Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Had Se Bhi Zayada Qayamat

SEHEMU YA TANO* SALMA MTAA WA SABA 😴

3rd Aug, 2025 Views 31


Farris alienda kuchukua gari baada ya dakika kadhaa alifika na gari yake na kusimama mbele ya Salma.
Salma alifungua mlango wa gari na kupanda na kukaa kwenye siti ya pembeni ya dereva.
Farris aliwasha gari wakaanza safari ya kuelekea mtaa wa saba.
Wakiwa njiani kila mmoja alikuwa kimnya.
Salma aliamua kuvunja ukimnya kwa kusema.
" Umeadimika sana hautaki kurudi uswahilini kwetu .
Fariss alitabasamu kisha akasema
" Hakuna ulichoniibia ningeweza je kurudi tena?
Salma aliishia kucheka.
" Ulisema labda uniibie moyo wangu lakini nilipokaribia kuutoa na kukukabidhi uliamua kuondoka.

Waliendelea kupiga story za kuchokozana walipokaribia kufika maeneo ya kwa kina Salma Fariss alichukua simu yake na kumpa Salma.
" Weka bamba yako hapo.
Salma alipokea na kuandika namba yake ya simu , alipomaliza alimrudishia simu yake.
" Unauhakika ni namba yako na sio namba ya gari?
" Hahaha ni namba yangu na jina nime save.
" Ume save nani?
" Malkia wa mtaa wa saba.
Fariss alimuangalia kisha aliachia tabasamu.
" Natamani kuwa na wewe muda wote maana mambo yako huwa yananifanya nifurahie sana.

Wakati huo walikuwa wamefika na gari ilisimama pembeni lakini bado waliendelea kuongea na Salma alishawahi kuwa anamuwahi Abuu asije akajua hayupo nyumbani.

Wakati wanaendelea kuongea dirisha la upande wa Fariss liligongwa.
Fariss na Salma waliangalia kwa makini . Fariss alitaka kufungua lakini Salma akamuwahi.
"Acha usifungue.
" Unajua ni nani?
" Ndio. Alijibu Salma huku akifungua mlango wa gari na kushuka.
" Haaaaaa kumbe ni wewe dogo unatoka wapi saizi?
Ilikuwa ni sauti ya Abuu akiongea kwa ukali.
Salma alimuangalia Abuu bila kujibu. Abuu alimfuata aliposimama na kumsukuma pembeni akachungulia kwenye gari.
" Wewe ndio unamvuruga dogo na kumfanya asittilie nyumbani si ndio. Hebu shuka haraka.
" Abuu hebu muache.
Abuu alimgeukia Salma
" Oya kaa mbali na hili acha niongee na huyu mzinifu mwenzio.
Oya toka humo ndani kabla sijapianzisha varangati langu.
" Sikiliza bro mimi nimempa lift tu....
" Acha kujipanga kishamba hivyo shuka.
Fariss akaona isiwe tabu alishuka kwenye gari na kukutana na vijana wengine wanne wakiwa wamevaa kihuni na mmoja alikuwa kashika panga.
" Songea hapa unaogopa ogopa nini mtoto wa kiume.
Fariss alisogea karibu na Abuu.
" Na wewe songea hapa.
Abuu alimuita Salma.
" Abuu tuheshimiane na mimi sio mtoto wa kusema unifuatilie na kunichunga endapo utamdhuru huyu kaka wa watu nitakutwanga jiwe la kichwa alafu baada ya hapo nitaenda kushitakiwa polisi, alafu huyo sio wa huku ujue baba yake ni mtu mkubwa sana kwenye hili taifa kumgusa tu safari hii unaenda kunyongwa sasa endelea.
Salma alitoa vitisho kumtetea Fariss .
Abuu alimuangalia Fariss kisha akasema.
" Sawa anaonekana mtoto wa kishua sasa ndio azini watoto wa watu?
" Wala sio mzinifu, soja zini nae .
" Sasa ni nani kwako mbona kama una uchanganya?
" Ni mpenzi wangu , mwanaume wangu ninaempenda.
Abuu alimuangalia Salma alafu akasema
" Umakini nini kujifungulia hayo maneno ?
" Ni mapenzi tu kaka naomba utambue huyu ndio moyo wangu popote utakapomuona mtambue kama shemeji yako.
Abuu alimuangalia Fariss ambae alikuwa kimnya muda wote kisha akauliza.
" Wewe unampenda mdogo wangu?
Fariss alimuangalia Salma , Salma alitingisha kichwa akimaanisha Fariss akubali.
" Ndio ni mwanamke ninaempenda sana.
" Sawa nakuacha sababu dogo anakupenda ila usije ukazibgua baba sitajari mtoto wa waziri au raisi nitakufanyia mbaya.
Abuu aliwaangalia wenzie kisha akasema
" Oya twendeni.
Walianza kuondoka huku waliwaacha Salma na Fariss wakiwa wamesimama.
Walifika mbele kidogo Abuu alisimama na kugeuka nyuma.
" Oya bwana shemeji nisababishie ya fegi.
Farris aliingiza mkono mfukoni akatoa kiasi cha pesa ambacho hakuhesabu akampa.
" Asante na unakaribishwa nyumbani.

Abuu alivyoondoka Salma alimgeukia Fariss.
" Uliogopa eee...
" Niliogopa lile panga tu.
" Nisingekubali akifanyie jambo baya alafu nisamehe kwa kusema kuwa ni mpenzi wangu ilikuwa ni njia ya kumfanya aondoke bila kujidhuru.
" Usijali hilo ni swala dogo.
" Mmmmh naona unataka kuwa hapa lakini muda umeenda na mitaa ya huku sio salama sana hasa kwako wewe mgeni .
" Sawa acha niende tutawasiliana.
" Sawa.
Salma aliingia uchochoro ni akaelekea kwao na Fariss alipanda kwenye gari akaondoka huku akiwa na tabasamu na kusema.
" Yani raha tupu shemeji yangu mbabe wa mtaa, mwanamke wangu malkia wa mtaa, aaah yani mtaa wa saba unanikosha.

Full 1000
Whatsp
0784468229.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

SEHEMU YA TANO* SALMA MTAA WA SABA 😴  >>> https://gonga94.com/semajambo/sehemu-ya-tano-salma-mtaa-wa-saba
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Had Se Bhi Zayada Qayamat
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
offa ya msimu wa nanenane
offa ya msimu wa nanenane

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

BLOOD MOON EPISODE 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CHANZO NI BOSS 03

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CHANZO NI BOSS 02

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CHANZO NI BOSS 01

majario rewards 100 Comments 0
 

MTOTO WA MAMA LISHE

majario rewards 100 Comments 0
 

MY LUNA SEHEMU YA : 06

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest