Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

MEETING MY MATCH (Ubavu wangu πŸ˜‹) 1-2

31st Jul, 2025 Views 22


______________________________________

SEHEMU YA KWANZA

(Location; Mumbai, India)

(Ndani ya Kampuni la Ajanta Pharma linalo jishughulisha na usambazaji wa dawa muhimu)

"Kuhusu zawadi niliyo kuahidi nitatimiza kabla ya hii wiki kuisha, nimekuwa bize sana najikuta nasahau hata kwenda haja kubwa" Vedant (CEO wa Kampuni la Ajanta Pharma) aliongea huku akikagua bahasha aliyoletewa.

Baada ya kugundua ni picha ya Mwanamke aliishiwa pozi

"Huyo Mwanamke ni Mwana mitindo maarufu Jijini Newyork ..naomba uitazame picha yake ukiwa umeshiba, hakikisha unavaa miwani yako pia. Kitu kingine iangalie ukiwa pekee yako....nahofia huenda ukafika kileleni bila kupush ni mrembo sana" Manuu (Shangazi yake Vedant) aliongea huku akijichekesha, hakutaka kusikia neno lingine kutoka kwa Vedant aliondoka

Secretary Aaron aliingia akiwa kabeba files, ni mmbeya hatari baada ya kuona tu bahasha mezani alijua ina picha ya Mwanamke

"Usijali kuhusu hii bahasha nitakusaidia....." Secretary Aaron aliongea huku akijipa mamlaka, kabla hajaitazama Vedant alimkwapua bahasha

"Kuliko uhangaike na vitu visivyo kuhusu ni heri ufunge zipu ya suruali yako. Tangu juzi haufungi zipu usiniambie hao Wafanyakazi wapya waliotoka China wanakutesa moyo wako"

"Si...si..siyo hivyo..." Aaron aliongea kisha akaondoka kwa aibu, kuna namna aliguswa penyewe

Vedant hakuwa na haraka ya kufungua bahasha, aliendelea kutimiza majukumu yake.

"Vipi umevutiwa naye?" Ujumbe kutoka kwa Shangazi yake uliingia kwenye simu yake.

Kabla hajatoa jibu alishika bahasha, alijikuta akikodoa macho baada ya kukutana na sura ya Mwanamitindo maarufu kutoka Newyork akiwa mtupu.
Ni kama alikuwa anatazama XXX video hivi.

Bila uoga wowote wala aibu alishika simu yake akampigia Shangazi yake

"Ni mrembo lakini kuna vitu havipo sawa"

"Vitu gani hivyo"

"Matiti yake ni makubwa sana, napenda Mwanamke mwenye matiti ya saizi ya kati tu...ana hips kubwa sana, makalio yake ni makubwa pia. Napendelea Mwanamke asiye na makalio makubwa wala hips kubwa. Kitu kingine umbile lake halina mnofu. Nyama za hips zake zingekuwa kwenye umbile lake ningefurahi zaidi. Kitu kingine macho yake yamejaa aibu..."

"Vedant, kwanini kila Mwanamke naye kuletea unakataa, huyu mrembo alikuwa anakufaa sana sitaki ku...." Kabla Shangazi hajamaliza kuzungumza simu ilikatwa

Vedant alichukua kiberiti akaiteketeza picha.

Masaa ya kazi yalipoisha aliondoka akiwa na Secretary Aaron

"Hawa Wanawake wa Kichina ulioleta safari hawajui kutabasamu, kila napowaonesha tabasamu wanakaza sura zao. Hakika zivutiwi nao kwanini usiajiri watu wengine" Aaron aliongea huku akiendesha gari

"Tafuta Malaya huko nje upunguze nyege zako!....wana mionekano kama Wanaume nashindwa kuelewa kwanini unakaa zipu wazi. Hizo ni nyege na si kingine" Vedant aliongea

"Unaelekea wapi" Aaron aliongea kwa kupandisha sauti kidogo, ni wazi hakufurahishwa na mtazamo wa CEO

"Napita Super market kwanza....nataka nimalizane na Shangazi kuhusu zawadi yake"

Aaron aliondoa gari kwa kasi kana kwamba kabeba mgonjwa mahututi.
Bahati mbaya sasa tairi la gari lilitia kwenye tope. Kila Aaron alipojaribu kuondoa gari ilishindikana.

Iliwalazimu washuke kwenye gari kwanza, Vedant ni Mtaalamu mzuri sana katika swala zima la kutoa la lawama

"Jeeez! Mwanaume kabisa analalamika namna hii anasahau kama kuna kitu kinaitwa ajali!, hizi ni nyege na si kingine" Aaron alijikuta akiongea kwa sauti iliyopenya vyema masikioni kwa Vedant

"Wee nguruwe ni kitu gani hicho umeongea!"
Kabla Vedant hajamkata mtama Aaron mwokozi alitokea.

Walishtukia tu gari linasukumwa, walijikuta wakimtazama binti Mmoja aliyekaa kama wa kiume hivi bila kummaliza.

"Shilingi elfu 20 tu itatosha sihitaji pesa nyingi" Emilia aliongea huku akiachia tabasamu

Vedant na Aaron walitazamana kwa mara nyingine kupata mwendelezo full bonyeza link hii Hapo juu au chini ukasome yote hadi mwisho kwa buku tu…

Itaendelea πŸ’₯

SEHEMU YA PILI

Baada ya Emilia kuona watu hawa hawachangamki kumpatia pesa yake aliipiga gari teke moja tairi likadidimia tena.

Si mtu wa kutaka kuzungumza aliweka mikono yake mfukoni akaendelea na safari yake.

"Alikuwa anataka tu shilingi elfu 20 usiniambie haukuwa na pesa ya kumpatia,...." Vedant alianza kulalamika utadhani gari ni la Aaron

"Isiwe tabu bhana... ' Aaron aligomba ndani ya moyo wake kisha akawaita Vijana waliokuwa karibu. Aliwapa kibarua cha kulitoa tairi la gari

Ni Vijana wanne wenye misuli yao lakini hawa kufanikiwa.
Mwingine aliachia hadi mishuzi lakini hakufanya chochote.

"Ni kitu gani hiki wanafanya!" Vedant aliongea huku mkono mmoja ukishikiria pua zake

"Kama haoni vile kitu kinacho endelea..." Aaron alilalamika ndani ya moyo wake huku akijikuna kichwa. Balaa la boss wake analijua pindi atakapo anza kulalamika watu watajaa

"Ondokeni hakuna kitu mmefanya" Aaron aliongea huku akiangalia utararibu mwingine

Bahati nzuri Emilia alirudi akiwa kashika zake kifuko cha chips.

"Hello...." Aaron alijitia mwema

"Nipatie elfu 20 niondoe gari lenu hapo..." Emilia aliongea

Aaron hakuwa na namna, alizama mfukoni akatoa noti mbili za elfu kumi. Moyo wake ulikuwa unamuuma hatari, alijipa pole ndani ya moyo wake.

Emilia alitumia mkono mmoja kunyanyua gari.
Watu waliokuwa karibu walimshangaa, Vedant alijikuta akimkagua haraka haraka.

"Hana misuli ya kutisha, ni maajabu gani haya anafanya!" Vedant alijiwazia kichwani mwake

Baada ya Emilia kumaliza kazi yake aliondoka kwa mwendo wake wa kunyata.

"Tuingie kwenye gari, nina uhakika anatumia nguvu za giza" Aaron aliongea akiwa kwenye mshangao

"Siwezi kuingia kwenye hilo gari tena" Vedant aliongea

"Kwanini? hili ni gari lako"

"Umesema atakuwa anatumia nguvu za giza, vipi kama tukipata ajali tukafa!...liache hapo watu wa service watakuja kulichukua na kuanzia leo sliendeshi tena" Vedant aliongea kisha akasimamisha tax, hakuwa na habari tena na Aaron.

"Mbwa koko huyu!..." Aaron alijisemea kisha akashika simu yake, aliwapigia watu wa service waje kulichukua gari

Mida ya usiku Vedant akiwa amelala chumbani kwake alijikuta akikumbuka namna Emilia alivyo nyanyua gari toka kwenye tope kwa kutumia mkono mmoja

"Isije kuwa ni jini....hakuna mtu mwenye nguvu namna hii kwenye hii dunia tena Mwanamke" Vedant alijisemea

Usingizi wake ulikuwa ni wa shida sana, ilitokea kama bahati tu usingizi ukampitia.
Alijikuta akipiga kelele baada ya kumuota Emilia akinywa damu ya mtoto wa mbuzi.

"Kitu gani kimekupata!" Manuu (Shangazi yake) aliuliza huku akimfuta jasho

"Nimeota ndoto ya ajabu sana!" Vedant aliongea akiwa ana tetemeka

"Kuwa na amani, nampigia Guru Dev (kiongozi wa dini ya Kihindu) sasa hivi. Inaonekana kuna mashetani yana kufuatilia" Manuu ndio alizidi kumtisha kabisa Vedant
.
Dakika 40 hazikupita, Guru Dev feki alifika.
"Huna haja ya kuogopa upo sehemu salama" Guru Dev aliongea huku akimshika kichwani Vedant, alijitia kufanya maombi.

Kuna namna Vedant alianza kupata amani kabisa ya moyo.

"Kijana wako anatakiwa kuoa, inaonekana kuna shetani la kike limeanza kumuandama. Kama ataendelea kuwa single hatopata amani ya moyo kila alalapo usiku. Mwisho wa siku atashindwa kutimiza majukumu yake"

"Una uhakika na hiki unachoongea!" Manuu aliuliza akijitia kushangaa

Guru Dev feki alitikisa kichwa chake, alijitia kubariki nyumba zima kwa kumwaga maji ya baraka.

"Siwezi kulala chumbani kwangu naomba tulale wote" Vedant alimshika miguu Shangazi yake baada ya Guru Dev kuondoka

"Nitakufadhili kwa siku ya leo tu ila kesho utalala chumbani kwako....kila kitu kitawezekana siku ya kesho. Tutalifukuza hilo shetani kwa kuleta Mwanamke mahali hapa"

"Una maanisha nini kusema hivyo"

"Kesho ni harusi yako" Manuu aliongea

Vedant alitaka kugoma lakini kila alipo kumbuka maneno ya Guru Dev feki aliingiwa na uoga.
Kwa mara ya kwanza kabisa alilala chumbani kwa Shangazi yake huku taa zikiwa zimewashwa kana kwamba kuna sherehe.

Ilikuwa ni ngumu kwa wote kulala kwa sababu walishazoea kuzima taa.

Upande wa Emilia akiwa chumbani kwake aliwasha mshumaa akaanza kuzikagua pesa alizopatiwa na Secretary Aaron.
Aligonga meza kwa hasira baada ya kugundua ni feki.
Aliutazama mkono wake uliotumika kunyanyua gari.

"Hao mbweha hawana bahati, kwa uhuni walioutenda ama zangu ama zao" Emilia alitangaza vita kisha akazima mshumaa.

Upande wa Secretary Aaron anaachia tabasamu ndani ya moyo wake baada ya kugundua pesa zilizomtoka ni zile feki anazotumiaga kutunisha mfuko wake akiwa ameishiwa.

Saa 12 juu ya alama, Manuu (Shangazi yake Vedant) alipiga simu katika familia moja maarufu hapa Jijini Mumbai walete mke.

Kufumba na kufumbua nyumba yote ilipambwa na kupambika.

Watu wachache tu ndio walialikwa akiwemo Secretary Aaron.

Vedant alijitazama kwenye kioo akiwa kavalia mavazi ya harusi. Hakuamini kama siku ya leo anaoa.

"Naomba kabla ya yote kutendeka nimuone huyo Mwanamke anayetakiwa kuwa mke wangu" Vedant alimuambia Shangazi yake.

Manuu aliachia tabasamu kumaanisha hakuna matata

Itaendelea πŸ’₯
Full sh 1000

Njoo WhatsApp katika namba 0683944333.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

MEETING MY MATCH (Ubavu wangu πŸ˜‹) 1-2  >>> https://gonga94.com/semajambo/meeting-my-match-ubavu-wangu-1-2
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

MTOTO WA MAMA LISHE

majario rewards 100 Comments 0
 

MY LUNA SEHEMU YA : 06

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest