Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  gonga94 official track

ALIFIRISIKA BAADA YA KUACHANA NA MKE ALIYECHUMA NAYE MALI | EP 11

27th Jul, 2025 Views 24



Mayner akiwa ndani alipata kusikia kile kilichozungumzwa na Mama Garma. Alibaki mdomo wazi ๐Ÿ˜ฎ, asijue ni wapi alisikia kwamba anataka kwenda kwa mganga? Alijaribu kuchanganya akili yakeโ€ฆ je, aliona ukaribu wa Rasma na mama yake? Lakini kumbukumbu kamili zilimkosa.
โ€œMama kajuaje kama nataka kwenda kwa mganga? Au itakuwa ni mwanga? Mbona anajikinga sana hivi?โ€ alijiuliza, lakini majibu hayakuja ๐Ÿคทโ€โ™€๏ธ.

Akiwa katika dimbwi la mawazo ๐ŸŒ€, alistuliwa na Garma ambaye alifungua mlango kisha akaingia ndani.
โ€œMama anasema kwamba unataka kwenda kwa mganga ili umroge... sijui kufanyaje... ya kweli hayo?โ€ aliuliza.
โ€œMganga? Kumroga Mama? Nani ambaye amesema?โ€ aliuliza Mayner kwa mshangao ๐Ÿ˜ณ.
โ€œNi yeye. Nilikuwa naongea naye hapo nje. Kasema kwamba amekusikia ukitaka kwenda kwa mganga. Kama ni kweli unataka kufanya hivyo, ebu simamisha mara moja!โ€ Garma aliongea kwa hasira ๐Ÿ˜ .
โ€œMume wangu, tangu lini umeniona mimi nikienda kwa mganga lakini?โ€
โ€œNdio nakuambia hapo. Tusije kuonana wabaya mbeleni. Mambo ya kishirikina, sijui makombe na mitishamba, humu kwangu sitaki. Ukiona unaumwa sana Qurโ€™an ile pale, fungua zako soma ๐Ÿ“ฟ,โ€ alizungumza Garma huku akiwa na sura ya kuchukiza ๐Ÿ˜’.

Kwa namna ambavyo alikuwa akiongea, ni wazi kwamba alikuwa amechukia kupita maelezo. Na huu ndio ulikuwa ni ukweli. Kwake, hakupenda kusikia lolote kuhusiana na waganga wa kienyeji ama jadi.

Aliwachukia kuliko hata anavyoichukia njaa. Hakuna hata mmoja ambaye alikuwa akimwamini. Alikuwa na dhana kwamba kila anayekwenda kwa mganga wa kienyeji ni mchawi ๐Ÿง™โ€โ™‚๏ธ.
โ€œMume wangu, sio kweli. Nilitegemea kwamba ungeniuliza hospitali wanasemaje hata kabla ya kuuliza kuhusu mimi na mganga. Hata sielewi,โ€ Mayner alijitetea kwa kuleta habari za hospitali ๐Ÿฅ.
โ€œMama kanichanganya hadi nashahau... enh, wanasemaje?โ€ aliuliza Garma.
โ€œSina ugonjwa.โ€
โ€œKhe! Tena?โ€
โ€œNdio. Hadi nashangaa ni nini ambacho naumwa.โ€
โ€œUlipima vipimo vyote?โ€
โ€œNdio. Nilifanya hivyo. Ila... ila kuna dawa ambazo wamenipa. Ni hizi hapa.โ€ alisema, kisha aliinuka na kwenda hadi sehemu aliyoweka mkoba wake uliokuwa na dawa ๐Ÿ’Š.

Alirudi tena sehemu ya mwanzo na kumkabidhi zile dawa Garma, ambaye alipokea na kuzitazama.
โ€œUnameza kwa siku ngapi?โ€
โ€œNi tano. Na kama sitakuwa sawa, natakiwa kwenda tena.โ€
โ€œInamaanisha huna hata fangasi au magonjwa ya ngono?โ€
โ€œNiyatolee wapi? Kila siku nalala na wewe na nimekuwa msafi kupitiliza ๐Ÿ˜‡. Hata hivyo, nikifanikiwa kumaliza tu kama sijapona, basi nitarudi tena hospitali.โ€ alisema Mayner.

Waliingia katika kina cha maongezi kilichojawa na stori za hapa na pale. Kila mmoja alisimulia na kuzungumza lake, huku mpango wa ndoa ukiendelea kuwa kiini kikuu cha mazungumzo ๐Ÿ’.
Waliambiana namna ambavyo ndoa yao itakuwa ya tofauti โ€” kuanzia muonekano hata namna ukumbi utapambwa. Hatimaye, usingizi uliwapa salamu, nao walikubali kuitikia ๐Ÿ˜ด. Walilala.

---

๐ŸŒ… Asubuhi ilipotia nanga
Garma alikuwa wa kwanza kuamka. Alienda kuoga ๐Ÿšฟ. Alipomaliza alirudi tena chumbani, akajiweka sawa hadi alipomaliza. Kisha akamwamsha Mayner.
โ€œNataka kutoka nawahi kwa designer, utaenda kazini?โ€ alimuuliza.
โ€œHapana, nahisi kama bado nina harufu,โ€ alisema huku akijinusa ๐Ÿคง.

Pua yake ilipokea harufu mbaya, akajikuta akipiga chafya ๐Ÿคง na kumtazama mume wake, ambaye alisema:
โ€œZingatia dawa. Hata hivyo, nitaenda pia kuangalia ukumbi. Nahisi kama nitachelewa kurudi.โ€
โ€œMh! Ila isiwe kama jana โ€” ile ilikuwa ni too much. Kupigwa na baridi muda mwingine kunachosha.โ€
โ€œHahaha! ๐Ÿ˜„ Usijali baby. Lakini zingatia, usitoke. Usiende kwa mganga.โ€
โ€œBaby bwana, mbona unashindwa kunielewa? Mimi na mganga wapi na wapi bwana?โ€ alisema Mayner huku akiweka sura ya kuchukiza kidogo ๐Ÿ˜’.

Garma aliona bora amuage kwa busu ndogo katika paji la uso ๐Ÿ˜˜ huku akisindikiza na neno โ€œNakupenda,โ€ kisha aliondoka. Alifika hadi sebuleni ambako alimkuta Rasma akiendelea na usafi ๐Ÿงน.
โ€œMwangaruka (Habari za asubuhi)โ€
โ€œMwangaruka Wawa, Mola sana (Habari za asubuhi, uko poa?)โ€
โ€œSalama,โ€ walisalimiana kwa Kisukuma huku wakipeana tabasamu ๐Ÿ˜Š.

Rasma alimwangalia kaka yake, akagundua kama alikuwa na jambo alilotaka kuzungumza. Ilibidi amuulize:
โ€œKuna nini, mbona kama kuna kitu hivi?โ€
โ€œNdio, nataka nikuambie kwamba usimruhusu Mayner kutoka hapa. Na endapo akifanya hivyo basi nipe taarifa.โ€
โ€œKwani haendi kazini?โ€
โ€œAnaumwa. Akipona ataanza.โ€
โ€œMh! Sawa, hakuna shida.โ€
โ€œOk,โ€ alisema Garma, na kuanza kupiga hatua ili kutoka nje. Lakini alikumbuka jambo na kusema:
โ€œHalafu nimekumbuka...โ€

Alirudi hadi sehemu ambayo Rasma alikuwepo, kisha akamnongโ€™oneza โ€” hali iliyowafanya wote wacheke ๐Ÿคญ.
โ€œKa fala hivi, nenda huko!โ€ Rasma alisema. Garma akaondoka mahala pale.

Utani ulikuwa ni sehemu ya familia hii. Licha ya kila mmoja kukuwa, Garma hakuacha kumtania ndugu yake. Muda mwingine alikuwa akimtoa na kumpeleka maeneo mbalimbali, ambako walipiga stori kama ndugu ๐Ÿค—.

Kufanya hivi, aliamini kungeimarisha udugu wao. Na hakika alifanikiwa kwa kiwango kikubwa sana, kwani mapenzi ya Rasma kwa kaka yake yalikuwa makubwa mno โค๏ธ.

Baada ya kaka yake kuondoka, alibaki sebuleni huku akitafakari:

> โ€œUsimruhusu Mayner kutoka hapa, na endapo akifanya hivyo basi nipe taarifa.โ€

Ilikuwa ni kauli ya kaka yake iliyopitapita kichwani mwake. Aliwaza โ€” je, kaka yake alisikia nini kuhusu kile walichokipanga na Mayner?

Wakati anaendelea kuwaza ๐Ÿค”, mama yake alitokea huku akiwa na tabasamu la kasi ๐Ÿ˜.
โ€œUnawaza kwenda kwa mganga na huyu mwenzako enh?โ€ aliuliza Mama Garma.
โ€œNani amekuambia?โ€
โ€œKhe! Kwani nani hajui kwamba huyu mwanamke ni mchawi? Unadhani sijui? Sasa wewe jifanye unapeleka peleka watu kwa waganga โ€” ufe huko huko, shauri yako!โ€ Mama Garma alisema kisha akarudi zake chumbani ๐Ÿšช.

Rasma alibaki njia panda ๐Ÿ›ค๏ธ, akiwa amechanganyikiwa na kukosa uelewa wa kile kilichokuwa kinaendelea. Aliwaza โ€” ni nani alimwambia mama na kaka yake kuhusu mganga? Mwisho aliamua kwenda kumuuliza Mayner.

Alipiga hatua hadi chumbani kwake, akagonga mlango na kujitambulisha. Mayner alimruhusu kuingia.
โ€œAsubuhi sana... kuna nini?โ€ aliuliza Mayner huku akijiweka sawa.
โ€œMama amejuaje kama tunataka kwenda kwa mganga?โ€
โ€œMh! Mwenyewe sijui kwa kweli. Usiku alikuwa akiongea na kaka yako... amemchimbia mkwara mpaka nikasema labda wewe ndio ulisema.โ€
โ€œAku! Niseme wapi? Ila sikia, twende tu. Jiandae nami naenda kujiandaa.โ€ alizungumza Rasma.

Mayner alifikiria kidogo kuhusu aliyosema mume wake usiku na asubuhi. Aliona bado hana uhuru wa kuondoka, hivyo alikataa ๐Ÿ™…โ€โ™€๏ธ.
โ€œMimi ndio mlinzi mkuu hapa, najua kila kitu. Kaa kwa kutulia, tuondoke zetu. Utabakia kuumwa hadi lini? Ugonjwa sio wa kawaida huo!โ€ Rasma alimsisitiza.
โ€œKwa jinsi ambavyo natoa harufu hivi... itakuwa ni kile chupi nilichopigwa nacho usoni?โ€ aliwaza Mayner, na mwisho akaona hana namna zaidi ya kukubali kwenda kwa mganga ๐Ÿ™ˆ.

Baada ya kukubali, Rasma aliondoka kwenda kujiandaa. Huku naye Mayner akibadilisha nguo na kwenda kuoga ๐Ÿšฟ. Dakika 50 zilitosha kwao kufanya kila kitu. Walikutana sebuleni.

โ€œMnataka kwenda wapi?โ€ lilikuwa ni swali la Mama Garma, ambaye alisimama kwenye korido ๐Ÿšถโ€โ™€๏ธ.
โ€œUshaanza maswali yako?โ€ aliuliza Rasma.
โ€œNataka kujua. Na kama kwa mganga basi msiende! Litakalotokea, mtajua wenyewe.โ€
โ€œBwana, usitutishe. Ebu tuondoke, Wizo!โ€ Rasma alimshika mkono Mayner ๐Ÿค na wakaondoka mahala pale, wakiwa na matumaini kwamba sehemu wanayoenda watapata msaada wa kuelewa nini kinamsumbua Mayner.

Baada ya kuondoka, Mama Garma alirudi chumbani kwake. Akachukua simu iliyokuwa kitandani ๐Ÿ“ฑ, akaichezea kidogo na kuweka sikioni.
โ€œTayari wameshatoka. Ndio... jukumu ni lako. Utachagua afe nani. Kama ni wote, hakuna shida. Ila itapendeza kama huyu anayeitwa Mayner huyu akafa.โ€ alisema kama akimpa maelezo mtu ambaye hakujulikana ni nani, kisha akakata simu... ๐Ÿ“ด

ITAENDELEA... ๐Ÿ”ฅ

Tupo kwenye dunia huru na salama zaidi. Raha ya kununua ipo pale ambapo muuzaji anakuambia, Lipia kwa pesa unayotaka. Leo, simulizi hii unaweza kununua kwa pesa yako mwenyewe. Nitext WhatsApp, namba ni 0717255498. Nunua kwa pesa yako..
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

ALIFIRISIKA BAADA YA KUACHANA NA MKE ALIYECHUMA NAYE MALI | EP 11  >>> https://gonga94.com/semajambo/alifirisika-baada-ya-kuachana-na-mke-aliyechuma-naye-mali-ep-11
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

gonga94 official track
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
offa ya msimu wa nanenane
offa ya msimu wa nanenane

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest