Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

DADA KIBOGA NA MJEDA 03

31st Jul, 2025 Views 41


Basi haikuchukua muda sana kama muvi ya kihindi ndani ya nusu saa tu tukafika mtipesaa , nikaagana na shogile wangu mama kibonge mie huyoo kila mtu akapita njia zake
Maana yeye kidogo maisha aliyawezea japo anauza supu ya mapupuπŸ€£πŸ€£πŸ‘Œ,kajitahidi mwenyewe shoo wangu anakaa kwenye chumba cha afu thelethini kina umeme japo wa mawazo ila sio ligi langu mimi nipo na kachumba ka afu ishirini cha gizaaa na bado natamba mwanamke kujiamini 🀣🀣

Kama kawaida nikawa nasokota kwato naelekea nyumbani kwanguuu ,njiani watu wote walikuwa wakinitazamaaa mie naskia rahaa balaa

Jamani nimenunua mcheleee kilo 15 staki wageni lakini🀣🀣,mimi sina siri jamani khaa basi mtaa mzima ukajua kua nimenunu mchele tena si kununua tu bali nimenunuliwa na danga langu jipyaaa

Dakika kumi tu zilinitosha nikawa tayari nimefika nyumbani

Da kibo nikupokee mchele??jirani mpambe aliniulizaa

Weee koma babu peleka njaa zako huko ,mwanamke usie jua kujituma weye kutwa kupanua miguu na kazi za maana zipo usije niharibia bajeti bure na miezi miwili🀣🀣

Hee da kibo yote hayo kisa mchele tule jirani aliongea
Hehehhehehe ntafute la undani nikupe yako ya ndani huo mchele unao??
Unataka ushindane na boss kibogaa??🀣🀣
Nikampandisha nakumshusha huyo nkachanja kwato hadi chumbani kwangu

Ukiachana na jinsi nilivo ila hii ngoma kuonewa ni no tena big NO sjui nipo sawa maana hili neno nililisikia kwenye muvi
Mie naitwa njoo kiumane aka mbabe wa mtaa

Basi na uchovu wangu mie nikatua mzigo nikajipandia kitandani kulala ,ilikuwa saa tisa hioo nkaja kushtuka saa 12 jionii tena simu ndo iloniamshaa mie pono

Haraka nikaiokota simu maana hata sikumbuki niliitupa wapi

Heeee jamani kiswaswa kiko wapi ?basi vurugu mechi ikaanza humo ndani tafuta tafuta hakunaa

Ikabidi nifungue kiroba cha mchele nikaingiza mkono ndo nikaipataπŸ€£πŸ€£πŸ™ŒπŸ™Œama kweli mmmmmmmh aaaaah

Muda huo ilikuwa imeshakata basi nikaangalia nani aliepigaaa nikagundua ni namba ngeni mfyuuuuuπŸ˜™πŸ˜™πŸ˜™πŸ˜™nikasema sipigi wala nini kama ana shida atapiga tena we ushaona wapi star kama mimi nikamnyenyekea mtu🀣🀣🀣

Nikaitupa simu huko nikachukua ungo nikapima mchele kilo moja nikaanza kuuchambua huko sina stress najua nna gesi hivo
Japo nilikuwa naskia joto kutokana na mtembeo wa asubuhi ila nikiwaza foleni la chooni uwiiii naishiwa poziπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œsi mnajua nyumba za uswahilini 🀣🀣🀣🀣choo kimoja nyumba kumii

Basi nikamaliza kuchambua mchele nikawasha gesi mweeehπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œpozi likaniisha kumbe gesi sinaaa sasa ntafanyaje na mchele nshauoshaa

Nikawaza mara mbili mbili ,nkapata akili nkatoka zangu hadi kwenye mianziii nikaokota vikunikuni ,nikatoka nnje ya nyumba ,nikakoleza moto mie nikaaanza kupikaa

Siku hio mtaa mzima ulijua kama mimi napika wali 🀣🀣🀣na nilivo na sifa nilienda kupika kati kati ya njia watu wote wajue nini napika sinaga jambo dogo🀣🀣🀣we usawa huu kupika wali mchezooi🀣🀣

Basi buana wali wangu ukaivaa nikanunua na viutumbo vya mia tano nikachukua sufuria langu huyo ndanii

Nikaanza kutafuta sahani sasa kama tano hivi,nikapakua wali mkavu nikaanza kuupitisha chumba kimoja hadi kingine kwa wale wapangaji wenye midomo na roho za husda na mie ndo kiboko yaoooπŸ€£πŸ€£πŸ€£πŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œ

Nikaziweka kwenye sinia nikatoka hadi nnje kwenye kordoo

"Majiraniiiiiii majiraniiiiiiiii nawaita mara mbili ya tatu ni ndoto tena ya alinacha"

Walivosikia hivo tu wotr wakatoka nnje
Aya shoga zangu nimepika ubwabwa kama mjuavo dogo sina ,sahani hizo mkimaliza zirudi safii

Piga kelele kwa dada kibooo wakeeeee🀣🀣nikaitikia weuweeeeeeee

Labda tu niwahadithie nyumba nilopanga mimi wapangai wenzangu wote ni madada poa nadhani mnawafahamu na danguro lao lilikuwa huko kinondoni na hivo juzijuzi limevunjwa tu ,basi wapo nyumbani hoi hawana mbele wala nyumaa maana katikati wanapo

Hivo hata ukiwapa ugali mkavu kwao sherehe,sembuse waliii unaopita hata kwa chai😜😜

Basi dada kiboga mie nikarudi ndani nikalala zangu mie sikutaka stress maaana nilikuwa nshashiba nilikula wali kidogo tu na vishombo vyanguuu

Usiku sasa majira ya saa tano nasikia simu inaitaa bwiiiii bwiiii bwiiiiiiiiiiii na vile kiswaswa kinavojua kukeraaa ukizingatia spika mbovi uwiiiiπŸ€£πŸ™ŒπŸ™Œ

Nikajivuta nikapokea japo nina wenge ka usingizi hatariii

Haloooo??haloooo?
Kimyaaaaaaa loooooh yani kuna watu mnajua kupoteza vocha yani mtu unapiga halafu huongei ndo nini sasa ovyoooo na mie sijui kubembeleza acha nijilalie zangu

Basi nikajitupa zangu kitandani mtoto wa watu staki shida na ninavokoroma sasa kama koroboi bovu🀣🀣🀣

Tukutane sehemu inayofuataaa
DADA KIBOGA NA MJEDA : 04

Hayawi hayawi sasa yakawa hatimae asububi ikafika kama kawaida yangu dada kiboga nikaamka nikaelekea hadi chooni

UwiiiiπŸ€£πŸ€£πŸ€£πŸ™ŒπŸ™Œjamani sjui foleni litaisha lini jamani khaa hapa bila ubabe sitoboi

Aya manirani nipisheni nioge mie, ila wali wa jana si ulikuwa pambe enheeee??
Sanaa tu dada kiboga tunae na tunatamba nae
Mie nikajibu teeeenaπŸ€£πŸ€£πŸ‘ŒπŸ‘Œhuku naingia bafuni kuogaa halooo

Basi nikakaa hukoo chooni nkajisugua haswa nilipotakata nikarudi zangu chumbani mie

Leo nikaamua nivae suruali na crop top nyeupeee huku kachuluari kangu keusi

Japo sjawahi kusifiwa ila najijua buana nikivaa dera haliwi kama kanzu kama tufudenge..... Au basi simtaji

Kisuruali kangu kalinikaa tako likajichora haswaa halooo nikafunga zangu mlango huyoo safari ya kuelekea kibaruani ikaanza

Dada kibogaa ni wewe kweli huyooo??? Mama kibo huyooo kashaanza na kuropoka zake maana huyu haongei huwa anakunya kwa kupitia mdomo

Sio mimi , ni bibi yako huyuuuu na kufuli kichwani🀣🀣🀣halooo mama kibo alicheka hadi akakaa chini

Mwendo wangu wa maringo sasa yaani ukiniona tu kama rijali unadindisha mwenyewee chezea wewe

Njiani nikakutana na ugomvi wadada watatu wanamchangia mdada mmoja si unajua mtaani tena watu walivyooo
Nikawaangalia kwa maneno waloyatoa nikajua pale kama hawajafumaniana si bureee

Enheee wadada mchana kweupe jua la utosi hili hapa mnaanza kumchania mwenzenu madera na alivomweupe hivi mumtie makovu kisaaa??? Kama desturi yangu nikavaa dera lisilonihusu , 🀣🀣nqjitia mwamba ngoja nipigike limshuke shuu

We sijui dada kiboga sjui kibo tobo la mlima kilimanjaro usizani sisi yunakuogopa wanaokuogopa wa huku sio sie fata hamsini zako tufate zetuu, vile vidada viwili visivyokuwa na nyama za usoni wala matakoni vikanijibu

Kwanza nikavitazamaa juu chini pembeni katikati , nikawapandisha nikawashushaa, nikawapima kwenye mzani wangu wa kilo tano nikaona hata moja hawafiki, 🀣🀣🀣

Kwanza asanteni kwa kunitambulisja bila kujitaja hqloooooo hehehehehehe, nadhani hamnijui vema mnanisikia kwenye redio tu ila bado tv hamjanunua

Sasa sikieni huu mtaa ugomvi mwiko hapo amueni muondoke mniachie huyo dada au tulipigee!, nikawakazia macho kwelikweli wanipe majibu mie🀣🀣🀣kama mtu kweli

Hatukuogopi bibi weeeh kama vipi tuzichapeee pambee tu

Kusikia lile jibu nikapandisha mizukaa kwanzaaa , nikavua crop topu yangu nikabakia na kitopu tu na surualiπŸ˜‚πŸ˜‚

Nikawasogelea acha niwavute nywele vuta vutaaa, niliwapiga makonde ya maana walijuta kunifahamu nakwambia

Nilipomaliza kila mtu akawa ananishangilia dada kiboga dada kibogaa mie tena bichwa hilo kam sufuria la msibani

We nae nyanyuka hapo chini umepoa kama uji wa dona usio na sukari loooh, nikampa mkono yule dada tukaondoka zetu haoo

Nikamtembeza dada wa watu haraka hadi tukafika saluni kwangu nikafungua kisha nikampa kiti akae

Aya shoga nambie nini kilikukuta hadi ikawa vileee

Yaani dada we acha tu , wale wamenikuta nyumbani kwangu na bwana angu wakaingia wakanivutaaa wakanikokota hadi pale eti wanasema ni bwana wao jamani

Pole shoga angu na wewe tuliza kibampuli hiko na kwanza sifanyi kazi buree nisafishie saluni ndo uondoke

Sawa dada
Basi mdada wa watu akasafisha kisha alipomaliza akaondoka

Nikabaki mwenyewe sasa kama kawaida siku ilikuwa mbaya hatarii wateja hamna na watu wa mtipesa wa bahili hata akija atasuka nywele ya mia tano kamaliza kwao rasta wanaziita nywele za maiti🀣🀣🀣

Wakati nimekaa zangu saluni kwa mbali nikaiona gari kali imepakii nikasema hiii tena fursaa jamani tajiri tajiriiii

Khaaaa !!!!! Si akatoka mjeda buanaa kwenyw garii na ajabu akawa kaongozana na yule kaka niliyemtapeli afu hamsini yake nikasema uwiiiii leo ukisikia kuisha ndo huku kama sio kupatikanaπŸ˜­πŸ˜­πŸ˜­πŸ˜­πŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œ
Itaendelea
Soma mpaka mwishooo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

DADA KIBOGA NA MJEDA 03  >>> https://gonga94.com/semajambo/dada-kiboga-na-mjeda-03
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

MTOTO WA MAMA LISHE

majario rewards 100 Comments 0
 

MY LUNA SEHEMU YA : 06

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest