Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

NIPE YOTE DADY SEHEMU YA 44

27th Jul, 2025 Views 79



Tulikaa na kuanza kula hapo anajifanya kuwa na mahaba nikawa namuangalia tu , tulimaliza kula nikatoa vyombo na kupanda kitandani , kichwani niliwaza kufanya nilichokusudia nikaona hapa tunaweza kugombana kwahiyo kuepusha ugomvi inabidi nitumie njia ya kiutu uzima.

Alipanda kitandani na kuanza manjonjo ya kutaka chakula cha usiku ,nikaona nitumie njia hiyo kujua alikuwa wapi.

Basi bwana nikampa ushirikiano vizuri mchezo ulipoanza nikashika usukani na kuanza kulipeleka gari kiufundi zaidi ,mtoto wawatu utamu ukamkolea nikaongeza viungo mpaka ikafika mda akaanza kunena hapo sasa nikaona niulize maswali yangu huku nikiwa na uhakika hawezi kuicontro akili yake kwa wakati huo.

Bwanaee nilivyouliza huku nikiendelea kuzungusha na kuweka manjonjo yakwenda kijana akatubu kuwa alikuwa na Nasra aloooh , nilichomoa fasta na kukaa pembeni akanifuata huku akiuliza shida nini mbona nimezima gari ghafla tena katikati ya safari.

Nilimuangalia kwa hasira na kusema "Selim nikitu gani nimekosa mpaka kufikia hatua unafanya hivi, we niwakutoka na Nasra bila kuniambia na mlikuwa mnafanya nn hadi ukawa unashindwa kupokea sm zangu?"
Alikaa pembeni yangu kwa taratibu na kuongea kwa Sauti ya upole akasema "Norah mke wangu nisamehe lakin haiko kama unavyofikilia , nikweli nilikuwa nae ila sikuwa nikifanya chochote cha tofauti kwani nakuheshimu sana ."

"Selim unajua sipendi siri na uongo na hili tulishaliongea toka mwanzo wa mahusiano yetu sasa leo unafanya hivi kwann ,hivi unafikili kuna kitu unachoweza kuongea nikakuelewa? au unadhani nitafikilia nini kama sio kuwa nyie wawili mna mahusiano "

"Hapana mke wangu sio hivyo siwezi kufanya kitu kama hicho "

"Hapana nini Selim hivi unafikili mimi leo ndio jingefanya hivi unafikili ungefikilia nn wewe ,yani nakupigia sm zaidi ya mara nne hupokei na hata ulivyoingia kwenye gari hukunipigia
Nabado nakuuliza unanificha unaona nisawa?"

"Naelewa mke wangu ila sikutaka kukwambia kwasababu
Alinitaka nisikwambie chochote " aliinuka na kuchukua sm akanionesha meseji alizomtumia Nasra , nikweli alimuomba waonane na akasema nisijue kwasababu nijambo private .

Nilisoma zile text zote kisha akanisikilizisha na record ya maongezi yao nikasikiliza kwa makini kisha nikamwambia ugomvi umeisha ila zile text na voice zote nikahamisha kwenye sm yangu, nilivyomaliza nikapanda kitandani kimyaa na kulala nikamuacha Selim akiomba msamaha .

Kesho yake asubuhi niliamka mapema nikaanda chai na kuwaandaa watoto wakaenda shule , Selim nae aliamka akajiandaa tukapata chai pamoja hapo bado anaomba msamaha mimi jibu langu moja tu ugomvi umeisha baasi.

Tulimaliza kunywa chai akatoa vyombo na kuviosha yani yote hayo nianataka kusamehewa πŸ˜ƒ hakuishia hapo akachukua pochi yangu na kubeba tukatoka mlango nao nikafunguliwa mie kimyaaa .

Basi tukaingia kwenye gari safari ikaanza mpaka chuo kabla sijashuka nikamwambia"Ukirudia ulichofanya jana talaka saba zinakuhusu"

"Sirudii tena mke wangu nimekoma kabisaaa naapa sirudii tena "
Alivyojibu nikashuka na kuondoka moja kwa moja tunapokutania na Amaira .

Nilifika tukasalimiana kisha nikakaa akaanza kusema " Shoga yangu nina ubuyu "

"Unaonekana mh sema nini kimetokea"

"Subiri kwanza mbona unaongea kipole ushapigwa tukio nini"

"Wakupigwa tukio awe mimi embu ongea huko unanijaza mate tu"

"Huna lolote nimeshakuona hauko sawa sema ngoja nikupe huu ubuyu,hivi unajua kama Naira amekubali kuolewa "

"We Naira amekubali ? kwani wamemfanya nini mtoto wawatu mpaka akakubali'"

"Mwenyewe nashangaa imekuwaje maana jana ulivyoondoka alibaki anasema hawezi kamwe sasa nashangaa mchana naongea nae akasema amekubali "

"Hamna hapa kuna kitu we subiri uone sidhani kama Naira anaweza kuchukua maamzi kama hayo "

"Ila sidhani kama kuna kitu nawasi wasi na baba yake anaweza kuwa kamtisha mpaka akakubali "

"Kwajinsi unavyomuona Naira ni mtu wakutishika na maneno ya baba yake , we tulia mimi ninaukakika atakuwa anajambo lake sema na wewe hujui namna ya kuongea nae vizuri."

Tuliongea kwa mda kisha tukaingia kwenye kipindi kama kawaida,sasa siku hiyo jioni huwa tunakutanaga wote kwa pamoja yani mimi Naira Amaira na Ney .

Na huwa tukikutana tunaweka mada mezani kila mmoja aongee mambo yake ili kama kushauriana tushauriane ,na mengine mengi basi jioni ilipofika kama kawaida tukakutana sehemu kwanza tukaagiza kila mtu anachotaka kisha tukaanza kupiga story .

Kama kawaida nikaanzisha "Mh Naira kulikoni dada umekubali kuolewa wakati ulishakataa na inakuwaje ukubali kuishi maisha na mtu usiempenda au unadhani movie la kihindi ee!?"

"Kwamna mvyoniona mnahisi naweza kukubali huo upuuzi ?" tuliangalia kisha Naira akakaa kimya Amaira akaongea "Sasa kama hutaki mbona umekubali au kuna kitu umepanga ?"

Naira alitabasamu na kusema "Kweli hamjui kunisoma ,sasa wapendwa iko hivi baba sianajifanya anatamaa na hela alafu na huyo mpuuzi Dully sikaona amenikomoa sana ee ,sasa nitawafanyia mchezo hawata amini maisha yao yote we ngoja "

nilitaka kuongea Ney akaniwahi kwakusema "We da Naira kama humtaki endelea kukataa usije kufanya kitu kibaya mwisho ukaingia kwenye matatizo
Naira alichukua glass akapiga fundo moja la juice kisha akamjibu Ney "Dada hiyo hainihusu yani nilichopanga kufanya itakuwa fundisho kwao hivi kwann tulazimishane kuolewa wanafikili ndoa ni lelemama ?'"

Nilikaa vizuri na kumuuliza Naira " Haya achana na vitu vibaya ,mh umepanga kufanya nn maana hapa nimejaribu kuisoma akili yako ila nimeshindwa "

Aliniangalia kwa tabasamu nono na kusema .

.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

NIPE YOTE DADY SEHEMU YA 44  >>> https://gonga94.com/semajambo/nipe-yote-dady-sehemu-ya-44
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

majario rewards 100 Comments 0
 

A.J.A.D SE03 EP02

majario rewards 100 Comments 0
 

Simulizi: MAPEPE **

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest