Dereva alikuwa ni alex, aliifata nyuma taratibu Gari ambayo ndani walikuwa juddy na zakia
Mwendo ulikuwa mrefu mnoo , tukatoka kabisa nje ya mji , tukaingia sehemu moja wanaita kibaha
Baada ya kufika kibaha kwenye tukaingia huko ndani ndani kabisa yaan ndani hukooo
Mwisho gari ilisimama baada ya gari ya Kina zakia kuonekana inaingia kwenye moja ya nyumba zipo ndani ndani yaan kijijini huko polini kabisa..
Tulipack pale nje , alex anasema jamani tuingie huko, inno akamwambia tutulie mpaka tupate mwongozo wa zakia .
Tulikaa hapo kama lisaa hivi
Inno akasema katuma sms anasema tuingie ndani moja kwa moja kwa huyo babu mana amethibitisha ni kweli huyu babu ndie karoga mpaka salma kuwa hivyo
Nikasema eeh Asante mungu , alex alinibeba pamoja na subira wakaniwek kwenye kile kiti changu cha mataili wakanikokota , tuliingia ndani moja kwa moja yaan juddy alishtuka baada ya kutuona alishtuka sanaaa , uso wake ulikuwa na woga kabisaaa .
Yule babu alitukaribisha vizuri akatuambia kuwa tusubiri hapo nje kwanza amalizane na wale
Alex akasema sawa tupo hapa nje babu ,alisema kwa heshima zotee kabisaa ..
Tulirudi kusubiri kwa nje baada ya sec kadhaa juddy nae alitoka akaja tulipo pale, alitusalimia vizuri tu akanambia salma kumbe bado hujaponaa??
Mi kimyaa anajitilisha huruma ooh mungu atakusaidia utapona tu kwani nani amekuelekeza hapa et
Yaan alikuwa hajiamini anauliza uliza tu muda wotee maswali ya kutetemeka
Alex akamwambia Juddy embu tuache kidogo et
Juddy hakuwa tayari kuondoka anatetemeka kweli amekazana anauliza ni nani ambae amewaelekeza hapa jamani et sijui nini
Baada ya kuona hapati ushirikiano aliamua kuondoka wakati huo zakia alikuwa ndo ametoka tu kwa yule babu, Juddy alirudi haraka mule ndani
Alikaa sanaaa afu akatoka anacheka cheka akamwambia Zakia tuondoke
Zakia akasema bado mie kuna dawa kipenzi
Tuliingia ndani sisi hapa wote , yule babu alitukaribisha lakini sio kama mwanzo hakuwa amechangamka kabisaaaa
Alex alianza kumuelezea akamwambia
"Babuu , tumekuja tunaomba msaada wako, mke wangu yupo kwenye hali hii na tumeambiwa wewe unaweza kutusaidia "
"Nani amewaelekeza??" Yule babu aliuliza akiwa Serious afu anatuangalia kwa zamuu
"Kuna mtu ni rafiki yangu ndie alituelekeza hapa kwenye kuhangaika hangaika tu" alijibu inno haraka
"Ngoja tuone"
Alianza kufanya madude yake pale kila mtu alikuwa kimyaa anamtazama
Baaada ya muda alitutazam tena akasema
"Siwezi kuwasaidia katafuteni sehemu ingine "
Mungu wangu moyo ulinipiga paaah
Nilitamani nipige magoti kumuomba yule babuuu ,nilianza kulia jamani nililia saana
Alex na inno walimuomba mnoo japo hata ajaribu tu kunisaidia
Yule mzee alishikiria msimamo wake kuwa hawezi tuende sehemu ingine ..
Mpaka alikuwa na mkalii, ilibidi Alex ainuke akasema tuondokeni
Tulivyotoka inno akamuuliza mbona umekata tamaa mapema akasema hapana tutafute njia ya kumuingia huyo mzeee
Twende hata police ,inno akasema hapana police hawawezi kusaidia wala nguvu piaa haisaidii tutumie akili hapa
Akili gani, lilibaki kuwa swali kila mtu akabaki anawaza mwenyewe
Alex akasema mpigie Zakia , subira akawaambia zakia kwa sasa bado yupo na Juddy sio rahisi kuongea
Maamuzi alitoa alex hakuna kuondoka kwa huyu mzee mpaka njia ipatikane
Kama kulala tutalala kwenye gari woteee
Inno aliondoka akafata chakula , hata sijui wapi sie tukabaki hapo , tunasubiri amalize kuwahudumia wengine na sie tuendelee na kuomba msaada
Mpaka usiku bado tulikuwa nje pale , yule babu hakutaka kabisa kutusikiliza yaan mpaka alikuwa anatutishia kabisa atafanya kitu kibaya
Hapo zakia hakututafuta hata tulimuuliza Dereva akasema ye aliwaacha wote sehemu moja kwahiyo hajui
ITAENDELEA....
KWETU morogoro.