Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Pyar Ho Jane Dushman

🔞 Onyo: Maudhui ya watu wazima (18+). Tafadhali soma kwa tahadhari. Zawadi Sehemu ya 13

5th Aug, 2025 Views 15

13
Simulizi za john
0789 824 178
1000

Nilitaka kugonga mlango, nifanye fujo kabisa ili mkewe ajue nadanganywa! Mara nikaskia, “Dada, nashindwa kulala, naota ndoto mbaya.” Alikuwa Zawadi Mdogo, nje ya chumba chao kwenye korido karibu na chumba cha wazazi wao. Nikamudu haraka, nikambeba, mara mamake na babake wakatoka—mama amevaa upande wa kanga, baba kaptula tu, akiwa amevimba mbele. Nilizidi kukeruka, nikamudu mtoto chini, nikaingia chumbani kwangu. Walimchukua, wakaingia naye chumbani kwao. Nilijisikia vibaya, mjinga sana. Nikamtumia ujumbe Neema, hakujibu. Nikampigia, hakupokea. Nikaingia kitandani, nikajikunyata.
Mara ujumbe ukaingia: “Bby, usifunge mlango, nakuja.” Ilitoka kwa Scott. Nilijisikia vibaya, nikamtumia: “Achana nami, sitaki!” Akasema, “Nakuja tuongee, mpenzi, usikasirike.” Sikumjibu, nikazima simu. Nikaenda kufunga mlango, lakini nikawaza, nikaufungua tena, nikatoa nguo, nikapanda kitandani kulala. Usingizi ulinipita bila yeye kuja. Nikastuka, nikaenda kusonya, nikafunga mlango na funguo, nikalala hadi asubuhi.
Siku hiyo sikuamka mapema, nilifungua macho saa nne, nikiwa nimenuna hatari. Scott hakwenda kazini, alikuwa mezani na Mama Zawadi, wanakunywa chai. Mama Zawadi akasema, “Boss, ndiyo unaamka? Karibu chai, wafanyakazi wako tumeipikia.” Scott akasema, “Mama Zawadi, tulishaongea kuhusu hili, sipendi unachofanya. Labda anajisikia vibaya?” Sikujibu, nikaenda juu, nikakusanya nguo zangu na za watoto, nikaenda kufua.
Nikiwa nafua, Scott akaja, akasema, “Ndiyo ulifanya nini jana? Mbona ulifunga mlango?” Nikasema, “Shida nini? Ulilala na mkeo, kwangu ulitaka nini?” Akasema, “Naomba tutoke, tuongee mahali, sawa?” Nikasema, “Sina muda.” Akasema, “Naomba, shika hii, nitakuambia niko wapi, nitakueleza kila kitu. Nakupenda sana, bby.” Alitoa shilingi elfu kumi, nikipokea. Akaondoka, kwani alikuwa anaibia kuongea nami.
Nilimaliza kufua, akatoka na gari lake, nikabaki na Mama Zawadi. Nikiingia ndani, akaniita, akasema, “Wewe unajiona nani hapa? Mbona umekuwa na kiburi?” Nikasema, “Naomba niache! Unashindwa kufanya mambo yako hadi unipelembe? Sio kosa langu nimekupita uzuri, acha kunifuatilia, nimekuchoka!” Nikapanda juu, akasema, “Wewe Zawadi unanitukana? Unanijibu hivi?” Sikumjibu, nikaingia chumbani, nikafunga mlango na funguo, nikaoga, nikajiremba, nikavaa jeans na top, nikachukua kioo, nikatia pesa, nikapulizia marashi, nikatoka. Alikuwa amevimba sebuleni, sikumuaga, nikaenda moja kwa moja hotelini ambapo Scott aliniita.
Alikuwa chumbani, nikamkuta nimenuna. Nikasimama, sikutaka kukaa. Akasema, “Bby, naomba ukae, mbona hivi?” Nikaanza kulia. Akasimama, akanifata, akasema, “Unalia nini?” Nikasema, “Nataka kuondoka kwako, sitaki kukaa tena!” Akasema, “Mbona tuliongea tutaishi pamoja?” Nikasema, “Hapana! Haukutimiza chochote ulichoahidi zaidi ya kunilala. Umenidanganya amekuja kwa watoto, lakini unalala naye, mnafanya mapenzi, unaniona mjinga?” Akasema, “Hapana, bby, nielewe. Vikao vimefanyika, nimeambiwa nijifanye mume mwema ili apate kisingizio cha talaka. Nakupenda, sitaishi bila wewe, nipe muda, atazingua, ndipo itakuwa mwisho wake.”
Nikasema, “Unanidanganya, sitaki!” Akasema, “Niambie unataka nifanye nini ujue nakupenda?” Nikasema, “Ulisema utatafuta msichana wa kazi, hujafanya. Ulisema utanisomesha, hujafanya.” Akasema, “Msichana natafuta, nimeambiwa kuna mahali naweza pata waliofunzwa, nipe wiki moja. Kuhusu shule, naogopa utakutana na wadanganyifu wakakudanganya ukaniacha.” Nikasema, “Nitakaa mpaka lini bila kujifunza, nikikaa ndani tu?” Akasema, “Nambie unataka nini?” Nikasema, “Nisomee usecretary.” Akasema, “Hapana, usecretary sitaki, utakuwa chakula cha mabosi!” Nikasema, “Unataka nini sasa?” Akasema, “Kwa sasa nipe utamu, bby.” Nikasema, “Si jana ulilala na mkeo?” Akasema, “Yule hanilidhishi kama wewe.”
Akanivuta, nikampa mauno hadi akaweseka, akisema, “Zawadi, utanitoa roho!” Alilia, kamasi zikamtoka. Baada ya mapumziko, akasema, “Nambie unataka nini?” Nikasema, “Simu ya kutachi, pesa ya saluni, na nguo.” Akasema, “Lilo tu? Sawa.” Nikamkalia tena, nikamudu segere, hadi akafika safari yake. Nikasema, “Simu nataka leo.” Akasema, “Twende tukale, tukanunue.” Tulioga, tukavaa, tukakula hotelini, kisha tukaenda benki, akatoa pesa, tukanunua simu ya laki tatu na nusu, tukarudi hotelini. Saa mbili akasema, “Bby, tangulia nyumbani, nitakuja saa nne, acha nizungumze na washkaji.” Nikasema, “Sawa.” Akasema, “Jitahidi uwe mpole, mtiifu.” Nikasema, “Mkeo akinizingua, sitakaa kimya.” Akasema, “Sawa, bby.”
Tulitoka, alinishusha Mwenge, nikaenda na usafiri hadi nyumbani. Mama Zawadi alikuwa amenuna, akasema, “Ulikuwa wapi? Unarudi saa hizi?” Nikasema, “Samahani, nilitumwa na baba mbali kupeleka mzigo.” Akasema, “Baba gani?” Nikasema, “Baba Zawadi.” Akasema, “Subiri.” Akampigia, akasema, “Baba Zawadi, mwanao mpendwa anarudi, ulimtuma?” Scott akasema, “Nilimtuma Kibaha, labda ndiyo kachelewa.” Mama Zawadi akaniangalia, akasema, “Ondoka hapa!” Nikaingia chumbani, nikiwa na raha, namng’onga kisogoni.
Maisha yakaendelea, nikitoka na Scott, tukipendana, tukifanya yetu kila tukipata muda. Nilijitahidi kuwa na heshima, kwani nili ahidiwa mema. Scott alitafuta msichana wa kazi, nikaanza kushinda Mwenge kwenye duka lake la mikate, keki, biskuti, na vinywaji, akasema ni langu, nitunze. Neema akasema, “Vumilia tu.” Ukaribu wangu na Keanu ulizidi, alininunulia chakula kila siku, akanipa nguo za bure, akiniongoza.
Siku moja, Scott na mkewe walisafiri kwa kina Mama Zawadi, kulikuwa na shida. Nikabaki na Stella (msichana wa kazi) na Masai. Keanu akaniambia twende klabuni, ambapo sikuwa nimewahi kwenda. Nikadanganya Stella na Masai kuwa Neema ana msiba. Nikaenda na Keanu, nikaenjoy, nikanywa pombe, nikachachuka. Usiku, Keanu alinipeleka kwake, tukafanya mapenzi. Asubuhi, nilistuka saa sita, nimechoka kwa ulevi na kumudu. Nikasema, “Keanu, mbona hujanianza?” Akasema, “Ulichoka, bby.” Nikachukua simu, nikaona missed calls za Scott kibao na ujumbe: “Uko wapi? Nakuhitaji nyumbani sasa!” Nilichanganyika, nikavaa haraka, nikatoka bila kumuaga, nikataka boda boda, nikaenda nyumbani.
Nilifika, Masai akasema, “Unashida gani leo?” Nikasema, “Niache, usiniulize!” Nikaingia ndani, nikawakuta Neema na Scott wamekaa kwenye sofa… Itaendelea.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

🔞 Onyo: Maudhui ya watu wazima (18+). Tafadhali soma kwa tahadhari. Zawadi Sehemu ya 13   >>> https://gonga94.com/semajambo/onyo-maudhui-ya-watu-wazima-18-tafadhali-soma-kwa-tahadhari-zawadi-sehemu-ya-13
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Pyar Ho Jane Dushman
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

RATIBA YA SIMULI ZETU

Ratiba ya Simulizi

  • USINITANGAZE 02 ❤❤ 05-08-2025 19:00

Ratiba ya Simulizi

  • USINITANGAZE 03 ❤❤ 06-08-2025 04:00

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest