Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

SINGLE DADY NA MAMA WA KUKODI* *________________________________________* *SSEHEMUYA 01 na 2

31st Jul, 2025 Views 40



" Max fanya haraka urudi mke wako ameondoka siku ya pili leo kamtelekeza mtoto hapa nyumbani kwangu. Ilikuwa ni sauti ya Irene dada wa Max, hizo taarifa zilimshitua Max lakini hakutaka kuamini kama mke wake anaweza kumfanyia hivyo binti yao .
" Haiwezekani Hilda hawezi kumtelekeza shalon.
" Ndio nakwambia fanya haraka urudi maana kasema hana uhusiano na nyie tena yani amewaacha na maisha yenu nae kaenda kutafuta maisha yake mengine.
max kwanza hakuamini kama mke wake anaweza kufanya kitendo cha ajabu cha kumuacha binti yao mdogo na kwenda kusikojulikana tena ukiwa max hayupo alikuwa safarini nchini sweden.

Max alipokataa simu ya dada yake aliamua kumpigia simu mke wake Hilda bahati alibahatika kumpata kwa njia ya video call na Hilda alipokea .
" Hallow max.
" Hilda.....
" Niambie max.
" Hilda niliyoyasikia ni kweli?
" Yapi hayo uliyoyasikia?
" Kuhusu wewe kuondoka nyumbani na kwenda kumtelekeza mtoto kwa dada Irene?
" Sijamtelekeza nimempeleka kwa shangazi yake ile ni damu yake pia anatakiwa kumlea mtoto wa ndugu yake.
" Na wewe upo wapi?
" Nipo sehemu inayostahili kuwepo, max unatakiwa kuanza maisha mapya wewe na mtoto wako .....
" Unamaana gani kusema hivyo au nimekukosea nini mpaka uchukue hayo maamuzi?
" Hakuna ulichonikosea nimeamua tu sababu nimechoka kuishi na wewe.
Max alitulia kwa muda huku akiugulia maneno makali yaliorarua moyo wake.
" Sawa vipi kuhusu mwanao Shalon?
" Hiyo ni zawadi nimekuachia.
Aliongea Hilda bila kuwa na uchungu hata kidogo ndio kwanza alinyanyua grass ya mvinyo na kunywa.
" Hilda....... Max hakumaliza kuongea alinyamaza na kukazia macho kwenye simu yake.
Alimuona Hilda akiwa na James ex wake wa zamani.
James alimbusu Hilda kisha akamuangalia max na kumpungia mkono.
Max alishajuwa sababu ya yeye na mwanae kuachwa hakuwa na haja ya kubishana na mtu alikata simu na kujiandaa na safari ya Tanzania.

Max ni mwanaume wa miaka 35 ni baba wa mtoto mmoja wa kike anayeitwa shalon, shalon ana miaka saba ana matatizo ya kuona hali hiyo ilitokea ghafla alipokuwa na miaka miwili . Max alihangaika sana kumtibia mwanae alienda hospitali mbali mbali kwani alikuwa na matumaini mwanae atakuja kuwa sawa pia madactari walimpa matumaini kuwa tatizo la shalon sio kubwa kuna uwezekano mkubwa wa kupona tena ila kuna hitaji muda kidogo hivyo uvumilivu unatakiwa.

Baada ya shalon kupata hilo tatizo mama yake Hilda aliamua kuwatoroka max na mtoto wake bila kusema sababu ya kuwaacha.
Max aliumizwa sana na maamuzi ya mke wake , aliishi kwa unyonge sana hasa pale binti yake alipokuwa akimuita mama yake.

Siku moja Shalon alikuwa alikuwa amekaa chumbani kwake akawa anamuita baba yake ambae alikuwa jikoni anaandaa kifungua kinywa.
" Baba, Baba.....
" Nakuja malaika wangu.
Max alienda chumbani kwa shalon akamkuta kakaa kitandani huku akiwa kapakata mto wake.
Max alikaa pembeni na kumbusu binti yake shavuni. Shalon alitoa tabasamu huku akimpapasa baba yake usoni.
" Baba nimeota ndoto nzuri sana.
" Eheee niambie princess wangu umeota ndoto gani?
" Nimemuota mama amekuja akanikumbatia na kunibusu nilifurahi sana .
" Mmmmmh. Max aliishia kuguna
" Baba ulisema mama atakuja hivi karibuni anakuja lini?
" Siku sio nyingi atakuja .
" Natamani awe mtu wa kwanza kumuona siku nitakayo weza kuona.
Hapo ilikuwa baada ya wiki mbili Shalon alitakiwa kufanyiwa upasuaji ili aweze kuona.

Max aliumizwa sana na maneno ya Shalon hakujua ameambiwa nini tena maana kila siku amekuwa alimdanganya kuwa mama yake atakuja .
"Ila Hiyo ni ndoto tu malaika wangu usifikie mamani.
Shalon alipoteza tabasamu lake baada ya baba yake kumwambia hivyo.
" Vipi mbona sioni tabasamu lako zuri kipenzi?
" Kwahiyo ndoto yangu haikuwa kweli mama yangu hatakuja? Lakini uliniambia mama yangu ananipenda na atakuja kwaajili yangu.
" Ndio atakuja .
Shalon aliachia tabasamu , alimpapasa baba yake na kumkumbatia kwa furaha
" Sawa unatakiwa kupiga maswaki na kuoga nimeshakuandalia chai.
Max alimchukua binti yake akaenda kumuogesha na kumvalisha vizuri baada ya hapo walikaa mezani wakawa wanakunywa chai.
Akili ya max haikuwepo pale alikuwa anawaza atapamta wapi Hilda mama yake Shalon maana tangia alivyoondoka hawakuwahi kuwasiliana na wala hajui alipo.
" Hilda sikuwahi kukifanyia kitu kibaya lakini kwanini umeamua kunikimbia na kumuacha binti yetu ambae unajua kabisa anahitaji huduma zako, ona sasa nitamwambia nini binti yangu kuhusu mama yake , itakuwa sawa nikimwambia mama yako alikutoroka na kwenda kwa mwanaume mwingine? Sijui siku akiona nitamjibu nini kuhusu mama yake na nimeshamuahidi mama yake atakuja.

Max aliwaza mengi mpaka ajisahau kama alikuwa analisha mtoto mpaka shalon alivyopapasa akishika mkono wake ndipo akashituka.
" Baba mbona hunilishi, kwani unafanya nini?
" Nipo pembeni yako mwanangu nisamehe kwa kuchelewesha kukulisha.
Aliongea max huku akiwa anaendelea kumlisha.

Upande wapili anaonekana dada mmoja mrembo Dala akiwa anakaa mbele ya kioo anajiremba uso wake huku mdogo wake Shakira akiwa amekaa kitandani anamuangalia
" Dada Dala unataka kutoka tena usiku huu?
Aliuliza Shakira mdogo wake Dala.
" Ndio mdogo wangu si unajua kazi zangu ni za usiku.
" Kwahiyo Nitakuwa nalala mwenyewe? Shakira aliuliza ,
Dala alimgeukia mdogo wake na kumwambia.
" Unatakiwa kuzoea maana hii ndio kazi yangu kwa sasa na ninafanya kwaajili ya kukidhi mahitaji yako unatakiwa kuusoma, kula na huduma nyingine zinazostahili.
" Kwani unafanya kazi gani?
Dala alisita kidogo kujibu swali la mdogo wake , lakini Shakira alimuangalia kwa makini akiwa anasubiri jibu kutoka kwa dada yake.
" Sio muhimu kuijua kazi yangu ila unatakiwa kujua dada yako nahangaika kwaajili ya maisha yetu , tunatakiwa kuishi vizuri kama watu wengine.
Aliongea Dala huku machozi yakitaka kutoka. Alimaliza kujipodoa akavaa viatu vyake .
" Acha niwahi.
" Sawa.
" Kuwa makini mdogo wangu , kumbuka kufunga mlango vizuri.
" Sawa.

Dala aliondoka akaenda kazini kwake kwenye bar moja maarufu pale mjini na siku hiyo ya weekend ilikuwa inapiga live band na watu wengi walikuwepo hapo wakipata moja moto, moja baridi huku waliburudika .
" Dala huu ndio muda wa kuja kazini?
Meneja wa ile bar alimuuliza huku akiwa anaangalia saa yake ya mkononi.
" Samahani foleni ilikuwa kubwa barabarani.
" Hii ni kawaida yako sasa leo iwe mwisho kuchelewa endapo ikitokea nitakifukuza kazi,
" Naomba unisamehe....
"Nenda kaendelee na kazi haraka
Dala alienda kubadili nguo haraka na kuanza kuhudumia wateja.

Max alikuwa kwenye hiyo bar akinywa huku akitafakari maisha yake na binti yake , pia bado alikuwa akijiuliza atapata wapi mwanamke wa kuwa mama kwa binti yake ambae atamchukulia Shalon kama mwanae.
Aliwaza sana badae akajikuta anasema
" Hakuna mwanamke anaeweza kuwa na uchungu na mtoto wa mwanamke mwenzie.
Wakati anaongea hivyo Dala alipita karibu yake na kusikia alichokiongea Max.

*SEHEMU YA PILI*

Dala alisimama akamuangalia jinsi anavyokunywa kilevi chake na kuongea mwenyewe kama mtu aliechanganyikiwa.
" Huyu mtu anaonekana anamatatizo.
Huruma zilimfanya asogea karibu yake na kumsalimia.
" Habari yako kaka!
Max alinyanyua macho yake akamuangalia juu mpaka chini kwa macho ya mtu aliekuwa kalewa kisha akamwambia
" Niambie mrembo, unataka nini kutoka kwangu?
" Kuna tatizo linakusumbua?
Max alitabasamu huku alinyanyua grass yake ya pombe na kunywa kisha akaweka grass mezani.
" Ni kweli nina tatizo unaweza kunisaidia?
" Kama hilo tatizo lipo ndani ya uwezo wangu nitakusaidia.
" Sikujua kama kwenye hii dunia kuna watu wanaoweza kujali matatizo ya wengine, hatimae leo imefikiwa na mimi.
" Unamaana gani kusema hivyo?
Max alitulia kidogo kisha alimuangalia Dala usoni na kusema.
" Naweza kuwa na wewe usiku wa leo?
Dala alimuangalia kisha alifikiria kwa muda kisha akasema
" Unamaanisha kuwa na mimi kivipi?
" Usijifanye mtoto ambae haelewi chochote .
" Tafadhali nipo kazini. Alijibu Dala kisha akataka kuondoka
" Hebu tulia mtoto wa kike mbona unarukaruka hivyo kama pesa mimi ninayo . Alisema Max huku akitoa pesa kiasi kama elfu 50 na kumpatia kabla hajafanya chochote.
" Hii ni kama advance tu. Shika hii baada ya hapo utafutaji zaidi, ninayo pesa ya kutosha.

Kwakuwa Dala alikuwa na majukumu mazito na pesa anayelipwa pale bar haikidhi mahitaji yake na alikuwa akidaiwa ada ya shule ya Shakira akajikuta anapata tamaa na kukubali kutoka na Max .
" Sawa utaniongeza shilingi ngapi?
" Usijali kuhusu pesa kikubwa anipe huduma nzuri .
" Sawa nakuja sasa hivi.
Dala alikubaliana na max akaenda kuongea na mwenzie akamuachia pesa kidogo kisha yeye akaondoka na max.

Walifika kwenye chumba cha hotel max aliagiza pombe akaendelea kunywa huku Dala akiwa anamsubiri afanye kazi iliyompeleka apewe chake aondoke.
" Mmmh kwa hizo pombe anazokunywa kama maji kuna jambo hapa ? Dala alianza kumtilia mashaka na kuona kama kaenda kuangalia mtu anashindana na pombe.
" Nimekuja kupoteza muda wangu bure kumbe mtu mwenyewe mlevi kupita maelezo.

Muda ulizidi kwenda hakukuwa na dalili ya kufanya chochote ikabidi Dala aulize.
" Mbona sikuelewi na muda unaenda wewe umekazana kunywa pombe tu.
" Kwani wewe shida yako nini mrembo?
" Kwani hapa nimekuja kukuangalia unavyokunywa?
" Nimekuambia tunywe umekataa sasa unataka nifanye nini?
" Mimi situmii pombe na hapa sijafuata hicho kumbuka umeniita kwa jambo lingine na sio kukuangalia....
" Kwani shida yako si nipesa nitakupatia hizo pesa wewe tulia hapo na muda wako wote wa kuwa na mimi nitaulipia mimi ndio Max bwana sina shida na pesa ndogondogo.

Max aliendelea kunywa, ile hali ilikuwa inakera sana Dala alitamani kuondoka ile sehemu lakini muda ulikuwa umeenda sana . Alizunguka ndani ya kile chumba huku alichungulia dirishani.
" Kwani huwezi kutulia sehemu moja?
Max aliuliza
" Tangia nimeanza kukutana na wanaume sijawahi kupata mwanaume kama wewe yani unaboa sana.
" Hivi unaitwa nani vile?
"Dala.
" Una miaka mingapi?
" Miaka yangu itakusaidia nini?
" Kama hutaki kujibu basi .
Dala alimuangalia kisha akamjibu.
" Nina miaka 21.
" Mbona bado mdogo sana alafu unafanya kazi hatari kama hizi? Umri kama wako sasa hivi wapo shule wanasoma lakini wewe unauza bar na kujiuza .
Hiki neno kujiuza kilimuumiza Dala kwani haikuwa tabia yake ndio kwanza siku hiyo alikuwa anaanza. Alitamani kumwambia lakini alijua hawezi kumuamini .
" Kila mtu anachagua jinsi ya kuishi na kujipatia kipato hivyo usiniingilie
" Hii ndio njia sahihi kwako kwa kujipatia kipato?
" Kaka kama unaona hii ni kazi haramu basi hata wewe umefanya kitu haramu maana mimi na wewe wote tunashiriki kwenye huo uharamu wewe unataka starehe mimi nataka pesa.

Maswali ya max yalikuwa kama yalikuwa yanaamsha machungu. Dala alienda kukaa kitandani mpaka usingizi ukampitia, alikuja kushituka majira ya saa kumi na mbili asubuhi, alimuona max Kalala pembeni yake. Alimuangalia na kutaka kuchomoa Wallet ili achukue pesa lakini akaamua kuacha
" Sijui kapatwa na nini, kunichukua kwaajili ya kunipotezea muda wangu bure, hii ni hasara.
Dala alivaa viatu vyake alipomaliza aliondoka na kumuacha max akiwa bado Kalala.

Baada ya wiki mbili kupita max akimpeleka binti yake hospitali kwaajili ya kufanyiwa upasuaji na zoezi zima lilikamilika . Shalon akiwa bado kafungwa bandeji kwenye macho yake alikuwa akiuliza kama mama yake kafika.
" Shangazi mama yangu amekuja?
Irene alimuangalia ndugu yake na Max alimuangalia bila kujibu chochote.
" Bado hajafika ila amesema kesho kutwa atakuwepo hapa.
" Nataka nikifunguliwa macho yangu nimuone yeye kwanza.
" Sawa nitamwambia awahi kufika. Utamuona akiwa kakaa pembeni yako.

Max alitoka pale wodini na Irene akamfuata nyuma.
" Unaenda wapi sasa?
" Acha nikapumzike kichwa changu hakipo sawa.
" Lakini umesikia mtoto wako anachokitaka sijui utamwambia nini ili akielewa.
" Niache kwanza.
Alisema Max alafu aliondoka akionekana hayupo sawa.
Ilipofika Jioni alienda kwenye ile bar anayofanya kazi Dala . Wakati anashuka kwenye gari alimuona Dala anarumbana na kijana mmoja .
" wewe ni malaya tu ndio maana una ng'ang'ania kufanya kazi hapa ili wanaume wakushikeshike.
" Nimekuambia kazi siachi , kwani tangia nimeanza mahusiano na wewe ilishawahi kunisaidia nini? Napitia maisha magumu , mdogo wangu ananitegemea, natakiwa kumlisha, kumvisha ,kumlipia ada ya shule na kodi ya nyumba kama mpenzi wangu ilishawahi kunisaidia hata jukumu moja ? Zaidi wewe mwenyewe unaniomba hela ndogo ndogo.
" Kwahiyo ndio unatangaza kila mtu ajue kuwa unanipa hivyo vibukubuku vyako.
" Huna msaada na mimi karisto kazi inayojua wewe ni kuoga kuvaa vizuri, kujipulizia marashi unukie vizuri, kuvaa Cheni na hereni watu wakuone wakusifie. Usharo baro ndio unaweza wewe lakini kufanya kazi aaaaaaaah.
"Basi sawa kuanzia sasa tusijuane endelea na mambo yako na mimi niendelee na yangu.
" Kila la kheri. Kwanza nashukuru kwa kutua gunia la misumari lililokuwa linaelekea mabegani kwangu.

Kalisto aliondoka kwa hasira na Dala alipiga hatua chache akielekea bar kabla hajafika mbali max alimuita.
" Dala....
Dala alisimama na kugeuka kumuangalia mtu aliekuwa anamuita.
" Ni huyu tena mwanaume asiyekuwa na hisia sijui anataka nini kwangu.
Alijisemea dala huku akiwa kasimama anamsubilia Max ambae alikuwa anamfuata pale aliposimama.
JE NINI KITAENDELEAAA!! "
OFAAAA KUPATA YOTE NI 1000 TU
NJO....
WHATSAP 0755090082.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

SINGLE DADY NA MAMA WA KUKODI* *________________________________________* *SSEHEMUYA 01 na 2  >>> https://gonga94.com/semajambo/single-dady-na-mama-wa-kukodi-________________________________________-ssehemuya-01-na-2
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

MTOTO WA MAMA LISHE

majario rewards 100 Comments 0
 

MY LUNA SEHEMU YA : 06

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest