Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

ALIFIRISIKA BAADA YAKUMUACHA MKE ALIYECHUMA NAYE MALI | EP 09

27th Jul, 2025 Views 4



Ninah ilibidi azuge maana hakukuwa na namna nyingine ya kuepuka aibu iliyokuwa mbele yake. Alimtazama Mama Garma kisha akasema:

โ€œMama... kwahiyo si muda wa kuondoka au?โ€ ๐Ÿคจ

โ€œKuondoka uende wapi? Kwanza ulikuwa unafanya nini chumbani kwangu? Na hicho unachokificha ni nini?โ€ ๐Ÿ˜  Mayner aliuliza huku akianza kupiga hatua.

โ€œKhe! Unauliza hivyo kama nani? Wewe ni nani humu ndani?โ€ ๐Ÿ˜ค alisema Mama Garma.

โ€œMama, hii haikuhusu. Samahani we binti, naomba unijibu nilichokuuliza.โ€ ๐Ÿ˜

โ€œNinah usipoteze nguvu kumjibu huyu malaya. Nenda.โ€ ๐Ÿ˜’ Mama Mayner alisema.

Kwa aibu ya hali ya juu huku akitetemeka, Ninah alianza kupiga hatua ili aweze kutoka nje. Mwili wake na miguu vilionekana kutengana kabisa, hofu ilimjaa kwa kudhani huenda angepigwa. Alipojaribu kutoka nje aligundua kuwa mlango umefungwa. ๐Ÿšช

Mayner alikuwa tayari ameufunga mlango huku akishika funguo mkononi, akamtazama Ninah na kusema:

โ€œSiwezi kuona nataniwa ama kuchezewa halafu nikuache tu. Naomba hiyo chupi.โ€ ๐Ÿ˜ก

โ€œYako?โ€ Mama Garma alidakia. ๐Ÿ˜ณ

โ€œHayakuhusu!โ€

โ€œToka bwana, Ninah nipe hiyo chupi!โ€ ๐Ÿ˜ค Mama Garma alisema huku akimsogelea Ninah.

Mikono ya Ninah ilizama kwenye matiti na kutoa chupi, kisha akamkabidhi Mama Garma. ๐Ÿ˜ฐ

โ€œMama unanitakia nini lakini? Kipi ambacho unakitaka kwangu? Nimekosa nini? Mbona sijawahi hata kukuchukia... ni nini lakini hii?โ€ ๐Ÿ˜ข Mayner alizungumza huku machozi yakimtoka.

โ€œWe! We! We! Naomba unikome, nikome kabisaaaa! Mimi siwezi kuzaa kifaranga kimalaya kama wewe! Mwanangu anajitambua! Rasma unamuona ana tabia kama zako? Unamwona Rasma kuwa malaya?โ€ ๐Ÿ˜ค Mama Garma alisema, kisha alipiga hatua hadi kwenye glasi iliyokuwa mezani.

Aliweka chupi ndani ya glasi, akaimimina maji kisha akaikamua. Maji yaliyodondoka chini yalikuwa na rangi nyeusi tii. ๐Ÿ˜ง Kwa jinsi chupi hiyo ilivyoonekana mwanzoni, haikutarajiwa kama ingeweza kutoa maji ya aina ile.

โ€œAha! Chukua chupi yako!โ€ ๐Ÿ˜  alisema Mama Garma huku akimtupia chupi ile usoni kwa Mayner.

Uso wa Mayner ulipokea chupi hiyo ambayo ilikuwa na harufu mbaya isiyo ya kawaida. Alijikuta akiichukia na kuitupa chini, lakini bado harufu hiyo iliendelea kuenea katika mwili wake. ๐Ÿคข

Ni kama vile marashi yasambavyo kwenye nguo, ndivyo harufu hiyo ilivyokuwaโ€”ilisambaa kwa haraka mno. Mayner ilibidi azibe pua yake kisha akaondoka kuelekea chumbani. Akili yake ilimwambia ni lazima aoge ili awe sawa. ๐Ÿšฟ

Nyuma aliacha maongezi yakiendelea, naye hakuwa na habari nini walikuwa wakikiongea.

โ€œWazungu wanasema deal done, sijui hata wanamaanisha nini... lakini ndio hivyo, dili limekamilika! Atanuka huyu kama papa!โ€ ๐ŸŸ Mama Garma alisema huku akimsogelea Ninah na kumpa mkono.

โ€œUjue alivyonifumania nikasema โ€˜Mama yangu leo nakufaโ€™. Kumbe kha, hana lolote! Ila Mama... si kila kitu kipo tayari au?โ€ ๐Ÿคญ

โ€œNdio, sidhani kama anaweza kukwepa. Na hili... halafu unadhani ana nguvu? Si unamuona alivyokuwa goi goi?โ€ ๐Ÿ˜

โ€œKanaonekana tu, sijui hakali vizuri! Halafu harufu iliyotoka... sio ya kitoto!โ€ ๐Ÿคข

โ€œHakuna wa kunichezea mimi wewe! Nazijua mbinu zote za kuangamiza kunguni kama hizi!โ€ ๐Ÿ˜  alisema.

Waliendelea na maongezi ya furaha hadi pale furaha hiyo ilipoisha. Ninah aliaga na kuondoka, lakini aliona taarifa ile ni muhimu kumfikishia mama yake kuwa kila kitu kimekwenda sawa.

---

โ€œMama, unajua siamini kama kweli ile dawa inafanya kazi...โ€ ๐Ÿค” Ninah alisema huku akiwa amekaa kwenye sofa sebureni kwa Mama yake.

โ€œMh! Sasa nawe uendage humo uolewe halafu ujifanye sijui unaleta mambo yako ya kipuuzi. Haki nahisi utatolewa kichwa kabisa!โ€ ๐Ÿ˜’ Mama yake alijibu.

Walikuwa sebureni kama familia, wakipanga mkakati wa namna ndoa itakavyokuwa, maisha yatakavyokwenda, na matumaini ya kudumu. Hawakujua kama mwanaume atakubali, lakini kwao, walitosheka kuamini kuwa kila kitu kitaenda sawa baada ya mafanikio kwa Mayner. ๐Ÿ’

โ€œWe! Hapa nishajipanga kwa kila kitu. Unadhani kukaa kwenye lile jumba ni mchezo au?โ€ ๐Ÿ˜Œ

โ€œHahaha! Shauri yako! Wenzako wanatafuta nafasi ya kuwepo pale lakini hawaipati. Ila pambana mwanangu!โ€ ๐Ÿ˜„

โ€œMama siwezi kukuangusha, siwezi kabisa! Najua ninachokifanya. Najua nitamteka huyo Garma, mbona mwaka wa kwanza tu hii nyumba yetu itakuwa imeboreshwa!โ€ ๐Ÿ˜Ž Ninah alisema huku akitazama nyumba yao.

Ilikuwa nyumba iliyochoka, wakazi wa Mkuyuni waliitambua kama miongoni mwa nyumba mbovu zaidiโ€”mvua ikinyesha, maji yalikuwa yakikaribishwa kama wageni sebuleni. ๐ŸŒง๏ธ

Umasikini ulikuwa upande wa Mama Ninah. Aliona mtaji wake pekee ni kwa Garma endapo binti yake angeolewa naye.

โ€œKikubwa, hali ya nyumbani unaiona. Mwanamke anapendezesha kwao. Mwenzako anavyoteswa vile... yule ni mjinga! Hela anapata lakini hana mpango wa kuboresha kwao. Usidhani ndoa ni furaha tu... wanaume wenyewe siku hizi licha ya kuwa wachache, hawafahamiki pia.โ€ ๐Ÿ˜ค

โ€œJamani mama, maneno mengi ya nini? Utaharibu ulichokisema mwanzo. Niachie mimi kazi, najua la kufanya. Halafu nasikia kuna watu wanaoishi huko milimani wanahamishwa?โ€ ๐Ÿค” alibadilisha mada.

Mama yake alivuta pumzi kisha akamwambia:

โ€œNdio, acha tu. Watu wanahamishwa huko. Ukiishi mabondeni ni tabu, milimani nako kazi tupu. Sijui tutakaa wapi...โ€ ๐Ÿ˜Ÿ

โ€œHaha! Kutafuta kiwanja maeneo mengine, ila nao wamekosa sehemu za kuishi bwana?โ€

โ€œKwa Mwanza utaenda kuishi wapi? Viwanja vimepanda bei hatari! Huko Nyashishi, Kishiri... bei usiseme!โ€ ๐Ÿ˜ฌ

โ€œBasi ngoja mimi niondoke zangu...โ€ Ninah alisema huku akisimama. ๐Ÿ‘œ

---

Majira ya usiku nyumbani kwa kina Garma, Mayner alionekana jikoni akipika. Mchuzi uliendelea kutokota, naye aliendelea kuonja kujua kama chumvi imetosha. ๐Ÿ‘ฉโ€๐Ÿณ

Garma alikuwa chumbani akichezea laptop, huku Rasma na Mama Garma walikuwa sebuleni wakiangalia runinga. ๐Ÿ“บ

โ€œKwa hiyo hiyo ndoa lini?โ€ ๐Ÿคจ Mama Garma aliuliza.

โ€œKwani unaitaka enh? Si ulisema huna mpango nayo. Tulia watu wale mpunga! We baki na kisirani chako, Akha!โ€ ๐Ÿ˜ Rasma alisema kwa nyodo huku akichezea simu yake.

Mama Garma alibaki kimya, akiwa na picha kichwani kuhusu maisha ya Mayner. "Mh! Mngejua huyu mtu wenu kashakuwa mzoga pale alipo, anatembea akiwa ameoza..." alijiambia moyoni. ๐Ÿ˜ค

Mayner alileta chakula mezani, Mama Garma alikohoa kisha akasema:

โ€œMbona nahisi kuna harusi ya mzoga? Nani kafa?โ€ ๐Ÿง

โ€œWe naye unachosha sasa kha. Wifi chakula tayari enh?โ€ Rasma alimkosa mama yake huku akibadilisha mada.

โ€œNdio tayari, karibuni. Ngoja nikamuite kaka yenu.โ€ ๐Ÿ˜Š Mayner alisema na kuondoka.

Ingawa alionekana mzima kimwili, kichwani kulikuwa na mateso. Kauli ya mama mkwe alijua ilikuwa juu yake. Hakutaka kujibu wala kuonesha kukerwa.

Aliingia chumbani, akamsogelea mume wake na kusema kwa upole:

โ€œBaby, chakula tayari.โ€ โค๏ธ

โ€œWow! Asante nilikuwa na njaa mno!โ€ ๐Ÿ˜‹

โ€œHahaha! Nilijua, ndio maana nimepika chakula ambacho unakiโ€ฆโ€ alisita baada ya kuhisi kuna kitu kinampita mapajani. ๐Ÿ˜จ

โ€œVipi mbona kimya?โ€ Garma aliuliza.

โ€œHapana... ila sawa. Tangulia nakufuata.โ€ Alielekea bafuni. ๐Ÿšถโ€โ™€๏ธ

Alipofika, alivua sketi na kujitazama. Aliona majimaji meusi yakitoka ukeni. ๐Ÿ˜ณ

โ€œNini hii?โ€ alijiuliza huku akigusa na kunusaโ€”harufu kali!

โ€œMungu wangu... ni nini hiki?โ€ ๐Ÿ˜ฑ alisema kwa sauti.

Alipoingiza kidole kuangalia, funza mkubwa mweupe alidondoka kutoka sehemu yake ya siri... akaanza kutambaa. ๐Ÿ›

โ€œInamaana nimeoza?โ€ alijiuliza kwa mshangao.

Wakati anajiuliza, mafunza zaidi waliendelea kutokaโ€ฆ

ITAENDELEA... ๐Ÿ‘€๐Ÿ’”

Utaratibu wa kumpangia mtu bei ulishapita na wakati. Tupo kwenye dunia huru na salama zaidi. Raha ya kununua ipo pale ambapo muuzaji anakuambia, Lipia kwa pesa unayotaka. Leo, simulizi hii unaweza kununua kwa pesa yako mwenyewe. Nitext WhatsApp, namba ni 0717255498. Nunua kwa pesa yako..
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

ALIFIRISIKA BAADA YAKUMUACHA MKE ALIYECHUMA NAYE MALI | EP 09  >>> https://gonga94.com/semajambo/alifirisika-baada-yakumuacha-mke-aliyechuma-naye-mali-ep-09
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest