@Kila Mtu
🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥🥥
Ukisikia mtaa wa saba ni mtaa wa saba kweli ni mtaa iliyochangamka matukio ya kila aina yanapatikana kwenye huo mtaa. Ukipita huku unakuta na wamama wanasutana au vigodoro, ulitokezea kule unakuta watoto wakicheza gololi , kuikata kushoto wavuta bangi na vibaka yani kwenye huo mtaa hakuna mtu mzembe mzembe kwanza wenyeji wote wanajuana akija mgeni anajulikana wanaanza kuulizana huyu katoka wapi? Au kaka kwa nani?
Haya sasa tuanze...
Ilikuwa majira ya saa kumi na mbili jioni kijana Fariss alikuwa anatoka kazini , kwenye gari yake aina ya range Rover velar nyeusi. Kwenye gari alikuwa na rafiki yake kipenzi Meyael.
Siku hiyo barabara ilikuwa na foleni kubwa sana walisimama kwenye foleni karibia nusu saa. Meyael alichokaa kukaa pale kwa muda mrefu akamwambia Fariss.
" Fariss huku kuna foleni sana tutakaa sana hapa kwanini tusipite barabara ya chini? Fuata hiyo gari inayoingia kwenye barabara ya vumbi alisema Meyael
" Alafu ni kweli sijui kwanini sikukumbuka hili mapema.
Alisema fariss huku akijaribu kutoka kwenye foleni akaingia kwenye sheri moja na badae akafuatia barabara ya vumbi iliyokuwa inapita kwenye mitaa iliyokuwa na nyumba nyingi za watu.
Fariss aliendesha gari kwa mwendo wa kasi alijisahau kuwa yupo kwenye barabara za mtaani huku akisikiliza muziki kwa sauti ya juu kidogo.
Wakati huo huo upande wa pili wa barabara kulikuwa na msichana mmoja anavuka barabara huku mkononi kwake akiwa kashikilia kipande cha gazeti lililofungwa .
Mara Meyael akasema kwa sauti ya hofu.
" Fariss unagonga mtu. Ilikuwa bahati fariss alifunga breki na gari ikasimama.
Fariss na Meyael walishuka haraka kwenda kumuangalia mtu waliotaka kumgonga. walimkuta mwanadada mmoja akiwa kachuchumaa na gazeti lake likiwa chini vitu vyake vyote vilimwagika.
" Wewe dada kwani ulikuwa huoni kama gari inakuja unavuka barabara kwa maringo kama vile anamiliki baba yako. alisema fariss huku akimuangalia yule binti kwa hasira.
Yule binti alisimama huku akimuangalia Fariss kwa macho ya ukali , alishika kiuno na kusema
" Wewe baba naomba ufungue huo mdomo wako mchafu kama kuongea hata mimi najua sana kuongea na isiombe nikaufungua huu mdomo wangu utaomba poo ...
alafu hapa ulipo kumbuka ni mtaani kwangu na mimi ndio Salma alwatan wa huu mtaa wa saba.
" Vitoto vya uswahilini bwana sijui vipoje?
" Koma wewe mtoto unaninyonyesha ? Alafu usijitie sana kuongea umeona mboga yangu imeanguka kwenye mchanga nataka mboga yangu haraka sana kabla sijakujazia nzi hapa.
Fariss aliangalia chini kisha akamuangalia Meyael wakacheza kwa dharau.
" Utumbo, miguu ya kuku ndio mboga? Wenzio wanakula kuku nyie mnaambulia hizo takataka hata nikimpa mbwa wangu hali hizo takataka.
Salma alikunja uso wake kwa hasira kisha akanyoosha mkono wake na kuumkunja Fariss.
" Oya hebu niache...
" Sikia hivi utanifanya nini na nipo mtaani kwangu.
" Wewe mtoto wa kike acha Shobo, usishobokee watu usio wajua. Alisema Meyael.
" Wewe tena nyamaza sitaki ujichanganya kwenye hii kesi. Maana sishindwi kuwachanganya wote wawili.
Meyael alitaka kunyanyuka mkono lakini Fariss alizuia maana alijua ikiwa atampiga yanaweza kutokea mengine.
Baada ya fariss kuona Salma hatanii akauliza
" Unataka nini sasa?
" Umetaka kunigonga hili ninesamehe , lakini hili la kuniharibia mboga zangu utalipa ili iwe fundisho siku nyingine usiweze kurudia tena kuwa na dharau kwa watu usiowajua.
Fariss alimuangalia alafu akauliza
" Kwani shilingi ngapi?
" Hapa ni buku tu.
" Sikiliza nikwambie kwa hadhi yangu siwezi kutoa hela yangu nikanunue miguu , maeneo haya wapi kuna super market?
" Kule barabarani.
" Panda kwenye gari nikakuchukulie kuku mzima. Hata kama utataka kuku wa KFC nitakununulia. Aliongea fariss kwa kujiamini ili kuweka heshima.
" Afadhali neema imenishukia siku ya leo.
Salma alipanda kwenye gari bila uwoga wowote Fariss aliendesha gari kwa kufuata maelekezo ya Salma mpaka wakafika super market.
Walishuka Fariss pamoja na Salma wakaingia super market .
Fariss alitoa hela na kununua kuku mzima na kumkabidhi Salma.
" Shika leo kusheherekeae pamoja na majirani zako.
" Unanipa kwa masimango unafikiri nita susa? Mwenzio sina tabia ya kususa kwaheri.
Salma alichukua mfuko wa kuku na kuondoka huku Fariss akimsindikiza kwa macho.
" Mshamba mmoja muone vimiguu vyake.
Baada ya hapo Fariss alirudi kwenye gari.
" Mmmh ya leo kali. Alisema Meyael.
" Nimekutana na slay queen wa buza. Na njia ya huku sipiti tena tusije tukakutana na balaa lingine.
Meyael aliishia kumcheka.
Fariss aligeuza gari na kuelekea njia nyingine.
Walifika sehemu Fariss alitaka kuwasiliana na mtu alitafuta simu yake alipokuwa kaiweka lakini hakuiona. Alisimamisha gari na kuendelea kutafuta.
" Vipi unatafuta nini?
" Siioni simu yangu.
Walitafuta kila sehemu simu haukuwepo.
" Meyael naomba unipigie.
Meyael alichukua simu akajaribu kupiga simu ilikuwa inaita lakini haikusikika ikiita ndani ya gari.
Fariss na Meyael waliangaliana , Meyael akasema
" Slay queen kachukue simu yako .....🤔🤔 Nyieeeee....Mambo ni ya motooo.😂 Kwani wewe auogopi Usipite bila kulike na kukomeniti fanya ku share kabisa ili sehemu inayofuata isikukose maana ndiyo sehemu balaaa🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥.
Jamani comment zenu zikiwa nyingi naleta mwendelezo fasta.
   
Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.