Baada ya masha kulivuta koti akahisi kuna kitu kwenye mfuko wa koti akamwambia Vicky hii ninii?? Huku anaingiza mkono mfukoni kutazama
Akakutana na saa nzurii Masha alipo iona tu aliijuaa hii kitu ni pesa ndefu sana yeye ni mdada wa mjini..
"Hii saa ni ya gharama kubwa sana bei yake ni zaidi ya Dola Milioni umeitoa wapiii"
Vicky akashangaa saa?? moyoni akawaza itakuwa yule kijana mjinga aliemnaniliu ndio kaiweka hiyo saa humoo kwenye kotiππ
Vicky baada ya kuwaza hivo Akamwambia masha embu nipee hiyo saa masha akamwambia hapana huwezi kuwa na saa ya gharama hivii halafu hii ni fake sio orginal "
Masha akavaa ile saa mkononi huyoo akaondoka zake, Vicky akabaki bado anajikokota mana hata kutembea hakuwa anaweza alikuwa na maumivu sanaaa
Masha alipo toka tu nje alikutana na Gari moja imetuliaa ya bei mbayaa , Tanzania haipoo sasa si unajua yeye anajua mambo ya Tofauti kidogo kwahiyo alipo iona ile gari akabaki kuishangaa hee hii gari ya wapi mbona gari ya hela sanaaa??
Akasogea karibu ili apige Self na gari ajiuzie zake sura mtandaoni
Na huku sasa kwa yule msaidizi wa Mr Alberto , Yeye alibaki Tanzania ili kuendeleza Taratibu zingine na kukamilisha kabisa miladi ya Boss wake ambaye ni alberto ,
yeye ndio aliachiwa kazi ya kumtafuta Mschana ambae mr Alberto anasema amemsaidia sana , kitambulisho ilikuwa ni koti na Saa ya Boss wake
sasa yule msaidizi wakati yuko kwenye harakati zake ghafla kwa mbalii akaona mtu yupo bize ana shika shika gari yake π³
Kuangalia kwa makini mkononi ana saa ya Alberto na koti alilovaa ndiyo hilohilo aliloelekezwa na Alberto.. nazani ni huyu binti ndo alomsaidia boss wangu..
Akamfata haraka akamwambia Madam habari yako, bila shaka sjakosea ... mimi ni kijana wa mr Alberto nipo hapa kumuwakirisha kwako
Sasa masha hakuwa anaelewa akabaki kushangaa mbona anapewa heshima za gafla lakini kabla hajaongea neno yule kijana aliendelea...
Na boss anaomba radhi kwa alichokifanya haikuw kusudio lake hivyo ameagiza niwe karibu nawewe na nikupatie mahitaji yote muhimu utakayohitaji kwa sasa mpaka siku zijazo hadi atakaporudi "
Yule kijana alikuwa anaongea kwa utulivu na kupangilia maneno yake heshima pia katika maongezi yake ilikuwa na kipaumbele zaidi kifupi alivutia hata kusikiliza .....
Masha alipo sikia jina mr Alberto akakumbuka wakati anamuilizia Vicky pale mapokezi aliambiwa yupo chumbani kwa Alberto,
kabla hajafika mbali akasikia wale wafanyakazi wanaongea habari za Mr Alberto kuwa ni Tajiri sanaa halafu mdogo mkaka na Pia ni Bonge la Handsome
Masha ana akili ya haraka haraka kwahiyo akakumbuka Vicky alimkuta kama kweli hayupo sawa na macho yake yalionesha kabisaa ametoka kulia sanaa
Lakini hata hakumjalii ni mtu ambae pia alishamchosha ni basi tu mama yake ndio anang'ang'ania vicky kuendelea kuishi hapo kwao bila hivyo angekuwa ashamtimua kitambooo
Sasa masha akabaki kuumiza kichwa Vicky amefanyiwa niniii??
Hapo kichwani Tayari Tamaa ilikuwa ishamsimama swala la kusema et sio yeye hakuwa hata na mpango huo kabisaaa ...
Masha akabaki kufikiria kwa sekunde, msaidizi wa Mr Alberto akahisi kama hajatoa maelezo yanayo faaa
Akamwambia tena
" Naitwa Rahul ni Msaidizi wa Mr Alberto ,Anaomba Radhi kwa...."
"Haina hajaa mwambie nimemsamehee lakini Kwa..yaan lazima police wajue " masha akaanza kulia
Rahul akamchukua haraka akamuweka ndani ya gari akaanza kuongea nae kwa utulivu huku anamuombea samahani Boss wake akamsihi sana masha asiende huko police kumshtaki
Rahul akamwambia Masha Alberto anasumbuliwa na ugonjwa wa hisia humkuta mara chache sana kwa miaka na hiyo ndio kama Tiba yake
Masha akasema napata faida gani kama nisipo kwenda kushtakii??
Rahul akamwambia nimepewa Kibali cha kukupa kila kitu unachohitaji nitakuhudumia chochote kile utalipwa kiasi kikubwa cha pesa na kila kitu ...
Masha akatabasam kwa mbali hakuonesha kwa rahul akasema moyoni asante mungu mbona kirahisi sanaa hivii
Akakubali akamwambia Rahul sawa nimekuelewa ukienda kinyume takwenda kukushtaki police nyie wote na huyo Sijui Alberto yupo wapi
Rahul akamwambia amerudi nyumbani mara moja atachukua muda kidogo kuja tena huku Tanzania ...
Wakati Rahul anaondoa gari hapo , ndio muda ambao Vicky alikuwa anatoka ndani ya hotel taratibu anajikokota kuondoka hapo
Je itakuwaje??
KWETU morogoro.