulia mwenyewe kama maji ndani ya mtungi kisha akasema “ niliamin sura nzuri na makalio makubwa ndio bora, ila mwanamke ni heshima na utii na kujali, hayo yote sijawah kuyahisi kwenye ndoa yangu mpaka nilipokutana na wewe, chichi nakuapia hata kama nina ndoa ya kanisani, ila nitakuoa, naomba nipe muda tu, na hakuna mtu ambae atajua kuwa wewe umezaa na mtu mwingine maana mtoto amefanana sana na mimi, akasema paul mpaka nikataman kumuambia kuwa “ sijazaa na mtu mwingine bali nimezaa na wewe, ila sikutaka mambo yawe mengi, na kimya kim ya nikaondoka zangu na kwenda kwenye chumba ambacho nilikuwa nalala na mwanangu….

Siku hio sikupata hata tone la usingizi, kwa sababu nilikwa nawaza ile miguso na mapapaso ambayo alikuwa ananipa paul, nikajikuta mwili unasisimka na usingizi unakosekana kabisa, kumbe na kwa paul hali ilikuwa ni hiyo hiyo, akawa anajambia kuwa “ kwanini sikukujua mapema chichi naapa ningekuoa, mbona najikuta kama nakupenda sana, na kuna muda nahisi kama wewe ndio ule ubavu wangu wa kweli, kwanini nina amani sana nikiwa na wewe, kiasi kwamba sitamani mke wangu arudi, ohhhh chichi au ndio umeniwekea libwata kwenye chakula chako, maana najihisi kama nachanganyikiw sana juu yako wewe mtoto, akawa anawaza paul…..

Ingawa ni kwa tabu sana, ila angalau giza la usiku likaisha na asubuh kukapambazuka, sasa mimi mwili wangu hakuwa vizuri, nikaanza kuhisi kama kahoma fkani hivi, maana kama mnavyojua sijakunjwa muda mrefu sana, alafu ndio nikakunjwa jana yake, na mwili wangu hakuwa umezoea heka heka, hivyo sikuwa sawa…

Nikaamka asubuh nikapika tu chai, na nikaweka mkate mezani, mwanangu akaenda kunywa chai kisha akaenda shule, na sikutaka hata kumsubiri paul mezani nikarudi zangu chumban na kujimwagia maji kisha nikapanda zangu kitandani ili niweze kulala…

Basi paul kaamka akategemea atanikuta jikoni au mezani ila sikuwa naonekana kabisa, akaanza kuwaza kwanini sikuwa pale mezani, kuna muda akawa anawaza labda namuonea aibu kwa kilichotokea jana, na wakati mwingine akawa anawaza labda ndivyo wanawake tulivyo, tukishapata tunachokitaka basi tunaanza kutokujal na dharau pamoja na jeuri…

Basi hakuwa anajua kama anatakiwa kuenda kazini au kuja kuniona, akakata shaauri la kwenda zake kazini, ila amefika kwenye gari akawa anajiona kama hayuko sawa, si ndio akaja mpaka kwenye kile chumba ambacho nilikuwa nalala na mwanangu akagonga na kwa sauti ya unyomge nikamwambia ingia, akaingia ndani, akanikuta natetemeka, ikabidi aniulize shida ni nini, nikamuambia kuwa nahisi mwili wote unaniuma, basi akaenda kuchukua panadol kisha akanipatia na baada ya hapo akaenda kuchemsha maji na kuanza kunikanda maana ni kweli nilikuwa naumwa…

Kisha akaenda jikon na kuniandalia supu kwa mikono yake kisha akaja akaninywesha, yaan kiufupi alikuwa anajitahidi kunionesha mahaba ya hali ya juu, mpaka nikaanza kujisikia vizuri sana…

Alipohakikisha nimekula akakaa akaniomba nilale, kweli nililala nay eye akawa amekaa pemben yangu ananiangalia mpaka nilipoamka, yaan siku hio hakwenda kazini kabisa, na kazi pekee ambayo alikuwa anaifanya ni kunitazama tu, na kuhakikisha usalama wangu, hakuwa hata anajali kama mke wake alikuwa anarudi nyumbani siku hio…

“ chichi unaendelea je? Umenipa wasiwasi sana, akasema paul…
“ nahisi pilika pilika za jana na mwili wangu ni kama haujazoea kabisa, nikasema…
“ kwani wewe na mzazi mwenzako mna muda gani tangu mmeshiriki hili tendo? Akauliza…
“ miaka sita, maana kuanzia nimelala nae, hata hajui kama nina mimba ya mwanae, na hajawah kurudi tena kuanzia siku hio, hivyo chukua miaka ya Jordan wake na muda ambao alikaa tumboni miezi tisa, kipindi chote hicho sijawah kukutana na mwanaume mwingine kimwili…

Nikashangaa paul anaanza kutabsamu kisha akasema “ ndio maana kulikuwa kumeziba kumbe ni kwasababu unajitunza, ila endelea kujitunza hivyo hivyo mamaa…

Basi tukiwa tunaongea mara simu ya paul ikaanza kuita, aliekuwa anapiga ni mke wake, akawa anasema kuwa yupo kwenye taksi anakuja nyumban…

Nikashangaa paul anasonya kisha akaniangalia na kusema “ natamani huyu mwanamke hata asingerudi…
“ kwanini unasema hivyo na wakati ni mke wako? Ikabidi niulize japo kuwa na mimi kuna namna ka moyo kangu kalikuwa kananiuma, maana sikuwa naelewa kama ni nimempenda paul au ndio nimemzoea…

“ sijawah kupata raha ya kwenye ndoa chiochi, huyu mwanamke amezoea kunikosea kila siku na mimi huwa ndio namuomba msamaha maana ukweli ni kwamba nilimpenda sana, amekuwa ananipiga matukio kutwa kucha, na hapa amerudi mapema kwa sababu sijamtafuta nilikuwa busy na wewe, ndio maana anarudi maana anaona kama kuna hali ambayo sio ya kawaida,ila usijali chichi, hata kama akija bado sitaacha kuwa mtu wako wa karibu sana, akawa anasema paul…

Nikatabasamu pale, mara tukasikia honi, na mlinzi alikuwa anafungua geti, paul akainuka kisha akasema ngioja nikamuangalie amekuja na vitimbi gani, basi huyo akatoka, aisee moyo wangu ulikuwa unaniuma sana ila nikajikaza tu, maana sikuwa nataka kuonekana dhaifu mbele ya paul…

Nikatoka kuchungulia, aisee huyu dada ni mzuri sana aisee, na najua anajijua kuwa yeye ni mzuri ndio maana anaringa sana kwa kweli, nikaanza kujilinganisha nae, kiukweli mimi simfikii hata robo…

Basi akamkumbatia paul kisha akambusu, hapo mimi naumia mpaka nataka kupasuka, ila ndio hivyo sina cha kufanya, basi wakaingizana ndani na kama baada ya dakika kumi mara sms ikaingia ilikuwa inatoka kwa paul na kusema “ laity kama angekuwa hajarudi sasa hivi ningekuwa nipo na wewe, najua ni muda mchache umepita ila nimekumisss sana chichi mamaa…

Ingawa nilikuwa na maumivu, ila hii sms ni kama ilinipa nguvu na nikajikuta natabasamu, sijui hata na waza nini mimi, na wakat najua kabisa ni mume wa mtu….
ITAENDELEA….

*SEHEMU YA SABA*

Basi mwanangu akarudi kutoka shule, na wakati huo nilikuwa nimepitiwa na usingizi, akapitiliza mpaka ukumbini, na kumkuta paul amekaa na mke wake, Yule mke wa paul alipomuona Yule mtoto alishtuka sana, kwa sababu Jordan wangu alikuwa amefanana sana na paul kupita maezo…

Mwanangu hakuwa anaelewa kinachoendelea, akamfata paul, akajua labda yuko na mgeni wake, hivyo akawasalimia wote kisha akamkumbatia Jordan na paul alimuonesha ushirikiano wa kutosha na hata alipomuita mama alikuwa anaona ni sawa tu, na yeye akawa anaitikia ndio mwanangu, kitu ambacho kilimuacha mke wa paul na taharuki pamoja na maswali mengi yasiokuwa na majibu…

“ paul usiniambie kuwa umezalia nje, unakumbuka ahadi zote ulizonipa, kwamba utakuwa kuwa na mimi kwenye shida na raha, na magonjwa na uzima, alafu leo unakuja kunileta mtoto wan je wa ndoa kweli, akawa analalamika mke wa paul hapo…

“ ahadi gani kubwa ambayo nimekupa ambayo haiwez kuvinjika, Jordan mwanangu embu twende nje tukacheze, na kama unajiona mgumba nenda kazae na wanaume zako, kama kawaida yako unavyotoa mimba, ukadhani kuwa nitakuwa nakuvumilia kila siku….

Yale maneno yalimuumiza sana mke wa paul, mke wa paul bana ni wale maslayquuen, yaan hajui kupika, hakuji kuosha vyombo, hajui kusafisha nyumba, yaa kiufupi hana anachokijua kuhusiana na kazi za nyumbani, na alikuwa anauhakika kuwa paul anampenda sana, hivyo kuna muda alikuwa mpaka anamsaliti na mwisho wa siku paul ndio akawa anashia kuomba msamaha maana alikuwa anampenda sana, sasa kitendo cha paul kutokujali kulimpa maswali mengi sana, na kujihisi kama hana nafasi tena kwenye moyo wa mume wake, na ndio ukweli iolikuwa hivyo…

Maaana sio kwamba hata alikuwa ameondoka nyumban kwa sababu ya maana labda bishara na vitu kama hivyo, ila aliondoka nyumban kwa sababu mume wake amemuambia hataki anywe pombe, ndio akasema kuwa hataki kupangiwa maisha, na sio mara yake ya kwanza, kuondoka, huwa anaondokaga hata miezi sita ndio anarudi nyumbani, na akikaa huko kwao anaanza kujikumbushia kuhusu wanaume wake wa zamani, na sio wa kumpigia simu, wala kutuma sms yaan vitu vyote alikuwa anafanya paul, na hata mwanamke akimkosea yeye ndio alikuwa anamuomba msamaha, kwa sababu aliamin kuwa paul anampenda sana na hawez kumuacha…

Paul hakuwa anaonekana kumjali kabisa, alikuwa yupo busy anacheza na Jordan hapo hajui kama nipo ndani kwa sababu nilikuwa najisikia vibaya hivyo sikutoka nje, Yule mwanamke akaanza chuki juu ya mwanangu akijua kuwa labda kuna mwanamke amemtelekezea paul mtoto, kumbe mwanangu sijamtelekeza na ninaishi nae…

Basi siku hio baada ya paul kumaliza kucheza na mtoto, akanifata chumbani, aliniletea matunda kisha akaanza kunisaidia kumbembeleza Jordan alale, baada ya kumuogesha na Jordan alipolala akaomba anilishe, nikakataa, na kumtaka aende kukaa na mke wake, maana sitaki matatizo…

“ nikienda kukaa na Yule mwanamke ni makelele tu na ndio maana nimechagua kukaa huku mpaka nikihakikisha amelala, akasema paul, ila bado sikutaka kukaa nae, maana ndoa iheshimiwe bana kwa watu wote, alipoona nasisitiza sana kuwa nataka aondoke, basi aliondoka na kwenda kwa mke wake…

Baada ya dakika chache, nikaanza kusikia Yule mwanamke anaanza kutukana, sikuwa nasikia kabisa sauti ya paul, Yule mwanamke alitukana na kugomba mpaka nikapitiwa na usingizi, sikujua hata alinyamaza saa ngapi…

Asubuh ya siku hio haikuwa siku ya weekend ila paul alichagua kutokwenda kazin, akaja na kunisaidia kumuandaa Jordan na hapo nilikuwa nimeshaanza kukaa sawa, ila alimuandaa mwanangu kisha akampa chai na kumtaka aende shule, na baada ya hapo akataka nitoke nikaungane nae kwenda kupata chakula cha asubuh…

Nilikuwa naogopa sana, ila akasisitiza sana kuwa hawez kula pekee yake, na mke wake ni mvivu sana, kwa hio hatoamka muda huo, basi nikatoka na kwenda kunywa nae chai, ile namaliza kunywa chai mwanamke huyo hapo, alikuwa amevaa vibaya, kwa maana alivaa kachupi na kasidiria tu na kagauni chepesi akawa anatoka, na vile mwenyezi mungu alimbariki sana ikawa ni balaa, yaan kwa namna alivyoumbwa mwanaume yoyote Yule hawez kuacha kumtazama ila paul hakuwa na muda na mkewe, kitu ambacho kilinishangaza sana, maana hata mimi ni kama niliduwaa na ni mwanamke mwenzake….

*SEHEMU YA NANE*

“ huyu ni nani? Akauliza mke wa paul…
“ mama yake Jordan, akajibu paul huku akiwa anakunywa zake maji bila wasiwasi…
“ hata kama ni ushenzi basi wewe umezidi, yaan ukaona mpaka uniletee mwanamke ulie zaa nae pamoja na mtoto wake kwenye nyumba yangu kweli paul, hakika unanikosea sana, akawa analalamika…
“ kama hautaki kukaa nao ondoka wewe, na Jordan sio mwanangu na wala huyu mwanamke sijazaa nae, ila kama huamini naomba ufikirie unavyotaka mwenyewe, akasema kisha akanifata na kunambia “ chichi tuondoke…

Nikasimama na kuanza kuondoka, aisee Yule mwanamke akanifata na kunirukia, akaanza kunipiga, na kwakuwa sikutegemea nikakosa balance, paul alimfata mke wake alimpiga sana, Yule mwanamke akaanza kulalamika kuwa “ kuanzia unanioa haujawah hata kuninyooshea kidole, na leo hii unakuja kunipiga kisa mwanamke, huyu dada atakuwa amekuwekea libwata sio bure, maana mimi namjua mume wangu ambae alikuwa na mapenzi ya dhati na mimi, akawa analalamika…

Paul akacheka kisha akasema “ haumjui mwanaume mwenye mapenzi ya dhati na wewe, bali unamjua mwanaume mpumbavu na ambae alishindwa kukufundisha adabu mapema mpaka ukawa mshenzi kiasi hichi, umekuwa mshenzi sana wewe mwanamke, umetoa mimba zangu nyingi kisa uliogopa kuharibu mwili wako, ukaona haitoshi ukaleta mwanaume ndani ya nyumba yangu na kulala nae kwenye kitanda changu sio mara moja, nimeshakufumania mara nyingi sana wewe mwenyewe unajua, haujawah hata kutandika kitanda ambacho huwa unalala mwenyewe hata mara moja, alafu unakuja kunambia sijui chichi kaniwekea limbwata, embu nambie hapo nani ndio mchawi kati yako wewe na chichi…

Yule mwanamke alikaa kimya kama vile amemwagiwa maji ya baridi, hakutia neno lolote lile hata kwa bahati mbaya, akawa anaangalia chini, na paul akataka kuondoka na mimi ila sikutaka maana sikutaka niwe sababu ya ugomvi wa wanandoa hata mara moja….

Basi siku hio sikutaka kuonana na paul wala mke wake, nikawa nayafikiria maisha yangu na nikaona kuwa nastahili kuondoka pale, kwa sababu sio busara kuvunja ndoa ya mtu…
Paul alinipigia simu mara kadhaa na kunitumia sms za kunimiss mara anashindwa kulala ila sikujibu sms hata moja, maana sikutaka kumpa shetani nafasi tena…

Cha ajabu siku hio Yule mke wa paul akaamka na kuanza kumpikia chai mumewe, ila paul hata hakutaka kunywa akaenda zake kazini, na kitendo cha paul kwenda kazini Yule mwanamke akanifata, akajua kuwa anaweza kuniotea tena, hapo mwanangu ameenda shule…

“ wewe Malaya mchukua waume za watu, ukaona usimpe tu kitumbua mpaka umzalie, akawa anafoka kwenye mlango wa chumba ambacho nilikuwa nakaa, ikabidi nitoke nje, ili tuonane uso kwa uso, maana kumjibu mtu hali ya kuwa hakuoni ni kama udhaifu mkubwa sana kwangu…
“ mimi sijazaa na mume wako, yeye mwenyewe ameshakuambia na kama umalaya basi nimerithi kwako, usijali nitaondoka nyumban kwako muda sio mrefu, maana sitaki kupigishana kelele na wewe, naomba nipe siku chache naondoka…

Su akanifata akataka kunipiga, aiseee nilimpasua mpaka akawa anakimbia kama kachanganyikiwa, kisha nikamuambia “ najua nimekosea kuja kukaa hapa nyumban kwako bila ridhaa yako, ila hauna haki ya kunigusa hata kucha mimi na mwanangu, na ukifanya hivyo ndio utajua kama nachezaga mereka au karate…
ITAENDELEA

*SEHEMU YA TISA*

Yule mwanamke aliondoka, ila kiukweli nilijiona mwenye hatia sana, na paul aliporudi nikamuomba niondoke, maana sikutaka kuendelea kukaa pale tena…
“ unataka kuondoka uende wapi mamaa, huyu mwanamke hatakaa akusumbue na kama anataka kuondoka anatakiwa kuondoka yeye na sio wewe, maana hii nyumba ni yangu nay eye ameikuta, angekuwa hata amenizalia au ananiheshimu ningesema tunagawa ila hana kitu hapa, akawa anasema paul…

“ hata kama ila huyu ni mke wako, na kila anachokifanya ni haki, maana anatetea ndoa yake, nikawa nasema…
“ anaitetea vipi ndoa amb ayo tayar imeshavunjika, nilimpenda na kumpa kila kitu ila alinilipa nini kwa upendo ambao nilimpa zaidi ya mateso ya kihisia na maumivu tu…
“ hio ni kati yenu paul, ila sitaman mimi kuwa sababu ya kuvunjika ndoa, nikasema nikashangaa natulizwa na busu, ila huyu mwanaume sijui ananitaka nini, nikajikuta nimepoa kinyama, na alipoona nimepoa akaendeleza harakati za kunikiss, aisee nilipewa busu moja matata mpaka nikajikuta nimetulia mpaka nywele, alipomaliza akasema “ I need you chichi, na hakuna mtu ambae anaweza kukuondoa hapa hata akisema nini na akifanya nini, maana hii nyumba ni yangu na mimi ndio najua ni nani anatakiwa kukaa kwangu na nani anatakiwa kuondoka, naomba usiendelee kutamka kauli za kukaa mbali na mimi kwa namna yoyote ile kisha akaondoka zake…

Nikabaki nimepoa sina cha kufanya, mapigo ya moyo wangu yalikuwa yanadunda sana na kila mdondo ulikuwa unataja jina la paul, nikajihisi kama nimeshaanza kumpenda ila ndio hivyo sikuwa najua natakiwa kufanya nini ili kumfanya akae mbali na mimi maana mimi sio mkorofi wala mvurugaji wa ndoa za watu…

Nikiwa pale nikaanza kusikia wanagombana, ila nilikuwa nasikia sauti ya Yule mwanamke tu, wakagombana sana sijui hata ni mpaka saa ngapi, mimi nikawa zangu ndani kwangu hata chakula nililetewa na Yule mfanyakazi, akawa ananiambia “ mama wa hii nyumba ni mshenzi sana, amemtesa sana huyu kijana hivyo kama unaweza kumpa faraja mpe tu, maana ameteseka kwa kipindi kirefu sana…

Nikaitikian tu, ila nilipanga niondoke,basi muda ulienda, na kwenye usiku mkali nikaanza kusikia mlango kama unafunguliwa, nikajua labda Yule mwanamke amekuja kuniangamiza, nikasimama na night dress tu, kumbe bana paul amenimiss, akaingia kwangu akiwa na boksa, mwanangu alikuwa amelala….

Aliponiona akaniparamia bila hata kuniruhusu niseme chochote kisha akaanza kunipa mabusu yasio na idadi…
“ paul unafanya ninio? Unatakiwa kukaa na mke wako muda huu..
Akaweka kidole chake kwneye lips zangu kwa ishara ya kunitaka nikae kimya, kisha akasema “ nimelala na Yule mwanamke ila akili na fikra zangu zote zipo kwako, I want you, I want you chichi, hapo anasema huku mikono yake ikiwa inafanya utalii wa ndani kwenye mwili wangu…

Sijui nilikuwaje maana nilikuwa mdhaifu sana kwa paul, nikajikuta nampa ushirikiano bila kutaka, basi tukafanya yetu na baada ya kumaliza paul akataka kunisababishia matatizo, kwa sababu akawa anataka kubaki chumban kwangu alale..
“ naomba uende kwa mke wako, hapa penyewe tunamkosea sana, nikawa nalalamika…
Akaniangalia kisha akasema “ haujui ni kiasi gani napata hisia na Napata futraha nikiwa na wewe, yaan nimeshajikuta siogopi chochote kile zaidi ya kukupoteza chichi, najua una mtoto ambae amefanana na mimi ila sio wangu, ila naomba tufanye tupate mtoto wetu, nakuapia namuacha huyu mwanamke akafundishwe na ulimwengu nakuoa hata kama nani aseme nini…

“ hapana sio sawa wewe nenda kwako, nikazidi kumsisitizia mwisho akakubali …
ITAENDELEA..

*SEHEMU YA KUMI*

Basi kesho yake mke wake akaamka na mkazo kuwa mimi na mwanangu natakiwa kuondoka kwenye ile nyumba, maana kama ni majukum ya mume wake anaweza kuyafanya vizuri sana, na hataki msaidizi…
Paul akamuambia mke wake kama anaweza kufanya kila kitu basi afukuze mfanyakazi, maana alikuwa anauhakika kuwa mke wake hajui kufanya kazi na amelelewa kimayai sana…

Mke wake hakutaka, ila paul akasisitiza kuwa kama anataka mimi na mwanangu tuondoke basi afukuze mfanyakazi, na kama hawez basi sisi hatutaondoka…
Mke wake hakujibu kitu na badala yake akaingia ndani kwa unyonge, siku hio ilikuwa ni ya purukushani sana, maana walikuwa wanagombana sana paul na mke wake mpaka nikawa nashangaa hawa watu wameshawah kuongeaga vizuri kweli au ndio vita ni vita mura…

Basi asubuh nikamuona Yule mama anaondoka, akanifata na kunakb ia “ huyu mwanamke ni zaidi ya shetani kuwa nae makini kisha akaondoka zake, na bada ya Yule mama kuondoka nikaingia zangu ndani nikawa nasikia wanatukanana, safar hii hata paul hakuwa anakaa kimya kama anavyokaaga…

Basi baada ya muda nikasikia ukimya unatawala, siku hio nilikuwa naogopa hata kuingia ndani kupika, yaan kuanzia nilipokula chakula cha asubuh sikula kabisa, nilikuwa nasubiri tu mwanangu arudi, na kwakuwa ameshalipiwa ada ya mwaka mzima, basi nikasema tutalala popote, basi wakati Jordan wangu anarudi nikuwa nimeshafungasha kila kitu nikawa natoka…

Wakati natoka Yule mwanamke akaanza kutukana pale, akatukana sana, na paul alikuwa kimya tu anatuangalia kana kwamba karuhusu sisi tuondoke pale nyumbani kwake…

Ila tulipotoka tu nje ya geti sms ikaingia kutoka kwa paul ilikuwa inasema “ nimeshawaandalia sehemu ya kuishi, naomba usikatae offer yangu…
“ nashkuru sana kwa moyo wako, ila naomba nikapambane mwenyewe, sitaki kukuona tena ukigombana na mke wako kwa sababu yangu, na mimi nikajibu hio sms alionitumia…

“ chichi haunijui vzr, nimekuomba kistaarabu kuwa uende sehemu niliyokuandalia, laa sivyo nitatumia nguvu na nitakurudisha humu ndani, na nimekuruhusu uondoke maana nakusikiliza sana na sitamani kukukwaza, ila naona kabisa tunapoelekea nitatumia mabavu, hivyo kwa amani ya bwana, panda hilo gari hapo nje na ukubali likupeleke litakapo kupeleka maana wewe na Jordan wote ni majukum yangu, akatuma sms nyingine inasema hivyo….

Nikaona nisiwe mbishi, nikapanda kwenye gari na kwenda moaka kwneye nyumba moja, ambayo ilikuwa ni selfu na ilikuwa na kila kitu ndani, ila sikujua paul alijipanga saa ngapi, mwanangu akawa anashangaa na akawa ananiuliza baba yake atakuja saa ngapi, nikamuambia tu atakuja…

Basi siku hio kwa mara ya kwanza tulilala kwenye makazi mapya mimi na mwanangu, na paul hakunitafuta, ila asubuh na mapema akaja kutusalimia na kutuletea mahitaji ya muhimu mimi na mwanangu kisha akatuaga kuwa anaenda kazini….

Kule kwa mke wake akaona muda sio mrefu ataachwa, akaanza kutafuta makungwi wamfunde ili amteke mume wake, maana alikuwa anamfanyia ujinga akijua kuwa alikuwa anampenda sana, ila kwakuwa ameshaanza kuona mume wake amebadilika na hamjali tena, akajiongeza na kuona hapa sasa talaka nje nje ila hakuwa anajua kuwa alikuwa ameshachelewa, maana mwanaume anaweza kuvumilia mambo yote ila sio usaliti ambao alikuwa anamfanyia…

Baada ya paul kutoka kazin akaja nyumbani kwangu, na kunambia kuwa anatyaka kulala pale, ila sikutaka, ila Jordan akaanza kusema “ mama muache baba leo alale na sisi, nikajikuta nimekubali kumbe mtego huo…..
ITAENDELEA ……

KWETU morogoro.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

*UNKNOWN BABY MAMA* *Muhudumu wa hoteli alielala na bwana harusi kwenye chumba cha honeymoon.* *6-10*  >>> https://gonga94.com/semajambo/unknown-baby-mama-muhudumu-wa-hoteli-alielala-na-bwana-harusi-kwenye-chumba-cha-honeymoon-6-10
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Pyar Ho Jane Dushman
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

SEHEMU YA 32💘💘

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

majario rewards 100 Comments 0
 

SEHEMU YA 30💘💘

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest