Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94

SITASAHAU YALIYONIKUTA BAADA YA KUMSOMESHA MPENZI WANGU ????????. Sehemu ya Kwanza ( 1 ) *************

18th Apr, 2025 Views 78

SITASAHAU YALIYONIKUTA BAADA YA KUMSOMESHA MPENZI WANGU ????????.
Sehemu ya Kwanza ( 1 )
*************
@Kila Mtu
????????????????????????????????????????????????????????
Ilikuwa ni Tarehe 25 kwenye mwezi wa kumi na Moja kama sijakosea, Mimi na Rafiki Yangu Muba tulikuwa tumesafiri kutoka Morogoro Wilaya Ya kilosa Maeneo Ya Dumila mpaka Mbeya, na Lengo la kwenda Mbeya Ilikuwa ni Mahafari Ya Chuo kikuu Cha Mzumbe kilichopo Mbeya, ilikuwa ni Mahafari ambayo Mpenzi Wangu Frida ambaye huwenda nilimpenda kuliko Nilivyo jipenda Mimi alikuwa anasherehekea kuhitimu masomo Yake Mara baada ya kusomea Shahada Ya Uongozi wa Umma (Bachelor of Public Administration) Kwa Miaka Mitatu.
Siyo kwamba Frida alikuwa kanialika Labda kwamba niende ama Laaa, ila alikuwa amenipa taarifa tu kwamba Kuna Mahafari, Basi Mimi na mwanangu Muba katika kushauriana tuliona itakuwa vyema endapo tutasafiri kwenda kumuunga Mkono kwenye Sherehe Hizo, Maana Hata Hivyo asilimia kubwa mpaka Frida anafika levo ile Mimi Ndo nilikuwa nimegharamia.
Siku zote Siku mbaya Dalili Zake huonekani asubuhi, na Dalili ya Mvua Siku zote ni Mawingu, Kwanza nakumbuka Siku Hiyo Dalili mbaya naweza Sema zilianzia Toka kwenye Gari, maana Siku hiyo tunasafiri kwenda huko Mbeya Ndo Siku ambayo Hata Dada Yake na Frida pamoja na Bibi Yake walikuwa nao wanasafiri na tulijikuta tunapanda Gari Moja Wote pasipo kujua!.
Na Dada Yake Frida alipo niona aliniuliza naenda Wapi, basi Jibu nililo mpatia ni kwamba wanako elekea na Mimi ndo huko Huko naenda, Lakini baada ya Jibu Hilo kiukweli safari nzima Dada huyo pamoja na Bibi Yake walikuwa wanatuangalia vibaya Muno yaani kama wana chuki na Sisi au hawajapenda kabisa Sisi kwenda huko kwenye Mahafari!.
"Oyaa!! Baloteli mwanangu una uhakika kabisa Frida atafurahia Sisi kuwepo huko kwenye Mahafari, maana naona Fina na Bibi Yake wanatuangalia vibaya Muno!"
"Oyaa Muba we Kausha Hata usiwaangalie! Mimi Najua Frida ananipenda na hawezi kwazika Kwa Mimi kwenda kwenye Mahafari Yake, kwanza itakuwa kama surprise naamini atafurahia Muno kuniona!"
"Daaaaaaa!! Sema haina noma Frida namuaminia ila Duuuuuu huyo mbibi na Fina wanavyo twangalia Sasa kama hawajafurahi hivi kutuona!"
Hayo yalikuwa mazungumzo Yangu Mimi na mshikaji Wangu Muba!.
Basi Safari ile ilikuwa ya masaa kadhaa, nakumbuka Mbeya tuliingia Mida ya Saa Kumi na Moja za Jioni, Lakini Dalili mbaya zilizidi zaidi kuonekana baada ya kufika Stendi Kuu ya Mbeya!.
Baada ya kushuka tu kwenye Gari nilimuona Fina na Bibi Yake wanaangaza Huku na Kule kana kwamba wanamuangaza Mtu ambaye kaja kuwapokea, ni kweli baada ya dakika kadhaa niliwaona wakibeba mabegi na kuelekea taxi zilipo, nilipo piga Macho Kwa mbali nilimuona Frida akiwa na Rafiki Zake kama wawili hivi, kwanza Macho Yangu na Macho ya Frida viligongana baada ya Hapo Frida alikwepesha macho na kujifanya hajaniona.
Fina na Bibi Yake walipokelewa mabegi na Frida baada ya Hapo Wote Kwa pamoja walizama kwenye taxi na kuondoka, kiukweli nilijisikia vibaya Muno, niliamini huwenda Frida Hajaniona kama ni Mimi Ndo maana kapotezea, kwanza sikutaka Hata kumshirikisha Muba kile kitendo, maana mchizi Wangu alikuwa ni Mtu wa maamuzi magumu, huwenda ningemwambia pale pale angenambia tugeuze turudi!.
Mimi na Muba Wote tulikuwa Wageni kabisa ndani ya Jiji la Mbeya, yaani hakuna ambaye alikuwa amewahi kufika, basi ilibidi tuulize Chuo Cha Mzumbe kilipo, Waungwana walituelekeza vizuri kabisa na walitushauri tupande Bodaboda maana Kwa Mguu ni mbali kidogo!.
Ni kweli Mimi na Muba tulipanda bodaboda mpaka Maeneo Ya Forest ambako Ndo chuo Cha Mzumbe kilipo, ilikuwa ni kama Saa Kumi na Mbili na madakika hivi, kigiza kilikuwa kimeanza kuchanganya Huku kibaridi nacho kikiwa Cha kutosha!.
Kwakuwa Mahafari yenyewe ilikuwa Siku ya Kesho Yake, ilibidi Mimi na Muba tutafute sehemu ya kulala Kwa Siku Hiyo na kweli kuna Guest karibia na maeneo ya chuo tuliipata!.
Sasa baada ya kuwa nimetulia Majira ya usiku niliamua nimpigie kipenzi Changu Frida ili nimpe taarifa,Japo nilikuwa naamini lazima Dada Yake na Bibi yake wamempa taarifa, Lakini nilitaka na Mimi nimwambie kivyangu!.
Kiukweli nilipiga Simu Siku hiyo mpaka Simu yenyewe Nahisi ilinichoka, yaani nilipiga Simu mpaka Ilianza kupata Moto, Frida hakupokea Simu Yangu Hata Mara Moja, Mwishowe Simu iliacha kupatikana!.
Kiukweli nilijikuta Mwili mzima umeanza kutoka Jasho, yaani na baridi lote la Mbeya Lakini Mimi nilikuwa natiririkwa na Jasho la kutosha, kwanza Hasira ambayo nilikuwa nayo ilikuwa Juu Muno!.
Mpenzi Msomaji Najua unajiuliza Nilikuwa najiamini Nini mpaka kuja kwenye Mahafari pasina Hata kualikwa na kwa Nini nilikuwa na hasira, Ngoja nikurudishe Nyuma kidogo, hakika Hii ni Huzuni huwenda ukatokwa na Machozi kabisa.............
Mimi naitwa Jupita Matandu ni Mzaliwa wa Kilosa Maeneo ya Dumila, Kwa Baba na Mama tulizaliwa wawili tu, Mimi na mdogo Wangu wa Kike anaitwa Febi!.
Nilisoma Shule ya Msingi Dumila na baada ya kumaliza Darasa la Saba nilifanikiwa kujiunga na Sekondari ya Dumila! Hapo Ndipo nilipo kutana na Binti aliye Julikana Kwa Jina la Frida, kiukweli Frida alikuwa ni Binti mwenye akili Muno pale Shuleni, na akili Zake zilifanya Mimi niwe najipendekeza kwake ili awe ananifundisha fundisha!.
Ni kweli baada ya kufika kidato Cha Pili urafiki Wangu na Frida ulizidi kuwa mkubwa na kilicho Fanya urafiki wetu kuwa mkubwa ni kwamba Mimi nilikuwa Masta wa kucheza Mpira, yaani nilikuwa nacheza Mpira kuliko Kawaida kiasi kwamba Shule za jirani wakiambiwa wanacheza na Shule yetu wote walikuwa wananiwaza Mimi, Yaani nilikuwa fundi kiasi kwamba nilipewa Jina la Utani la Baloteli ambalo Mwishowe Ndo lilikuja likavuma zaidi kuliko Hata Jina Langu la Jupita.
Basi tulivyo Fika kidato Cha Tatu Kwa bahati mbaya Mama Yake na Frida alifariki Dunia, na Mama huyo Ndo alikuwa kila kitu Kwa Frida maana Baba Yake na Frida alikuwa ashafariki Muda Sana!.
Baada ya Mama Frida kufariki maisha ya Frida yalianza kuwa magumu Muno, maana ilibidi Frida na Dada Yake Fina waanze kulelewa na Bibi Yao ambaye naye alikuwa hajiwezi kila kitu!, Dada Yake na Frida ambaye ni Fina ilibidi aache Shule ilimladi aweze kufanya vibarua kusaidia familia! Na Dada Yake Huyo aliacha shule akiwa kidato Cha Nne, na ilikuwa Rahisi kuacha Shule Kwa sababu hata hivyo Fina alikuwa akili za Darasani Hana, yaani walikuwa ndo wale wanaosindikiza wenzao Shuleni, aliona ni Bora aache ili amsaidie mdogo Wake Frida ambaye huwenda alikuwa na akili Shule nzima!.
Basi maisha yaliendelea tukiwa tumemaliza kidato Cha Tatu kuingia Cha Nne, baadhi ya Rafiki Zangu walinishauri nimtongoze Frida, kama tujuavyo marafiki wanavyo juaga kujaza maneno!.
"Oya Baloteli unakwama wapi, Demu anaonekana anakuzimikia kabisa yule, Wewe tupia nyavu!"
"Tuna uhakika yule hawezi kuruka kamba!"
Hayo ni baadhi ya maneno ya ujazo kutoka Kwa washikaji Zangu, na kweli maneno hayo yalifanya nivimbe kichwa na kumtongoza Frida!.
Kiukweli mwanzo Frida aligoma Kwa Msisitizo Muno kwamba Yeye hajafuata Mapenzi Shuleni Bali masomo, Lakini baada ya Frida kushauliwa na Dada Yake Fina aliamua kunikubalia, niligindua tu Fina kamshawishi mdogo Wake anikubalie Kwa sababu ya vimali vya nyumbani, maana kiukweli nyumbani tulikuwa tunajiweza Japo Siyo Sana!.
Mapenzi Moto Moto yalianza kati Yangu Mimi na Frida, kiukweli nilitokea kumpenda kupita kiasi, yaani Muda Wote nilikuwa nasafiri mpaka Kijiji Cha Pili Kwa kina Frida.
Hatimaye tulimaliza kidato Cha Nne, Hapo Ndo mapenzi yalizidi kuwa Moto Moto Mara baada ya kuonja Tamu ya Frida na nakumbuka Mimi Ndo nilikuwa Mwanaume Wake wa kwanza kumuonja. Yaani asubuhi na mapema nilikuwa nawahi kuondoka nyumbani mpaka Kwa Bibi Yake na Frida.
Nilijikuta nimeacha kufanya Kazi nyumbani badala yake nikawa nafanya Kwa kina Frida!.
Yaani nyumbani kulikuwa na mashamba kibao ya kulima, Lakini nilikuwa nawahi kulima Kwa kina Frida, kitendo hicho kilifanya Baba Yangu kunigombeza Muno na kutishia kunifukuza nyumbani.
Basi miezi kadhaa ilipita, baada ya matokeo kutoka kiukweli nilifurahi Muno, Siyo kwamba nilikuwa nafurahi Kwa sababu nilikuwa nimefaulu Bali furaha Yangu ilikuwa ni kuona Frida kafaulu kwenda kidato Cha Tano!.
Mimi nilifeli tena vibaya Muno, Lakini wala sikuumizwa na kufeli Kwangu Kwa sababu niliona kufaulu Kwa Frida Ndo kufaulu Kwangu!.
Basi baada ya Muda kupita Frida alipangiwa kwenda kusoma Songea Girls iliyopo Songea mkoa wa Ruvuma.
Kiukweli ilikuwa changamoto Kwa familia ya kina Frida kumudu Gharama, maana mahitaji yalikuwa mengi, pia changanya nauli na Gharama zingine.
Dada Yake na Frida alikuwa ni Mtu mjanja mjanja wa maneno matamu, basi Kwa sababu Yeye Ndo alikuwa kama kichwa Cha familia aliamua kunifuata Siku Hiyo kunipangilia.
"Baloteli najua unampenda Muno mdogo Wangu, na unajua Wewe Ndo utakuwa Mume wake wa maisha Yake, na mdogo Wangu anavyo kupenda mpaka Usiku huwaga anataja Jina lako akiwa usingizini, najua mdogo Wangu akifanikiwa na kupata maisha mazuri atakaye faidika zaidi ni Wewe! Kwa Hiyo kitu ambacho nakuomba jitahadi ufanye Namna tupate pesa Frida aende Shuleni, Mimi hapa nilipo ninayo Tsh elfu hamsini tu, na nimepiga mahesabu ni Kama Tsh Laki Tatu zinahitajika!" Hayo yalikuwa maneno matamu ya Fina, kiukweli nilijisikia fahari Muno kusikia mtoto Frida huwaga ananiota usiku, Japo kuwa nilikuwa sina Kazi Yoyote ya kuniingizia kipato ila nilimuahidi Fina kwamba hiyo Pesa ntaipata tu!.
Basi Siku zilisogea hatimaye Sasa ule Muda ambayo ilitakiwa Frida asafiri kwenda Shule ulifika! Kiukweli nilikuwa sikubali kabisa kuikosa pesa ya kumpatia Frida!.
Nakumbuka pale nyumbani palikuwa na Duka la matumizi ya Nyumbani, Siku Hiyo wazazi Wangu wakiwa shambani niliamua kuingia Dukani kiwizi wizi, maana nilikuwa nimekatazwa kabisa kuuza Duka, Bali mdogo Wangu Febi Ndo alikuwa anaruhusiwa tu.
Mwanaume nikiwa sijali nilivuta Droo kwenye Duka na nilibeba Pesa zote ndani ya Droo, baada ya Hapo nilizunguka upenuni kuzihesabu, zilikuwa kama TSH elfu 80 hivi, niliona hiyo haitoshi, nilizama Tena ndani niliamua kuingia chumbani Kwa Wazazi Wangu, nilipekenyua mpaka nilipata wanapo hifadhi Pesa!.
Nilichukua Pesa Zote ambazo nilizikuta, nakumbuka zilikuwa zimewekwa kwenye kisado kidogo alafu zikawekwa Chini ya kitanda!.
Baada ya kuhesabu Zile Pesa nilikuta zipo kama Laki mbili na Nusu Hivi changanya na ile ya Dukani zilikuwa zinatimia kama Laki Tatu na kitu.
Basi nilichukua Laki na Nusu na kuiweka pembeni, zile zilizo bakia nilizibeba ili nikarudishe chumbani ili nisije shitukiwa Sana!.
Bahati mbaya Wakati nataka kurudisha nilikuta Wazazi Wangu wamerudi Kwa hiyo nilishindwa kuzirudisha!.
Baada ya Hapo nilielekea mpaka Kwa kina Frida, nilimpatia Frida pesa zote, yaani hata Zile zingine Nazo nilimpatia Huku Bibi Yake na Dada yake wakinisifu Muno kwamba Mimi ni kijana mwenye Upendo mkubwa na Bila Shaka ntamuoa mtoto Wao!.
Siku Hiyo nilirudi nyumbani majira ya Saa Tatu Usiku, niliulizwa kuhusu Pesa zilizo potea Dukani kiukweli nilibisha Muno Siku Hiyo na bahati mbaya au nzuri Bado walikuwa hawajaangalia hata chumbani kama Nako Pesa zimeibiwa, kwakuwa kulikuwa hakuna ushahidi niliponea chupu chupu!.
Basi baada ya Siku mbili Frida alisafiri kuelekea Huko Shuleni na Mimi nilbaki nakenua tu Meno nikijiona shujaa!.
Baada ya Siku kama mbili Hivi Baba aligundua kwamba Pesa Zake kwenye kisado zimeibiwa, Hakika Siku Hiyo Baba aliwaka Muno yaani Mimi na mdogo Wangu tulipigwa kipigo Cha mbwa Koko, Lakini tulikataa kutoziona zile Pesa na pia Mama alisaidia kututetea kwamba hatuna tabia ya Wizi Bali huwenda kuna Mwizi alikuja.
"Okay Sasa nimechoka kuibiwa, Awamu hii lazima niende Kwa mganga, atapatikana tu aliyeziiba!" Hiyo ilikuwa Kauli ya Baba akiwa na hasira, kiukweli Kauli hiyo ilifanya Macho yanitoke kama nimedungwa na sindano matakoni!.
Je ipi hatima ya Kijana Baloteli au Jupita!? Kwa nini anasema hatasahau, yapi yalimkuta!?? .......???????? Nyieeeee....Mambo ni ya motooo.???? Kwani wewe auogopi Usipite bila kulike na kukomeniti fanya ku share kabisa ili sehemu inayofuata isikukose maana ndiyo sehemu balaaa????????????????????????????????
..ITAENDELEA...... Hii ni bonge la simulizi isikubali ikupite.
@wafuasi
#itaendelea_story_ni_kali_sana?
Mkiwa wavivu kucoment namimi nakuwa mvivu kupost hivyo comment kwa wingi jamani ili mnie mizuka
# PIA USISAHAU KUNI FOLLOW MIMI KULUTI MC ILI USIWE UNAPITWA NA STORY ZANGU FAIDA YA KUNI FOLLOW NI KUWA WA KWANZA KUPATA STORY KILA NINAPO POST
@everyone.

Za hivi punde ni za 🔥🔥🔥 | Sema Jambo
Your settings were saved successfully!
Something went wrong!
You're not logged in
Click here to login and post your story

Welcome gonga94 Continue reading the various stories available here. Click here. Are you an artist then create an account here Signup/Login


mjukuu rewards 100
 

NASEMA KWA MAMA SEHEMU YA 10*

mjukuu rewards 100
 

NITAKUPA USINIROGE (1)

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP: 19

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP: 18

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP: 17

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP: 16

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 42

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 41

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 40

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 39

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 38

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 37

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 36

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 35.

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 34

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 33.

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 32

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 31

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 30

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 29

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 28

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 27

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 26

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 25

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 24

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 23.

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 22

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 21

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 20

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 19.

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 18

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 17.

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 16

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 15.

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 14

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 13.

majario rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 12

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 11.

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 10

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 09

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 08

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 07.

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 06

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 05.

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 04.

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 03

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 02

mjukuu rewards 0
 

PENZI LA MHALIFU 01.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 22.

mjukuu rewards 0
 

NASEMA KWA MAMA **** 3--4

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP: 15

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP: 14

mjukuu rewards 0
 

WIFI KHAA 04

mjukuu rewards 0
 

NASEMA KWA MAMA* 1-----2

mjukuu rewards 0
 

KIJIJI CHA WAGENI! 04

mjukuu rewards 0
 

MKE WA MGANGA ( 1——5 )

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP: 13

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 21.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 20.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 19.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 18.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 17.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 16.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 15.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 14.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 13.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 12.

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 11

mjukuu rewards 0
 

WIFI KHAA 02 #Tulipoishia

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 10

mrindia rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 09

mjukuu rewards 0
 

*MY CHUNUN* 01

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP: 09

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA. EP: 08

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP 07

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP 06

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP 05

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA. EP: 4

mjukuu rewards 0
 

SHANGATISA EP: 3

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA EP: {02}

mjukuu rewards 0
 

SHANGA TISA. EP: 1

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 08

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU (06 & 07)

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 05

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 04

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 03

mjukuu rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU (01& 02)

mrindia rewards 0
 

RUNGU LA KIPOFU 01

mjukuu rewards 0
 

MTOTO WA GETI KALI 1 - 6

mjukuu rewards 0
 

MIMI SIO KICHAA

mrindia rewards 0
 

SITOMWACHA HATA IWEJE

mjukuu rewards 0
 

BINTI MCHAWI

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest