Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

NILIZANI MWIZI KUMBE MMMH SEHEMU YA 45__46πŸ’˜πŸ’˜

31st Jul, 2025 Views 207



.... yaan ukikutana na alex unaweza kusema huyu kaka alishafilisika maisha yamempiga kweli kweliiii

Tangu hapo nilianza kuona hata tabasam kwa familia yangu , sikuwa nimepona lakini nahisi niliwapa matumaini makubwa sana ..

Siku zilienda ,muda wangu wa kujifungua ulifika ,nikafanyiwa OPERATION, Alhamdulillah nilipata watoto wawili wote wa kiume , wazuri zaidi hata ya baba yao , sikuwa naweza kuwashika hata kuwapa nyonyo subira alikuwa beneti na mimi muda wote , kuhudumia watoto , wakilia anawaweka kwenye ziwa langu

Lakini mama mkwe nae alikiwa anawajali mnoo yaan walikuwa kwenye uangalizi karibu wa watu wote humo ndani, hapo nilikuwa naweza kusogeza tu mkono labda mguu kidogo lakini kuongea sikuwa naweza wala mwili ulikuwa bado hauwezi kufanya kitu chochote kile ...

Niliuguza kidonda changu,kilichelewa mno kupona mana sikuwa nafaya mazoezi yeyote zaidi ya kulala tu , katika vitu ambavyo siwezi kusahau na hili pia
Nilipitia kipindi kigumu sana wakati huo

Lakini siku zote sikuacha kuomba kwa Dini zangu iwe islam au kristo sikuacha kumuomba mungu sikuacha kabisaa, nilimlilia asubuhi mchana na usiku anitoe kwenye haya mateso ...

Nakumbuka ilipita miezi mitatu tangu nimejifungua , kidonda kilikuwa kinapona siku mbili kina rudi kwa kasi ,
Kilianza kutoa harufu nasikia maumivu makali sana yaan ile furaha yetu ilipatikana baada ya muda mfupi tu ilipotea niliona haya ni mateso kuliko yale ya mwanzo
Nilikuwa namuomba mungu bora nife tu , kwanini nateseka mie tu kwanini mimi mungu wanguuu!!!?

Nilichoka hata kuomba nikabaki tu kuwa nalia , alex alikuwa ananipa moyo kuwa atapambana kadri anavyoweza kunitoa hapo lakini ilikuwa ngumu

Mama yangu ndo kabisa akazidi kuisha yaan ni kama vile nilianza matatizo upyaa
Nilikuwa natoa harufu mpaka mie mwenyewe nina jisikia
Madaktar waliletwa wa kila wadhifa lakini hakukuwa na matumaini ya mie kupona hata kidogo

Nililijua hilo nikaanza kutubu taratibu, huku naikabidhi nafsi yangu kwa mungu yeye ndie atajua anipe nafasi ingine au muda wangu ulisha isha basii ...

nikiwa nipo kwenye nafasi ya mwisho kabisa nilihisi hivyo kwa sababu ,siku za wakati huu naumivu yalizidi na ugonjwa ulikuwa umenizidia sanaaa

Siku hiyo alikuja Zakia baada ya muda mrefu mno kupita mnoo ,nilikuwa hadi nimekwisha kumsahau wala sikumpa nafasi kwenye maisha yangu tena si yeye wala Juddy
Nilitaka tu niachie maisha mengine aendelee kama kufa ni jukumu langu basi nitalitimiza tu, hata wao hawataishi milele najua

Kila mtu alistaajaabu baada ya kumuona zakia , ndipo subira alikuja ndani mbio akanambia dada zakia amekuja , mwenyewe nilishtuka nikawaza sijui amekuja kufanya nini tu

Nilitolewa kwenye kitu , Alex akanambia njoo tumsikilize zakia mke wangu kuna neno amekuja kusema , kipindi hichi hata lile tabasam sikuwa nalo tena .

Yaan kwa kipindi ambacho nilianza kuumwa na kidonda , watoto wote aliwachukua mama mkwe kwahiyo sikuwa nanyonyesha tena wala kulala nao , walikuwa kwa mama mkwe pamoja na kutoa harufu chumba chote bado alex hakuwa analala pengine zaidi ya pembeni ya kitanda changu....

Tulienda mpaka sebleni yaan baada ya kumuona Tu zakia nilikumbuka tukio zima ni kama jana tu imetokea yaan ni kama jana usiku nilikuwa mzima sana nikanywa ile juisi , nilitamani kurudisha masaa nyuma mie hata niende kuimwaga mie!!
Zakia alikuwa amependeza kanenepa ameng'aa mnooo yaan amependeza kawa mdada wa maana sio yule wa zamani wa uswahilini
Mi nilivyomuona nililia sana nililia mnooo, niliongea mengi moyoni nikasema mungu huyu mtu amekuja kufanya nini??
Inamaana amekuja kunionyesha kuwa amependeza anamaisha mazuri ,Et hajateteleka??

Kaja kufanya nini kwangu huyu mwanamke
Mi nilikuwa natoa harufu sanaaa afu yeye ananukiaaa??

Zakia alikuja akapiga magoti mbele yangu , akanambia salma ,nilikuwa mpuuzi sikuwa na akili nzuri naomba unisamehe nimekuja nikiwa na akili zangu nimepatafuta hapa sana na leo nimefika naishi kwa raha nilipo lakini moyo wangu kila siku unahisi kuna deni nyuma yangu

Salma wewe ni kama umenifunga kabisa siwezi hata kulala nimekuja kukutaka radhi

ITAENDELEA...

Tuktane saa 3:00 usiku
KWETU morogoro.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

NILIZANI MWIZI KUMBE MMMH SEHEMU YA 45__46πŸ’˜πŸ’˜  >>> https://gonga94.com/semajambo/nilizani-mwizi-kumbe-mmmh-sehemu-ya-45__46
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

MTOTO WA MAMA LISHE

majario rewards 100 Comments 0
 

MY LUNA SEHEMU YA : 06

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest