Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Pyar Ho Jane Dushman

KISASI KILICHOZAAA MAPENZI🥰🥰 EP 01)

27th Jul, 2025 Views 28


Story na Nash
Tsap 0773792227

(Location; Kigali, Rwanda)

Japo mvua ilikuwa inanyesha lakini Paulina alimhimiza Binti yake waongozane sehemu aliyokusudia 😒😒😒

"Mama, mvua ni kubwa kwanini tusisubiri ikatike kwanza😒" Mariah alizungumza kwa sababu hawakuwa hata na mwamvuli🙄🙄.

Kitu kingine alikuwa na uchovu kupita kiasi usiku wa jana alikesha akitumbuiza😇😇 kwenye Casino linalojulikana kwa jina la SUPER IVY😇

"Acha kuwa msumbufu, tembea🤨🤨" Paulina alizungumza huku akiongeza kasi kwenye miguu yake hakujali kama binti yake kavaa chupi na tisheti kubwa🙄

Mariah alimfuata Mama yake kwa nyuma.😒😒
Radi na ngurumo zilivyo sikika alijificha nyuma ya Mama yake😔😔

"Mwanamke kabisa unaye tarajia kuitwa Mama miaka ijayo unajificha kwenye mgongo wa Mama yako🤥! hakika wewe ni kichaa🤨" Paulina alizungumza kisha akaendelea kutembea😌

Mariah alizidi kumfuata nyuma asielewe wanaenda wapi🙌🏾. Magari waliyopishana nayo yaliwarushia tope🤥....

"Tunajitahidi kukaa mbali lakini bado wanaturushia tope☹☹" Mariah alilalamika akionekana kukasirika

"Acha kuongea sana nifuate tumekaribia kufika🧐🤔...." Paulina alizungumza

Baada ya dakika 25 kupita walifika sehemu wakasimama🙌🏾.

Mariah aliangalia sehemu waliyosimama kwa umakini mkubwa akafanikiwa kuona bonge la nyumba😬😬, hakuelewa kwanini Mama yake kamleta sehemu hii.🙄

"Hii nyumba kwa kukadiria unahisi imegharimu kiasi gani cha pesa🤔🤔" Paulina aliuliza

"Laki tisa😬...." Mariah alizungumza bila kufikiria

"Pumbavu🤨! kwa jibu lako hilo inaonekana unawaza kumiliki laki tisa maisha yako yote😏😏....naomba uangalie kwa umakini muonekano wa nyumba hii kisha uniambie ni kiasi gani cha pesa kitakuwa kimetumika🤔🤔'' Paulina aliongea huku akimtazama Mariah kwa macho yaliyobeba msisitizo🧐

"Milioni 450🤔🤔....." Mariah alijibu bila kufikiria ni vile tu macho ya Mama yake yalimtisha😥

"Umekosea kidogo nitakusahihisha🙄, milioni 500 zimetumika hapa🤔🤔" Paulina alizungumza akionekana kuwa na machungu😥😥

"Kwanini umenileta hapa🤔" Mariah aliamua kuuliza

"Hii nyumba ilikuwa ni ya kwetu ila sababu ya upumbavu wa Baba yako alibadilisha kila kitu akampatia Mwanamke😒😒.....nilifukuzwa sehemu hii nikiwa na ujauzito wako😥, mpaka sasa tunaishi maisha magumu sababu ya Mwanamke anayeishi humu ndani☹" Paulina alizungumza

Mariah aliamini Mama yake anaumwa akili kwa sababu tangu jana usiku hakuwa akimuelewa kabisa🧐

"Mama naomba tuondoke🥺...." Mariah alishauri

"Hii nyumba imeghalimu milioni 500 halafu unataka tuondoke tena bila hata kuuliza maswali mengi😳😳! hivi wewe ni mwanangu au nilibadilishiwa hospitali😥! hii ni nyumba yetu Mariah😔😔" Paulina alizungumza huku machozi yakimtiririka 😪

Baada ya Mariah kuona machozi kwenye macho ya Mama yake alielewa anamaanisha🥺

"Mama, milioni 500 ni pesa nyingi sana🙌🏾.... inawezekanaje sisi tuishi maisha magumu wakati unadai hii ni nyumba yetu😥😥 " Mariah aliuliza

"Sasa naona umeanza kuwa na akili🤔, hayo ndio maswali niliyotegemea uniulize😒" Paulina alizungumza akajifuta machozi kisha akamshika mkono Binti yake😔

"Kabla sijaingia kaburini naomba uirudishe hii nyumba mikononi mwetu😪😪....ndani ya hiyo nyumba kuna Kijana mzuri naomba ufanye juu chini awe rafiki yako🙌🏾. Wanawake na Wanaume ni watu dhaifu sana katika mapenzi endapo utafanikiwa kuuteka moyo wake kila kitu kitakuwa chetu🤨🤨"

"Bado sijaelewa hadithi yako🧐...." Mariah alimuambia Mama yake

"Ulisema unaweza kukimbia umbali mrefu bila kuchoka si ndiyo🤨? basi naomba uende sehemu anayouza karanga Mjomba wako🤌....muombe akusimulie kuhusu hii hadithi nina imani kubwa utamuelewa yeye kuliko Mimi🧐" Paulina alizungumza

Mariah alikuwa na shauku ya kujua kila kitu hivyo aliondoka kwa kukimbia mpaka sehemu anayouzia karanga Mjomba wake😟😟.

Alisimuliwa kila kitu kama alivyoomba🤌....machozi ya uchungu yalimtiririka kwa uchungu😥😥.

Kwa haraka aliweza kuelewa kwanini Mama yake kawa mtu wa hasira muda wote☹☹. Laiti kama Baba yake angekuwa hai basi angemkata kata panga kisha akatokomea na Mama yake kusikojulikana🙌🏾.

"Kwahiyo Kampuni la green tea ni la kwetu🤔🤔?....yaani hizo mali zote ulizonitajia kwa haraka haraka zote ni zetu🤨?...kwanini Baba amthamini kupita kiasi mtoto wa mchepuko ambaye siyo hata damu yake🙌🏾!..." Mariah alilalamika

"Nina uhakika mkubwa Baba yako alimpenda Mama yako kupita kiasi🤌. Yule mchepuko alitumia nguvu ya ziada kumlaghai Baba yako🤨🤨. Sijui ni kwanini Mama yako kaifufua hii hadithi iliyokwisha kupita🙌🏾. Naomba usifanye kitu chochote🤌" Mjomba aliongea

Mariah aliondoka bila kuongea chochote😥, anafika nyumbani kwao akiwa kalowa tepe tepe☹☹.

Paulina alimuonea huruma Binti yake kwa namna anavyo huzunika😥😥

"Kama si ujinga wa yule mchepuko🥺, Kampuni la green tea lingekuwa chini yako🥺, cha ajabu umeishia kuwa mwimbaji wa Casino😥"

"Mama naahidi kurudisha kila kitu kilicho chetu mikononi mwetu😥..... nitahakikisha huyo mchepuko na Kijana wake wanaishi maisha magumu kuliko hata ya kwetu🙌🏾" Paulina aliongea kisha akaelekea chumbani kwake kubadili nguo🧐.

Muda wa kwenda kazini ulikuwa umewadia🤔. Hakuona sababu ya kupumzika ile anataka kufungua mlango Mama yake alimsubirisha🙌🏾

"Hii ndio picha ya mtoto wa Mchepuko🙌🏾, jina lake anaitwa Max😒. Kama Mama yake aliweza kumshawishi Baba yako mpaka akatusahau sisi jitahidi kumshawishi pia aweze kukupatia kila kitu chetu🙄🙄"

Mariah alipokea picha akaiweka ndani ya begi lake😒, alimuonesha Mama yake tabasamu kumaanisha kila kitu kitakuwa sawa🙌🏾

Paulina alimsindikiza Binti yake kwa macho ya huruma😔😔....kazi anayoifanya ni ngumu kuliko zote😥. Lakini ili waweze kula ni lazima Mariah akawaburudishe watu kwenye Casino la IVY☹☹.

🎵Chai ya maajabu imegundulika,
tumia kwa Mwanaume tajiri
Kama ni masikini achana naye mwaya atakusumbua tu🎵
Mariah aliimba wimbo huu huku akicheza kiuno chake😅😅😅

Nje ya Casino hili Max, CEO wa kampuni kubwa ya green tea, alipark gari lake😌. Alikuja mahali hapa kupumzisha ubongo wake kutokana na uchovu wa kazi🙌🏾.

Kitendo cha kugusa mlango wa Casino la Ivy, alikutana na sauti ya Mariah😌😌. Alivuta kiti chake kisha akakaa🙌🏾 ....akili yake yote aliielekeza kwenye wimbo wa Mariah😅😅

"Chai ya maajabu!" Max alijisemea huku akishushia wine🍷

Itaendelea

Nash stories
Tsap 0773792227
Full 1000.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

KISASI KILICHOZAAA MAPENZI🥰🥰 EP 01)  >>> https://gonga94.com/semajambo/kisasi-kilichozaaa-mapenzi-ep-01
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Pyar Ho Jane Dushman
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
offa ya msimu wa nanenane
offa ya msimu wa nanenane

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

SEHEMU YA 32💘💘

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

majario rewards 100 Comments 0
 

SEHEMU YA 30💘💘

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest