MASHUSHUSHU WA MOROCCO KAZI YAO IMEKUWA NGUMU.
1.Walizoea kumuona YUSUPH KAGOMA kwenye Shilling 6 ila Fadlu Davids kampa nafasi zaidi Augustine Okajepha na kazima vizuri kila alipopewa nafasi,Hapa sijui wanaenda na faili na Kagoma au Okajepha?
2.JOSHUA MUTALE ndo stori ya mjini kwenye mechi za viporo vya Simba kazima sana tofauti na matarajio ya wengi amebadilika ghafla kama Zuena wa Mondi hapa sijui RS Berkane watajipanga kumzuia Mutale au Kibu Denis
3.ATEBA NA MUKWALA wote wa moto kila aliyepewa nafasi kafanya kweli sasa hapa sijui RS BERKANE wanaenda na faili la nani?
4.KARABOU CHAMOU kwenye mechi zilizopita za CAF confederation Cup amezima pacha na Abdulrazack Hamza ila kwenye mechi za viporo hajapewa dakika nyingi sana Hamza na Che Malone wamecheza sana pale nyuma,Hapa napo lazima wachanganyikiwe hawajui Fadlu atakujaje?
5.AHOUA kama kawaida yake kuna muda Simba ipo salama kwenye mikono yake akiwa kwenye form yake kila kitu kwake kinakuwa bora wanaondoka jina lake kama top scorer wa Ligi kuu hapa napo wanazidi kuchanganyikiwa hawajui mtu hatari kwenye goli ni Ahoua au Ateba na Mukwala.
5.Kwenye Midfield ndo wanachanganyikiwa kabisa maana Debora Fernandez kazima vizuri dhidi ya Pamba Jiji hapohapo Okajepha alikuwa kwenye kiwango bora kabisa bila kumsahau Fabrice Ngoma ambaye alifunga dhidi ya JKT Tanzania.
6.VALENTINE NOUMA amecheza dakika nyingi sana kwenye hizi mechi za viporo kuliko ZIMBWE JR hapa napo Rs Berkane sijui wataenda na faili lipi maana hawajui bwana Fadlu Davids atakujaje kwenye left back.
7.ELIE MPANZU KIBISIWALA kapewa mapumziko ya kutosha energy bado ipo wakati ambao mafaili ya Waarabu yanawaza kama Joshua Mutale anaweza kupewa nafasi basi faili la Elie Mpanzu wawe nalo karibu huyu moto wake upo pale pale na pia wasimsahau Kibu Denis maana yeye na Waarabu wana ugomvi mkubwa ???? mwisho kabisa watambue Ladack Chasambi amerudi kikosi na hata Edwin Balua pia yupo gado.
WEWE NDO UNGEKUA MUARABU UNGEENDA NA FAILI LIPI?.
Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.
Maoni
Click here to login and comments