Ingia

Sema Jambo 2025

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  gonga94 official track

Utajiri mkubwa ambao mpaka leo haujulikani upo wapi Kuna madini mengi

19th Sep, 2025 Views 11

yalipotea na kuibwa, kuna vitu vingi navyo vilipotea, mpaka leo watu hawajui vipo wapi.

Wengine wakaingia kazini na kuvitafuta kwa kuhisi vipo huku na kule, wakapoteza muda, pesa lakini bado hawakuviona. Haya ni baadhi ya vitu vilivyopotea ambavyo kama kuna siku utaviona mahali, hakika utakuwa tajiri mkubwa sana.

Taji lenye utajiri wa dola milioni 6.

Hili lilikuwa la mfalme katika jumba la kifalme la Dublin. Liliibwa mwaka 1907 na mpaka leo hakuna anayejua lilipo. Je, liliuzwa? Liliharibiwa ama? Nobody knows.

Vitu mfano wa mayai vya nchini Urusi

Kabla ya mapinduzi nchini Urusi kulikuwa na vitu mfano wa mayai ambavyo vilitengenezwa kwa kutumia madini ya bei mbaya. Vilikuwa saba na vilitengenezwa mahususi kwa ajili ya nyumba ya mfalme. Vitu hivyo vina gharama ya dola milioni 230 lakini baada ya mapinduzi makubwa nchini humo, havikuonekana tena mpaka leo hii. Nani aliviiba? Alivipeleka wapi? Hakuna ajuaye.

Dhahabu na Almasi nyingi huko Virginia

Kulikuwa na kikabati kikubwa kilichokuwa kimehifadhiwa dhahabu na almasi ndani yake. Kilifungwa vizuri na mnyororo na ndani vitu hivyo vilikuwa na thamani ya dola milioni 60. Miaka ya 1800 vilizikwa huko Virginia lakini mpaka leo hii hakuna mtu anayejua mahali vilipozikiwa. Vimetafutwa mpaka leo hii sehemu hiyo imekuwa siri.

Dhahabu nyingi kupotea nchini Marekani

Marekani ilijikusanyia dhahabu zake nyingi sana, zilikuwa na thamani ya dola milioni 400. Zilihifadhiwa vizuri kabisa lakini baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kutokea mwaka 1861 chini ya rais Jefferson Davis, dhahabu hizo zikapotea na mpaka leo hakuna anayejua mahali zilipo. Wahuni walipita nazo baada ya vita kumalizika.

Meli ya dhahabu ikapotea baharini

Hiyo ilitokea mwaka 1511. Kulikuwa na meli ya Ureno iliyobeba dhahabu zenye thamani ya dola bilioni moja, ilipotea baharini na mzigo huo mkubwa na kwa bahati mbaya sana hakuna anayejua mahali ilipopotelea. Je, ilizama? Ilitekwa ama ilikuwaje? Nobody knows.

Meli ya almasi nayo ikasepa

Miaka ya 1600 napo meli ya Waingereza ikapotea baharini. Ilibeba almasi za Kihispania zenye thamani ya dola bilioni 1.25. Ilikuwa meli ya kifalme, ikapotea baharini ikiwa na mzigo huo mkubwa. Ilitafutwa kila kona, haikuonekana. Taarifa zilisema tu kulikuwa na wajanja waliamua kusepa nazo. Hapo ndipo ninapowakumbuka akina Jack Sparrow

Aztec treassure nayo ikasepeshwa

Yaap! Kulikuwa na dhahabu kubwa ya Montezuma Aztec ambayo ilikuwa na thamani ya dola bilioni 3, nayo iliwahiwa na wana, meli ikapotea na dhahabu hiyo haikuonekana tena mpaka leo.

Mji wenye dhahabu nayo umepotea

Kulikuwa na mji uitwao Paititi ambao ulikuwa na dhahabu nyingi sana mpaka kuitwa mji wa dhahabu. Inakadiriwa kuwa na dhahabu zenye thamani ya dola bilioni 10 ila cha ajabu mpaka leo hakuna ajuaye huo mji ulikuwa wapi. Umejaa dhahabu ila nao umepotea. Wanahistoria waliingia chimbo na kuutafuta kila kona wakaambulia patupu.

Wahispania nao walilia sana

Wakati mapigano yanaendelea mwaka 1708, Whispania walikuwa na meli yao iliyokuwa na dhahabu nyingi sana zenye thamani ya dola bilioni 20, meli ilizamishwa huko pwani ya Colombia na mpaka leo dhahabu hizo hazijaonekana tenaaaaa.

Wajapan nao hawakuachwa na kisanga hiki

Wakati wa mtawala wa Japan aitwaye Yamashita, aliamua kukusanya dhahabu nyingi sana mpaka kufikia za dola bilioni 400. Baada ya dita kutokea, jeshi lake likaamua kuzichukua dhahabu hizo na kwenda kuzificha huko karibu na Ufilipino na mpaka leo hakuna anayejua mahali dhahabu hizo zilipofichwa. Zimetafutwa, hazijaonekana..
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

Utajiri mkubwa ambao mpaka leo haujulikani upo wapi Kuna madini mengi  >>> https://gonga94.com/semajambo/utajiri-mkubwa-ambao-mpaka-leo-haujulikani-upo-wapi-kuna-madini-mengi

#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Maoni

You're not logged in
Click here to login and comments
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
gonga94 official track
ZETU
SIMULIZI NA SAUTI ZETU
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Tangazo - MTAKATIFU GEMMA UTUOMBEE SHIRIKA LA MASISTA WA MT GEMMA WA DODOMA
MTAKATIFU GEMMA UTUOMBEE SHIRIKA LA MASISTA WA MT GEMMA WA DODOMA
MTAKATIFU GEMMA UTUOMBEE SHIRIKA LA MASISTA WA MT GEMMA WA DODOMA
Tunao Wapenda ndio wanao tuua baba
Sikiliza Wimbo Kamili

RATIBA YA SIMULI ZETU

Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.


Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest