Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

SEHEMU YA 55💘💘 Nilizani mwizi kumbe mmmmmmh ooooooooh my god 🤩🤩🤩🤩💔

5th Aug, 2025 Views 273



Usiku hakuna alielala wotee tulikuwa macho tunasubiri huo muda ufike wa mambo kufanyika ..

Tulikuwa wote kwenye chumba kimoja huwezi amini hakuna aliezungumza kitu yaan wote tulikuwa kimyaaa , nahisi kila mtu alikuwa na lake .

Nilikuwa naona kama miujiza yaani baada ya leo mie natembea naongea nacheka nitaweza kubeba watoto wangu nitamkumbatia Alex wangu afu tutafunga ndoaaa mungu wanguuu naona hata siwezi kusubiri zaidiii ,nilikuwa na hamu mnooo mnooo..

Muda ulifika bwana , yule mzee alikuja chumbani kwetu akasema muda tayari njoeni wote anaemtoa mgonjwa aje ki nyume nyuma asiangalie anapo enda mpaka nitakapo mwambia
Inno ndo alishika ki baskel changu akawa anakivuta kwa nyuma yaan mimi naangalia tunapo toka na hata yeye anaangalia tunapo toka Yule mzee anamuonesha njia ya kupita ...

Tulienda hivyo hivyo ki nyuma nyuma mpaka tulifika karibu na ule mti wa mbuyu
Ilikuwa ni usiku sana sana sanaa Giza lilikuwa kubwa panatishaa mi sauti ya ndege wadudu nilikuwa naogopa lakini ndo hivyo, jumlisha sijui jini mmh ndo kabisa nilizidi kuogopa aisee

Basi yule mzee akatuambia

"Kabla sijaanza kazi nataka kujaribu kuokoa wote , huyu mbuzi tutamtumia kama sadaka ya damu badala ya damu ya salma kama sadaka itakubaliwa basi juddy ataishi ila ikikataliwa basi sina njia tena ya kumsaidia Yule mtoto "

Wote walisema sawa ,Alex wangu alivyochoka kusikia jina la juddy aliona kama tu anapotezewa muda wake

Nilianza kupakwa ma unga unga usoni na vitu kama asali hivi , afu akachukua damu ilikuwa kwenye kibuyu hata sijui ya nini ile damu inanuka achaa
Nilimwagiwa kuanzia utosini kushuka chini
Yaan inanuka nusu nitapikeee ,nilikuwa najionea kinyaa mwenyewe, moyoni nasema jamani uchawi upo ,upo kabisa uchawi sijawahi kuona hichi kitu na wala sikuwahi kufikilia et ipo siku nitakutana nacho

Alichukua damu ingine akaanza kunipaka kwenye nyayo zangu za miguu akapaka na kwenye magoti yangu nyingi tu baada ya hapo

Ilichukuliwa zile shuka mbili nyekundu alizoleta Inno nikafunikwa mwili wote ,
Akawa ananichapa na yale sijui ni mikia ya ng'ombe ilee anaongea ongea ananichapa nayo anaongea ongea ananichapa nao , mkononi alikuwa na kibuyu tena cha damu anainywa afu ananitemea anaongea na maneno .
Nikawa najitikisa labda hata dawa zimeanza kufanya kazii , wapii mwili upo vile vile , zoezi lilitumia muda mrefu mnoooo mpaka nilikata tamaa mana hata dalili sikuwa nazo..

Mwili ulianza kutoa jasho jingiii, nilivuja jasho mpaka zile nguo zililowa zoteee , aliwaambia
"Nani mume wa huyu??"

"Mimi hapaaa" alijibu alex

"Basi wengine naomba msogee mbali kidogo ,"
Inno bwana akagoma kuondoka , yule mzee akasema haya kama unataka kuona Uchi wa shemeji yako , we njoo uanze kumtoa nguo"

Sikusikia tena sauti ya inno zaidi ya nyayo tu nikacheka inno bwana

Basi alex alikuja akanitoa yale mashuka yotee hapo najaribu tena kutikisika lakini hakuna kitu yaani nipo vile vile ..

Baada ya kutoa zile shuka akaambiwa anivue nguo zoteee , alex alinitoa nguo zangu zote nilibaki kama nilivyozaliwa .

Baada ya hapo yule mzee akachukua jembe dogo dogo akachimba sehemu hapakuwa hatua nyingi na nilipo kuwa nimeketi
Alichimba kidogo akatoa chupa frani hivi zile zinakuwaga na konyagi , akanambia niishike ndani ya hiyo chupa kulikuwa na Mdoli , mungu wa ajambu sana wakati huo kulikuwa kumeanza kukucha kuna mwanga mzuri japo sio sana niliiona yule mdoli ananguo yangu kabisa nilishtuka yaan nakumbuka vizuri sana nilikuwa na khanga ya hivi na sikuwahi kujua ilipo na hata sikufatilia sasa kuna kipande kidogo ndio amefungwa huyo mdoli ameshinewa kama ki gauni hivii

Niliishika ile chupa yule babu akachukua Yule mbuzi akamleta mbele yangu anaongea mengi maneno hata siyaelewi , akachukua mkuki zile nguo ambazo nilikuwa nimevaa mie et akavishwa yule mbuzi mhu jamani dunia ina mengi hii asikwambie mtu aiseee ..

Akaanza akamzunguka kama mara 6 hivi afu akamchoma ule mkuki mbuzi alianguka chini , hapo hapo alikufa mi nilishangaa mbona mbuzi amewahi sana kufaa kwa mkuki mmoja hata hajaangaika et

Baada ya yule mbuzi kuanguka chini yule mzee akanambia fungua hiyo chupa nikaifungua ulitoka kama moshi mweusiiiii ukapaa juu akanambia Njoo haraka hapaaa nikashangaa yaan nakuja vipi

Alex akataka kusukuma ile baskel yule babu akamwambia hapana ainuke hee nikashangaa , akanambia inuka haraka kabla hicho kilicho enda juu hakijarudi kinatafuta pa kwenda na kutarudi hapo hapo ulipo kaa

Weee kusikia hivyo nilijirusha mbele , yaan hapo naamini mie nguvu za kutembea sina bado ...

ITAENDELEA... hatari afu sio zile Boda boda yaan we unamiliki ki ISt afu unasema et una garii??
Hahha siwacheki jamani si unajua maskini akipata matako hulia bwata bwata bwataaa ndio mimi sasa yaan nilikuwa siamini kabisaa
Et namimi leo namiliki gari weuweeeee hahaha nilikuwa najiongelesha hatari yaan naongea maneno kama yote kucheka sasa hata sijui kwanini aisee

Baada ya kila kitu akalipia afu akanambia twende zetu hee sa na Gari yetuu?? , mwenzangu nilimuuliza hata sikuvunga alex alicheka akasema daah bora umeniulizia humu ndani
Embu twende bwana kwani mi nimekwambia hiyo ni gari yako
Woii ,nikasema embu kuwa Serious Serious bwana alex akasema kweli tenaaa hiyo sio yako
Alikuwa anaongea huku anacheka nikajua tu hiyo ni yangu ananitania nikajinunisha hapo , tukaenda zetu Home ..

Nilianza darasa kwa yule Doctor naingia Asubuhi mpaka sa 6 alex anakuja kunichukua Mi mawazo yangu ile gari nami nianze ku drive lakini sipewi hee wacha nimnunie alex yaaan nilinuna ile kidogo kidogo mpaka anisemeshe ndio najibu
Ye anacheka tu ananiuliza we una shida gani mbona umebadilika hivyo mi nasema hamna nipo sawa
Sa kusema nataka ile gari ndio hivyo tena naona aibuu atanicheka ...

Kule kwa Doctor nilikuwa nafanya maziezi ya Ubongo yaan naingizw kwenye mashine flani hivi humo ndani wanawasha mwanga mkubwa kweli mi nafumba macho

Ilikuwa ni zoezi la utambuzi wa namba, ilabu na zile Alfabet , yaan hiyo ilikuwa ni kuamsha ubongo , aisee wanajua wenyewe hukoo ila Niliona mwenyewe mabadiliko yangu makubwa sana

ITAENDELEA.....
Babie love.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

SEHEMU YA 55💘💘 Nilizani mwizi kumbe mmmmmmh ooooooooh my god 🤩🤩🤩🤩💔  >>> https://gonga94.com/semajambo/sehemu-ya-55-nilizani-mwizi-kumbe-mmmmmmh-ooooooooh-my-god
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

RATIBA YA SIMULI ZETU

Ratiba ya Simulizi

  • USINITANGAZE 02 ❤❤ 05-08-2025 19:00

Ratiba ya Simulizi

  • USINITANGAZE 03 ❤❤ 06-08-2025 04:00

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest