Baada ya Nesi Tina kumchoma sindano ya sumu mgonjwa, akamwambia muuguzaji "haya nishamtibia mgonjwa wako 'una lingine??, hapana nesi nashukuru sana. Tina aligeuka kurudi zake ofisini ,bado aliendelea kuuwazia usiku ule ulioonekana mfupi lakini ulikua na maajabu mengi kwake, alikumbuka pale alipozishambulia nyama pasi kujua ni za binaadamu hadi alipomaliza, akasisimkwa mwili 'mh zilikua tamu, ndio maana Dr mery siku ile alikwenda mochwari kula nyama ya binadamu ila yeye anakula zisizopikwa hiv zina utamu kweli????. Ni mambo aliyokua akiyawaza Nesi Tina .muda ulifika kuwapa wagonjwa dawa, alinyanyuka kurudi tena wodini, alianza kupita kitanda hadi kitanda, alipofika kwa yule mgonjwa aliemchoma sindano yenye sumu, alimkuta muuguzaji .Anaendeleaje mgonjwa wako??, bado amelala nesi. OK muache aendelee kupumzika. Kidogo alimuona mgonjwa mwingine akinyanyuliwa kitandani. Nyie mnampeleka wapi huyo, hamnioni kama nimeanza kugawa dawa?, anataka kwenda chooni kujisaidia. Muwahisheni sasa, mnamchukua taratibu hivyo akijinyea?. Sawa nesi ngoja tumfunge nguo, walipomtoa kitandani, kabla ya kufika chooni akajinyea kwenye kordo. Nesi Tina akawaambia ',nilisema mpelekeni haraka ona sasa alichokifanya ndugu yenu nawaambia mtayazoa hayo,. Nesi bahati mbaya tu naomba maji nisafishe hapa. Usitake kunichefua we mkaka, bahati mbaya kwani huyo amekua mtoto mdogo hawezi kusema, eti unaomba maji!!!!!!!!, unafikiri tuna maji ya kuchezea hapa, nataka iwe fundisho kwa wauguzaji wengine nimekwambia yazoe .akatokea muuguzaji mmoja alimpa ushauri mwenzie " we usibishane na nesi yazoe kwa kutumia nguo. Akaenda kuchukua nguo akazoa kile kinyesi, ndipo akampeleka chooni kwa ajili ya kumsafisha. Baada ya kuzolewa kinyesi, Tina alimwita mhudumu wa wodi ile apige deki. Imekuaje tena Nesi??,. Kuna lipumbavu moja limejinyea hapo nikamuamuru ndugu yake ayazoe. Ahaaa safi Sana Nesi umemkomesha, mambo gani hayo ya kuchefuana asubuhi asubuhi. Nesi Tina alimalizia kugawa dawa akarudi zake ofisini. Samahani nesi " nini tena?. Mgonjwa namuwamsha nimpe chakula hali. We kaka unajua msumbufu Sana au umeniamulia Leo, asubuhi umenibwatiza eeee nikaja kumtibia mgonjwa wako, umekuja tena 'eti mgonjwa haamki iyo inanihusu nini?, nenda kaendelee kumuamsha. Siyo hivyo nesi, mgonjwa wangu anaonekana hayupo kwenye hali ya kawaida. We hali ya kawaida unaijua???. Tina alishajua nini kinaendelea, alitabasamu kimoyo kimoyo akisema nimekukomesha mbwa we, nesi huwa hafokewi kaandae mazishi tu. Twende tukamuone. Tina alimuangalia mgonjwa akimgeuza huku na kule hii yote ilikua geresha tu kwani alijua alichokifanya, ngoja nikamwite daktari. Dokta alifika akampima kifuani kuangalia mapigo ya moyo akaona yapo kimya, hii hali imemuanza saa ngapi??, Tina akajibu "asubuhi alinikuta huyu kaka akiniambia mgonjwa wake hali s nzuri ndio nikaja kumchoma sindano. Dokta alimwomba kijana amfate ofisini kwake, alipewa ripoti ya kifo cha ndugu yake 'alilia sana, kurudi wodini alikuta tayari mwili ushapelekwa mochwari .Tina alimwangalia kwa jicho la wizi 'siku nyingine uwe na adabu, unakuja kunikoromea ukifikiri ni nesi wa kawaida .Tina, zamu yake iliisha akarudi nyumbani ,alibadili nguo akaenda kujimwagia maji, aliporudi ndani kufungua kabati achukue nguo akakutana na malundo ya pesa, akiwa bado anazishangaa zile pesa, sauti ikasikika "huo ni mshahara wako kwa kazi nzuri uliyoifanya,umetuletea nyama ,.akajiuliza nyama ",usijiulize wewe, yule kijana uliemchoma sindano ya sumu tumeshamchukua na tayari ameshabanikwa Kama zile nyama ulizokula usiku.Tina akaanza kuzitoa zile pesa akiwa haamini, kwani katika maisha yake hakuwahi kushika fedha nyingi kiasi kile. Loo mi nilijua namkomoa yule kijana kwa kunikaripia kuhusu mgonjwa wake, kumbe nishafanya kazi ya kuzimu hee,. Dokta Mery alitokea chumbani kwa Tina "wacha weee naona unaogelea minoti tu. Tina aliacha kuzihesabu zile pesa akaenda kumkumbatia Mery 'thanks jamani,, umenipa utajiri Mery, ona, ona 'yaani Leo tu mihela mingi hivi je nitakavyokua nikiendelea .Mery akamtania "utakua na mihela hadi utanunua dunia "wakacheka kwa pamoja. Tina acha nikuache si unajua nami naingia zamu. Dokta Merry akiwa ofisini kwake, aliingia mtu wa makamo hivi.shikamoo mzee ", marahaba binti ujambo??, sijambo ' unaumwa nini mzee wangu??, hapana mi si mgonjwa bali ninashida binafsi. Mery alikaa sawasawa kumsikiliza. Yule mzee aliifungua breafkes yake kulikua na noti za shilingi elfu kumi, kumi, zimejipanga, kisha akaifunga. Binti" wewe ni daktari, kuna kitu naomba unisaidie, ukifanikisha hizi pesa ni zako. Dokta Merry alipumua 'akamuuliza kitu gani hicho mzee wangu.
ITAENDELEA
FULL 1000
0699286085.