Kila mtu alikuwa anashangaa mambo ya masha kubadilika gaflaa maisha yamemnyookea kama uyoga unaota Tu kwa sec chake
Vicky alitoka nje hakuwa hata na mood ya kusherehekea
Rahul nae alitoka nje alikuwa anahitaji kuvuta sigara
Wakati anawasha sigara akamuona Vicky amekaa pembeni ya bwawa la kuogelea
Taratibu Rahul akamfata ,
"Naweza kukaa nawe"
"Yeah , kaa.. karibu kaa...aah" Vicky alifuta machozi haraka haraka
Rahul.akaona akamuuliza unalia?? Vicky akasema Noo ni baridi tu na huu upepo ,, huku anajichekesha chekesha
Rahul akatoa Big G akampa huku anamwambia , haupo sawa eeh nimekuona kama unaumwa hivii!?
Vicky akasema hapana mie hata siumwi ,rahul akamwambia kama utahitaji mtu wa kuongea nae mie nipo hapa
Vicky akamjibu sawa usijali , rahul akainuka kabla hajapiga hatua aligeuka akamuuliza Vicky
"Masha ni dada yako??"
"Ndio "
Rahul akacheka kidogo akawasha sigara yake akaondoka hapo , Vicky nae aliinuka kurudi ndani
Gloria alikuwa analia mama yake yupo bize na sherehe hata hakuwa anamuwaza mtoto
Vicky ikabidi amchukie ili ampeleke kwa mama yake ,
Wakati amembeba anapiga hatua kwenda alipo masha , masha aliona na akajua kabisa analetewa mtoto
Akachukua chupa ya pombe aliyokuwa ameshika akampa rafiki yake akaanza kuja upande wa Vicky na muda huo Rahul nae akawa ametokea
Vicky akamwambia nilikuwa nakuletea mtoto analia , Rahul akamuuliza masha kumbe una mtotoo???
Sura ya Rahul ilionesha mshangao ambao hata masha aliuona akacheka akasema sio wangu bwana ni mtoto wa Vicky
Haya nenda kwa mama G eeeh mie nipo bize kidogo"
Hee !!! Vicky akabaki mdomo wazi hata mama yake aliona Vizuri jinsi masha alivyomkana mtoto wake
Wote wakabaki mdomo wazi ,masha alikuwa anajichekesha chekesha sanaaa
Rahul akakumbuka wakati anaongea na Alberto alimwambia kuwa mschana huyo amemkuta akiwa bkr yeye ndio amemfungua..
Ndio sababu kidogo Rahul alishangaa kuona huyo Bkr et anamtotoo
Masha nae anamachale akaruka chap ...
Vicky ikabidi tu atoke na huyo mtoto nje mana alikuwa analia sana , mama yake akamuita pembeni akamuuliza wewe masha unaakili kwanini unakataa mtoto ??
"Mama jamaniii ,.mambo ndo kwanza leo yameanza mtu aanze kuona mizigo embu tulia basi huyo ni mwanangu tu kwani nikisema sijamzaa ndio inakuw kweli sijamzaaa ??"
"Jamani we mbona unavuka mipakaa sanaa "
"Mama usiniharibie siku embu malizeni mwende kwenu"
Mhu ...
Mama yake alisikitika tu mana mtoto ndo wake hana pa kumpeleka , Vicky aliona hawezi kukaa hapo tena kwanza yupo bored sana
Aliamua kuondoka bila hata kuaga wakati anatoka getini Rahul akamuona akamfata akamuuliza unaenda wapi Vicky
akasema naenda hom akamwambia kwanini .. aah nimechoka tu kuwa hapa nataka nikapumzike .. okey naweza kukupeleka kama hutajalii...
aah bwana ahsantee hata usijali mie nitafika ....hapana nataka kukupeleka mimi tafadhalii ... jamaniii hayaa ...
Rahul alijikuta tu anamkubali Vicky mana hafanani hata kidogo na mashaa kwa tabia mpaka muonekano
Vicky na G wakapanda kwenye gari la Rahul ,
Rahul hakuwapeleka nyumbani aliwapeleka kwanza kwenda kula story za hapa na pale
Vicky nae akajikuta amemzoea Rahul
Rahul akamuuliza baba wa huyu mtoto yupo wapi Vicky akacheka tu akwambia ipo siku utamuonaa hata usijali ,
Baada ya kula Rahul ndio akawapeleka moja kwa moja na tayari ilikuwa usiku , rahul akawaacha na kuondoka zake ...
Siku iliyofuata Masha alikuja nyumbani kwao akamwambia Vicky nataka tuongee na wewe ,,,wakatoka nje wawilii
Masha akamwambia "nishamjua aliekubk Vicky "
Vicky alishtuka zilikuwa taarifa kidogo za kutisha kwake hakuwa anazifurahia hata kidogo
"Sitaki kumjua masha achaa ilhal naishi mwache wala sihitaji "
"Yaan wewe bwana kwahiyo kwa vile sio tajili ndio humtaki enhee ila ulivyokuw unajua ni yule Tajiri mbona ulimtaka?? Au ulitaka ulipwe pesa eeh???"
Vicky akatabasam kidogo kwa uchungu
"Sipo hivyo mashaa ,Wala sihitaji tu kumjua"
"Hahah sasa kwa taarifa yako ni yule mlinzi yule anaekutaka wewe kila siku ndio hiyo siku baada ya mtu aliechukua chumba kuondoka yeye alijua wazi utakwenda pale kusafisha
ndio sababu aliingia ndani kukusubiri polee dadaa bora hata ungemkubali kuliko amekula tunda buree heheheh hayaa kwaheriii"
Masha akaondoka zakee, Vicky kichwa kama kilianza upyaa kumuuma et aliemnaniliu ni mlinzii?? Mbona haingii akiliniii
Yule mlinzi kwanini amfanyie hivo?, anakumbuka mtu alikuwa mwembaba mrefu na yule mlinzi ni mwembambaa Mrefuu
Alioanisha picha kwa mbali ikajaa
" Mungu wanguu!!! " Vicky aliingia chumbani ndio alilia sanaaa
Masha akamfata chumbani akamwambia
"Sikia Vicky,, We mkaushie tu wala usimuulize au kumwambia kitu sawaa mana utampa kichwa mjinga huyo "
"Sawa nimekuelewa"
Moyoni masha akasema yesss dili lake limeenda sawaa
"Kwishaa kabisaa, maliza chuo uende kwenu sikuhitaji karibu yangu tena Vicky "
Akaondoka huku anajisemea mwenyewe ...
Maisha ya masha sasa gafla tu yalibadilika akawa mtu mwenye pesa hata chuo aliacha hakujali kumalizia pesa ipo hakuna kitu alikuwa anakosa magari kubadilisha , simu za gharama viwanja vya bei mbayaa kote alipitaa
Walio mdharau alihakikisha wanamsalimia kwa kutetemeka na kwa kumuogopaa
Pamoja na yote aliona hawezi kutoboa mpaka jambo lake la ndoa lipite iwe isiwe lazima aolewe na Mr Alberto kama sio hivyo aliona hawezi kutoboa
Hali ya Vicky ilikuwa inabadilika siku hadi siku hakuacha kuumwa siku zilivyozidi ndio alizidi kuumwa vitu visivyoeleweka alikuwa wa kulala tu ndani
Akijitahidi kwenda chuo ndo hali inazidi kuwa mbaya na alikuwa mwaka wa nwisho kumaliza , alikuwa akijisomea Sanaa
Siku moja aliamka Asubuhi akajiambia acha tu aende hospital akapime maana hali kila siku inabadilika kama kaathirika basi ajue tu..
Vicky Aliondoka kwenda kituo chambali na nyumbani kwao
Sasa wakati anaingia kwenye kituo cha huduma
Masha nae alikuwa kwenye heka heka zake kwa mbalii akamuona mtu kama Vicky hivii
Akasimamisha gari yake kumtazama alikuwa ni yeye mwenyewe
Masha akajiuliza kwahiyo amepata pesa ya hospital eeh mama alivyokuwa ananipigia kelele kila siku nimpe mwenzangu helaa mfyuu
Akasogeza gari yake pembeni , akawa anamwangalia Vicky
Vicky akaingia mpaka kwa Doctor ni kituo cha mtaani tu hata haikuwa hospital
Akamwelezea Doctor anavyojisikia aliandikiwa vipimo vingi kati ya hivyo vipimo na mimba aliwekewa , akaenda maabara
Baada ya muda majibu yakatoka , Vicky alikuwa na UTI ,pamoja na Ujauzito
Je nini kitafuata?
KWETU morogoro.