Safari ya kina Mayner iliishia Magu, ambako walienda hadi kwenye moja ya nyumba iliyokuwa inaonekana kama kibanda, ikikaliwa na bibi mzee. ποΈ Walipofika, walivua viatu na kuingia ndani.
Kwa Mayner, hii ilikuwa mara yake ya kwanza kwenda kwa mganga wa jadi, hivyo alijikuta akijawa na hofu na wasiwasi. π Muda wote alichunguza mazingira ya ndani kwa tahadhari. Akili yake ilimwambia huenda angeliwa na mizimu, lakini haikuwa hivyo.
"Mnaweza kukaa hapo chini," alisema mganga huku akiwaonyesha mkeka uliokuwa umechoka mno.
Mkeka huo ulikuwa makazi ya viroboto na kunguni, kama ungefika ukiwa mchafu, basi usingepona. Lakini kama ungekuwa msafi, basi usingengβatwa. Mkeka huo pia ulitumika na bibi mzee huyo kama βkiooβ cha maisha yake. πͺ²π§Ό
Baada ya kukaa wote kwa pamoja, Mayner alianza kujikuna sana. Mwili wake ulitoa marenge renge na alijuta kukubali kukaa kwenye mkeka ule. Alijaribu kuinuka lakini alizuiliwa na mganga.
"Kaa tu, hata usitoke," mganga alisema.
"Wananingβata, na mwili wangu muda wote unawasha!" π
"Najua. Ndio maana nakuambia ukae. Wewe binti, njoo hapa," alimwambia Rasma, ambaye aliinuka na kukaa pembeni.
Kimya kilitawala. Mayner aliendelea kujikuna bila mafanikio, na ghafla mganga alivunja kimya kwa sauti ya mamlaka:
"Wewe ndio mwenye matatizo β tena makubwa sana. Ni bahati tu kwamba umefika, la sivyo ungekufa!" π§π½ββοΈ
"Kufa?!" aliuliza Mayner kwa mshangao.
"Ndiyo. Unatafutwa kila siku. Kuanzia kipindi cha mimba, walitaka wakuuwe, na siku ya kujifungua wakakosa, wakampata mtoto wako. Sasa wanakutafuta tena β na safari hii wanataka wakumalize kabisa!"
Rasma alisikiliza kwa makini. Kila neno lilichunguzwa na akili yake kwa kina.
"Kina nani wanataka kuniua?" aliuliza Mayner.
"Familia ya mumeo. Hawataki kukuona ukiwa na binti yao." π
"Mama yangu?" Rasma aliuliza kwa mshangao.
"Ndiyo. Mama yako anaongoza mpango huu. Lakini hawakuwezi. Wameshindwa kukuua na sasa wanakutesa hadi ukate tamaa mwenyewe."
"Kwa nini wasinimalize tu? Si bora nife nijue moja kuliko mateso haya?" Mayner alisema kwa uchungu huku machozi yakimdondoka. π’
Taarifa hizo zilimvunja moyo. Nafsi yake ilisinyaa na uso wake ukaonyesha huruma ya hali ya juu.
"Kinachokulinda ni mizimu ya kwao Kigoma β wazazi wako. Lakini kwa sasa mizimu hiyo imeanza kuchoka," alieleza mganga na kusogea kwenye kaniki aliyotandika chini.
Ndani ya ile kaniki kulikuwa na kioo kidogo, lakini kilitosha kuonesha picha. Mganga alichuchumaa na kusema:
"Njooni hapa kwa kutambaa."
"Wote?" Rasma aliuliza.
"Ndiyo, wote."
Mayner, aliyekuwa amechoshwa na viroboto, alifika kwanza na kukaa kitako. Rasma alifuata na wakamuweka mganga katikati.
"Hiki ndicho kilichokufanyiwa," mganga alisema huku akionesha picha ndani ya kioo.
Kwenye kioo, walimuona Mama Garma akiwa na Ninah.
"Mpango huu wa kumuua Mayner unaongozwa na mama huyu. Anataka binti huyu akae nyumbani kwake. Anapendwa na mizimu zaidi yako. Anajua ukifa, mali ya mtoto wake hutarudi kwake pekee β bali nawe utadai. Hiyo ndiyo sababu."
Mganga aliendelea kuonesha video ya daktari akimchoma mtoto wa Mayner sindano β tukio ambalo liliashiria kwamba mtoto hakufa kwa kawaida.
Kisha aliionesha video nyingine ya mtoto akitikiswa vibaya siku aliyokuwa akioga na mume wake. πΆπ½π
Mayner alizidi kulia.
"Nimemkosea nini mimi mama yako? Nimemkosea nini mimi?" π
"Hana sababu. Hilo ni hasadi. Suluhisho ni kutoka kwake β sahau kuhusu mtoto wake. Mizimu yako imechoka, ukibaki utakufa," alisema mganga kwa msisitizo.
"Kwahiyo unamaanisha niachane naye?"
"Ndiyo jibu lake."
"Na ndoa je?" Rasma aliuliza.
"Haina maana. Ukiolewa tu, unateketea. Ngoja nikuonyeshe mtego uliopo mbele."
Alionesha video ya mwanamke aliyeungua kwa moto mbele ya umati bila msaada wowote. π₯
"Ulishawahi kuiota ndoto kama hii?"
"Ndio..." Mayner alijibu kwa sauti ya chini.
"Sasa nenda kahame. Anza maisha mapya. Na wewe binti, chukua hii dawa," mganga alimpatia Rasma dawa ya maji kwenye chupa ndogo.
"Nifanyaje nayo?"
"Weka chini ya mto kila usiku. Ukisahau tu, jua yatakayokupata. Na wewe Mayner, hii ni ya kusafisha sehemu yako ya siri," akampa pia dawa yake.
Mayner alikunywa dawa ile huku akitetemeka.
"Mnaweza kwenda. Mkikosea masharti, mtajua."
"Mimi langu ni kuhama tu?" Mayner aliuliza.
"Ndiyo. Dawa uliokunywa itakusaidia kujisafisha. Kila la heri," alisema mganga.
Wakaondoka. Lakini moyoni, Mayner alihisi huzuni. Je, ataweza kuishi bila mume wake? β€οΈβπ©Ή
Wakiwa ndani ya gari maeneo ya Kisesa, Mayner alisema kwa sauti ya huzuni:
"Mi naona bora nibakie tu pale pale..."
Sauti hiyo ilimshtua Rasma aliyekuwa tayari kufunga breki.
"Usiwe kichaa, utakufa!"
"Nawezaje kuishi mbali na Garma? Inamaanisha ndoa yangu imeisha. Basi nife tu kuliko kuachana naye!" π
Aligeuka upande mwingine wa kiti na hakutaka kusikiliza kitu tena. Rasma aliendelea kumsemesha, lakini Mayner alikaa kimya...
ππ¨ ITAENDELEA...
Tupo kwenye dunia huru na salama zaidi. Raha ya kununua ipo pale ambapo muuzaji anakuambia, Lipia kwa pesa unayotaka. Leo, simulizi hii unaweza kununua kwa pesa yako mwenyewe. Nitext WhatsApp, namba ni 0717255498. Nunua kwa pesa yako..