MTNZ: ZAMRATA MBWANA (ZM)
NO: 0698095257
Tulipo ishia ni Pale Baba yake Zenafa anataka Akafanyiwe Operation na Gharama Zote Amelipa Mzee Kazumari .
Songa nayo ...
Hatimae Muda wa Kufanyiwa Operation Baba yake Zenafa Ulifika Na Zenafa na Ndugu zake Walikuwa nje ya Chumba cha Operation huku Wakiwa na Hofu tele na Kumuomba Mungu Awasaidie . Zenafa Alikuwa Atulii kwenye Kiti cha Hospital mda Wote Aliinuka na Kukaa
Baada ya Masaa Matatu Jopo la Madokta Lilitoka nje na Dokta Patrick Aliwafata.
Dokta:"Samahanini Jamani "
Zenafa : "Vipi Dokta Baba yangu Anaendeleaje "
Dokta: "Anha Hali ya Mgonjwa. Ni kwamba tumejitahidi kadri ya Uwezo Wetu Tumefanikiwa Kuunga mguu Baadhi ya Mifupa iliyokuwa Imevunjika na Mgonjwa tumefanikiwa Kumuwekea Antena Mguuni kwaajili ya kuunganidha Mifupa hivyo Hali ya Mgonjwa inaendelea Vizuri Ataamka mda si.refu baada ya Sindano ya Usingizi kuisha Nguvu "
"Sawa Dokta , Asante Sana "
"Sawa na Kunabaazi ya Dawa Mutapatiwa kwaajili ya Kumpa Mgonjwa "
"Sawa Dokta"
Hatimae Masiku Kazaa Yalipita na Baba yake Zenafa Aliludi Nyumbani Akiwa Anauguza Mguu wake Uliofungwa Antena huku Akiendelea Kutumia Dawa
Siku iyo Zenafa Alimtafuta Juma na Kumshukulu
"Umekuwa Rafiki Bora Kwangu Juma kila Siku unazidi kuwa wa Umuhimu kwangu Asante Sana , Pia Shukrani za ati ni Kwa Mzee Kazumari Ameludisha Tabasamu la Baba yangu . Mungu Amzidishie Rizki "
"Anha Usijali Zenafa Unaonaje Ingependeza Zaidi kama ungenda Kumwambia wewe Mwenyewe "
"Anha, Sawa "
Baada ya Mda Mchache Zenafa Alimfata Mashambani Mzee Kazumari . Siku iyo Alikuwa Amenda kuangalia Mashamba yake. Zenafa Alimfata uko uko kwa Msaada wa Juma
Walisalimiana
"Mh! Samahani Mzee Kazumari nipo hapa Kwaajili ya Kukushukulu kwa Kumsaidia Baba yangu Mzazi Pesa za Matibabu Asante sana "
Alisema Zenafa nakupiga Magoti chini bila Kujali hali ya Udongo Chini . Huku machozi yakimlenga
"Hapana , Zenafa Hauna haja ya Kufanya ivo . Pia Wakumshukuru Zaidi ni Mwenyezimungu Aliye Juu Embu inuka kwanza"
Zenafa Aliinuka
"Vipi hali yake kwasasa inaendeleaje Baba yako "
"Inaendelea vizuri tu , Tunashukulu Mungu "
Waliongea Kidogi na Zenafa Akaondoka kwao
"Ama Kwahakika uyu Binti ndo Anaefaa kuwa Mke wa Kijana Wangu Mahili , Nakalibia Kuondoka Dar es Salaam nitahakikisha nitaondoka na huyu Binti. Na sasa Taratibu za Kufunga Ndoa Zifate "
"Mh! Mzee unazani ni Rahisi ivo ?"
"Juma Mbele ya Pesa hakuna kinachoshindikana "
Maisha ya Kawaida yaliendelea Na Baba yake Zenafa Aliendelea Vizuri Kadri Siku Zilivyozidi Kwenda na Siku hiyo Mzee mmoja Anaetambulika hapo Kijijini kama Mzee Saidi Alikuja Kuleta Barua ya Uchumba .
Hawa Pamoja na Amina Walifurahi sana .
Amina : "Khe ! Jamani Hatimae na Mimi Mungu Kaniona nataka Kuolewa Sasa nimetolewa Ela ya Posa "
Hawa : "Chefu hivi Apo ulipo hivyo ulivyochunda unafikiri kuna Mwanaume atakae Jilocha kuja Kukuoa Wewe Paka la Baa kwa Bwana gani wa Maana Ulienae "
Amina : "Kha ! Ushanza Mambo yako Sina Mabwana Mimi kuna Masudi Kiwete, Kuna Abdala Nyaupala na "
Hawa : "Yaani Jina lenyewe tu Kiwete Ndo atakuja Kukuoa Wewe , Embu niache Uko Alafu Watu Wazima tunapokuwa na Majambo yetu Mtoto Usingilie . Hiyo Posa Ni Yangu Bwana Angu Ally Ndo Alienambia kuwa Ataleta Posa Siku Si Nyingi "
Mama : "Eee ! Nyie tena Mshaanza Makelele yenu Si mchamaze Barua itaelezea kila kitu "
Amina : "Au ya Zenafa ?"
Hawa : "Aaaa! Wapi Naluka Kichula chula hapa na Dar huyo Aliechunda. Ana Bwana gani ? Kelvin Kamkataa Amebaki Analia na Mapenzi cha Msingi Achukue Jembe Akalime tu "
Mda Huo huo Wanaongea Zenafa Alikuwa Analudi nakuni Nyumbani Kwao Alifika na Kuzitua Na Kuelekea Ndani Alimkuta Mama yake Wakambo na Dada Zake
Mama : "Vipi nimwambie Zenafa Kuhusu hii Barua ya Uchumba ?"
Hawa : "Jamani ! Jamani ! Mama Mtu ana Stress Zake unataka Kumvuluga Zaidi hapa Ata ukimwambia itasaidia nini Mtu ata Bwana hana Kwasasa "
Mama : "Mh ! Sawa MaBibi harusi "
Amina : "Kweli Mama Yeye Ashtukie Jambo lipo Miguuni tu hapo ndo kilicho baki "
ITAENDELEA ...9....
πSimu yangu ilikuwa inasumbua ndomana nilikuwa kimya ila sasa nitakuwa hewani ndani ya Ndoa ya mie mambo yanazidi kua moto kaa mkao wakula mtaarifu na jirani yako..